< 1 Nyakati 17 >

1 Baada ya Daudi kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, akamwambia nabii Nathani, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mierezi, wakati Sanduku la Agano la Bwana liko ndani ya hema.”
Or, comme David vivait tranquillement en sa demeure, il dit à Nathan, le prophète: "Vois, j’habite un palais de cèdre, et l’arche d’alliance du Seigneur est logée sous une tente!"
2 Nathani akamjibu Daudi, “Lolote ulilo nalo moyoni mwako litende, kwa maana Mungu yu pamoja nawe.”
Nathan répondit à David: "Tout ce qui est dans ta pensée, exécute-le, car le Seigneur est avec toi."
3 Usiku ule neno la Mungu likamjia Nathani, kusema:
Cependant cette nuit même, la parole de Dieu s’adressa ainsi à Nathan:
4 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Wewe hutanijengea mimi nyumba ili nikae humo.
"Va dire à David, mon serviteur: Ainsi a parlé l’Eternel: Ce n’est pas toi qui me construiras un temple pour ma résidence!
5 Mimi sijakaa ndani ya nyumba tangu siku ile niliyowatoa Israeli kutoka Misri mpaka leo. Nimehama kutoka hema moja hadi jingine na kutoka mahali pamoja hadi pengine.
Pourtant je n’ai pas demeuré dans un temple depuis le jour où je tirai Israël de l’Egypte jusqu’à ce jour, mais j’ai voyagé sous une tente et dans un pavillon.
6 Je, popote nilipokwenda pamoja na Waisraeli wote, wakati wowote nilimwambia kiongozi yeyote niliyemwagiza kuwachunga watu wangu, kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?’
Tout le temps que j’ai marché au milieu d’Israël, ai-je dit à un seul des Juges d’Israël que j’avais donnés pour pasteurs à mon peuple, ai-je dit: Pourquoi ne me bâtissez-vous pas une maison de cèdre?
7 “Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikuchukua machungani na kutoka kuandama kondoo ili uwatawale watu wangu Israeli.
Donc, parle de la sorte à mon serviteur David: Ainsi a parlé l’Eternel-Cebaot: Je t’ai tiré du bercail où tu gardais les brebis, pour que tu deviennes chef de mon peuple Israël.
8 Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
Je t’ai assisté dans toutes tes voies, j’ai détruit devant toi tous tes ennemis, et je t’ai fait un nom égal aux plus grands noms de la terre.
9 Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali na nitawapa ili wawe na mahali pao wenyewe pa kuishi na wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
J’Ai assigné à mon peuple Israël une résidence où je l’ai implanté et où il se maintiendra et ne sera plus inquiété; des gens pervers ne le molesteront plus comme précédemment.
10 na ambavyo wamefanya siku zote tangu nilipowachagua viongozi kwa ajili ya watu wangu Israeli. Pia nitawatiisha adui zenu wote. “‘Pamoja na hayo ninakuambia kwamba Bwana atakujengea nyumba:
Depuis l’époque où j’ai préposé des Juges à mon peuple, j’ai fait plier tous tes ennemis et je t’ai annoncé par là même que c’est l’Eternel qui t’érigera une maison.
11 Wakati wako utakapokuwa umekwisha, nawe ukawa umekwenda kukaa na baba zako, nitamwinua mzao wako aingie mahali pako kuwa mfalme, mmoja wa wana wako mwenyewe, nami nitaufanya imara ufalme wake.
Quand tes jours seront accomplis et que tu auras rejoint tes pères, j’élèverai à ta place ta progéniture un de tes fils et j’affermirai son empire.
12 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili yangu, nami nitakifanya imara kiti cha ufalme wake milele.
C’Est lui qui m’édifiera un temple, et moi, j’assurerai à jamais son trône.
13 Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Kamwe sitaondoa upendo wangu kwake, kama nilivyouondoa kwa yeye aliyekutangulia.
Je lui serai un père, et lui me sera un fils; je ne lui retirerai jamais ma grâce comme je l’ai retirée à celui qui t’a précédé.
14 Nitamweka juu ya nyumba yangu na ufalme wangu milele; kiti chake cha enzi nitakifanya imara milele.’”
Je le maintiendrai pour toujours dans ma maison et dans mon royaume, et son trône sera stable pour l’éternité."
15 Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
Toutes ces paroles et toute cette vision, Nathan les rapporta à David.
16 Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
Le roi David alla se mettre en présence du Seigneur et il dit: "Qui suis-je, Seigneur Dieu, et qu’est-ce que ma famille, pour que tu m’aies amené jusqu’ici?
17 Kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Mungu, umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Umeniangalia kama mtu aliyetukuka kuliko watu wote, Ee Bwana Mungu.
Encore était-ce trop peu à tes yeux, ô Dieu, et tu as annoncé, dans un lointain avenir, le sort de ma famille, me considérant comme un personnage de marque, Seigneur Dieu!
18 “Daudi aweza kukuambia nini zaidi kuhusu kumheshimu mtumishi wako? Kwa maana wewe unamjua mtumishi wako,
Que pourrait te dire encore de plus David sur l’honneur fait à ton serviteur? Ton serviteur, tu le connais bien!
19 Ee Bwana Mungu. Kwa ajili ya mtumishi wako, tena sawasawa na mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa sana na kujulisha ahadi hizi zote zilizo kubwa sana.
Seigneur, c’est en faveur de ton serviteur et selon ta volonté que tu as accompli ces grandes choses, de manière à faire connaître tous tes exploits.
20 “Hakuna aliye kama wewe, Ee Bwana Mungu, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe.
Seigneur, nul n’est comme toi, point de Dieu hormis toi, ainsi que nous l’avons entendu de nos oreilles.
21 Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli: taifa pekee duniani ambalo Mungu wake alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe na kujifanyia jina kwa ajili yake mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
Et y a-t-il comme ton peuple Israël une seule nation sur la terre que Dieu lui-même soit allé délivrer, pour en faire son peuple et t’assurer un nom grand et redoutable, en chassant des nations devant ton peuple que tu as délivré de l’Egypte?
22 Uliwafanya watu wako Israeli kuwa watu wako wewe mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana Mungu, umekuwa Mungu wao.
Tu t’es consacré ton peuple Israël comme un peuple à toi pour toujours, et toi, ô Eternel, tu es devenu son Dieu.
23 “Sasa basi, Bwana ahadi uliyoweka kuhusu mtumishi wako na nyumba yake na uithibitishe milele. Fanya kama ulivyoahidi,
Et maintenant, ô Seigneur, puisse la parole que tu as dite au sujet de ton serviteur et de sa maison se confirmer à tout jamais! Puisses-tu faire comme tu l’as dit!
24 ili ithibitike na jina lako litakuwa kuu milele. Kisha watu watasema, ‘Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu aliye juu ya Israeli, ndiye Mungu wa Israeli.’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itafanywa imara mbele zako.
Oui, qu’elle se réalise, et que ton nom soit exalté à jamais par cette parole: "L’Eternel-Cebaot, le Dieu d’Israël, est un Dieu puissant pour Israël!" Et que la maison de ton serviteur David se maintienne devant toi!
25 “Wewe, Mungu wangu, umemfunulia mtumishi wako Daudi kwamba utamjengea yeye nyumba. Hivyo mtumishi wako amekuwa na ujasiri wa kukuomba maombi haya.
Puisque toi-même, mon Dieu, tu as révélé à l’oreille de ton serviteur ta volonté de lui édifier une maison, ton serviteur s’est trouvé enhardi à t’adresser cette prière.
26 Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu! Umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
Or, Seigneur, tu es le vrai Dieu, et toi-même tu as promis ce bien à ton serviteur.
27 Basi imekupendeza kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu milele machoni pako; kwa ajili yako, Ee Bwana, umeibariki, nayo itabarikiwa milele.”
Veuille donc bénir la maison de ton serviteur: qu’elle subsiste constamment devant toi, puisque aussi bien, si toi, Eternel, tu la bénis, elle restera bénie à tout jamais!"

< 1 Nyakati 17 >