< 1 Nyakati 17 >

1 Baada ya Daudi kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, akamwambia nabii Nathani, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mierezi, wakati Sanduku la Agano la Bwana liko ndani ya hema.”
Kad se David nastanio u dvoru, rekao je proroku Natanu: “Pogledaj! Ja, evo, stojim u dvoru od cedrovine, a Kovčeg saveza Jahvina pod zavjesama!”
2 Nathani akamjibu Daudi, “Lolote ulilo nalo moyoni mwako litende, kwa maana Mungu yu pamoja nawe.”
Natan odgovori Davidu: “Što ti je god na srcu, čini, jer je Bog s tobom.”
3 Usiku ule neno la Mungu likamjia Nathani, kusema:
Ali još iste noći dođe Natanu ova Božja riječ:
4 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Wewe hutanijengea mimi nyumba ili nikae humo.
“Idi i reci mome sluzi Davidu: 'Ovako govori Jahve: Ti mi nećeš sagraditi kuće da prebivam u njoj.
5 Mimi sijakaa ndani ya nyumba tangu siku ile niliyowatoa Israeli kutoka Misri mpaka leo. Nimehama kutoka hema moja hadi jingine na kutoka mahali pamoja hadi pengine.
Nisam nikad prebivao u kući otkako sam izveo Izraela iz Egipta pa do današnjega dana, nego sam išao od šatora do šatora i od prebivališta do prebivališta.
6 Je, popote nilipokwenda pamoja na Waisraeli wote, wakati wowote nilimwambia kiongozi yeyote niliyemwagiza kuwachunga watu wangu, kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?’
Dok sam hodio sa svim Izraelom, jesam li ijednu riječ rekao nekom od Izraelovih sudaca, kojima sam zapovjedio da budu pastiri mojem narodu, i kazao: Zašto mi ne sagradite kuću od cedrovine?'
7 “Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikuchukua machungani na kutoka kuandama kondoo ili uwatawale watu wangu Israeli.
Zato sad ovo reci mome sluzi Davidu: 'Ovako govori Jahve nad vojskama: Ja sam te doveo s pašnjaka, od ovaca i koza, da budeš knez nad mojim izraelskim narodom.
8 Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
Bio sam s tobom kuda si god išao, iskorijenio sam sve tvoje neprijatelje pred tobom. Ja ću ti pribaviti veliko ime, kao što je velikaško ime na zemlji.
9 Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali na nitawapa ili wawe na mahali pao wenyewe pa kuishi na wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
Odredit ću prebivalište svome izraelskom narodu i posadit ću ga da živi na svojem mjestu i da ne luta više naokolo niti da ga zlikovci muče kao prije,
10 na ambavyo wamefanya siku zote tangu nilipowachagua viongozi kwa ajili ya watu wangu Israeli. Pia nitawatiisha adui zenu wote. “‘Pamoja na hayo ninakuambia kwamba Bwana atakujengea nyumba:
onda kad sam odredio suce nad svojim izraelskim narodom. Pokorit ću sve tvoje neprijatelje i učinit ću te velikim. Jahve će ti podići dom.
11 Wakati wako utakapokuwa umekwisha, nawe ukawa umekwenda kukaa na baba zako, nitamwinua mzao wako aingie mahali pako kuwa mfalme, mmoja wa wana wako mwenyewe, nami nitaufanya imara ufalme wake.
Jer kad se ispune tvoji životni dani i dođe vrijeme da počineš kod otaca, podići ću tvoga potomka nakon tebe, koji će biti između tvojih sinova, i utvrdit ću njegovo kraljevstvo.
12 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili yangu, nami nitakifanya imara kiti cha ufalme wake milele.
On će mi sagraditi dom, a ja ću utvrditi njegovo prijestolje zauvijek.
13 Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Kamwe sitaondoa upendo wangu kwake, kama nilivyouondoa kwa yeye aliyekutangulia.
Ja ću njemu biti otac, a on će meni biti sin: svoje naklonosti neću odvratiti od njega, kao što sam je odvratio od tvoga prethodnika.
14 Nitamweka juu ya nyumba yangu na ufalme wangu milele; kiti chake cha enzi nitakifanya imara milele.’”
Utvrdit ću ga u svojem domu i u svom kraljevstvu zauvijek, i prijestolje će mu čvrsto stajati zasvagda.'”
15 Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
Natan prenese Davidu sve te riječi i cijelo viđenje.
16 Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
Tada kralj David dođe i stade pred Jahvu i reče: “Tko sam ja, o Bože Jahve, i što je moj dom te si me doveo dovde?
17 Kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Mungu, umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Umeniangalia kama mtu aliyetukuka kuliko watu wote, Ee Bwana Mungu.
Pa i to je bilo premalo u tvojim očima, o Bože, nego si dao obećanja domu svoga sluge i za daleku budućnost i pogledao si na me kako se gleda na ugledna čovjeka, o Bože Jahve!
18 “Daudi aweza kukuambia nini zaidi kuhusu kumheshimu mtumishi wako? Kwa maana wewe unamjua mtumishi wako,
Pa što da ti još David govori o slavi tvoga sluge; tÓa ti poznaješ svoga slugu!
19 Ee Bwana Mungu. Kwa ajili ya mtumishi wako, tena sawasawa na mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa sana na kujulisha ahadi hizi zote zilizo kubwa sana.
Jahve, radi svoga sluge i po svome srcu učinio si sve ovo veliko djelo, obznanivši ove veličajnosti.
20 “Hakuna aliye kama wewe, Ee Bwana Mungu, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe.
Jahve, nema takvoga kakav si ti, niti ima Boga osim tebe, po svemu što smo ušima svojim čuli.
21 Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli: taifa pekee duniani ambalo Mungu wake alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe na kujifanyia jina kwa ajili yake mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
Postoji li ijedan narod na zemlji kao tvoj izraelski narod, radi kojega je Bog išao da ga izbavi sebi za narod, da tako stečeš sebi ime velikim i strašnim čudesima, izgoneći krivobožačka plemena pred svojim narodom koji si otkupio iz Egipta?
22 Uliwafanya watu wako Israeli kuwa watu wako wewe mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana Mungu, umekuwa Mungu wao.
Tako si učinio svoj izraelski narod svojim narodom zauvijek, a ti si mu, Jahve, postao Bogom.
23 “Sasa basi, Bwana ahadi uliyoweka kuhusu mtumishi wako na nyumba yake na uithibitishe milele. Fanya kama ulivyoahidi,
Zato sada, Jahve, neka bude čvrsta dovijeka riječ koju si dao svome sluzi i njegovu domu i učini kako si obrekao.
24 ili ithibitike na jina lako litakuwa kuu milele. Kisha watu watasema, ‘Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu aliye juu ya Israeli, ndiye Mungu wa Israeli.’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itafanywa imara mbele zako.
Neka bude čvrsta, da se veliča tvoje ime zauvijek i da se govori: Jahve nad vojskama, Izraelov Bog, jest Bog nad Izraelom, a dom tvoga sluge Davida neka stoji čvrsto pred tobom.
25 “Wewe, Mungu wangu, umemfunulia mtumishi wako Daudi kwamba utamjengea yeye nyumba. Hivyo mtumishi wako amekuwa na ujasiri wa kukuomba maombi haya.
Jer si ti, moj Bože, javio uhu svoga sluge da ćeš mu podići dom, zato je tvoj sluga smogao hrabrosti da se pomoli pred tobom.
26 Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu! Umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
Uistinu, Jahve, ti si Bog i ti si ovo lijepo obećanje dao svome sluzi.
27 Basi imekupendeza kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu milele machoni pako; kwa ajili yako, Ee Bwana, umeibariki, nayo itabarikiwa milele.”
Zato se sada udostoj blagosloviti dom svoga sluge da ostane dovijeka pred tobom, jer kad ti, Jahve, blagosloviš, bit će blagoslovljen zasvagda.”

< 1 Nyakati 17 >