< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
ASÍ trajeron el arca de Dios, y asentáronla en medio de la tienda que David había tendido para ella: y ofrecieron holocaustos y pacíficos delante de Dios.
2 Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
Y como David hubo acabado de ofrecer el holocausto y los pacíficos, bendijo al pueblo en el nombre de Jehová.
3 Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
Y repartió á todo Israel, así á hombres como á mujeres, á cada uno una torta de pan, y una pieza de carne, y un frasco de vino.
4 Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
Y puso delante del arca de Jehová ministros de los Levitas, para que recordasen, y confesasen, y loasen á Jehová Dios de Israel:
5 Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
Asaph el primero, el segundo después de él Zachârías, Jeiel, Semiramoth, Jehiel, Mathithías, Eliab, Benaías, Obed-edom, y Jehiel, con sus instrumentos de salterios y arpas; mas Asaph hacía sonido con címbalos:
6 nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
Benaías también y Jahaziel, sacerdotes, continuamente con trompetas delante del arca del pacto de Dios.
7 Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
Entonces, en aquel día, dió David principio á celebrar á Jehová por mano de Asaph y de sus hermanos:
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Confesad á Jehová, invocad su nombre, haced notorias en los pueblos sus obras.
9 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Cantad á él, cantadle salmos; hablad de todas sus maravillas.
10 Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Gloriaos en su santo nombre; alégrese el corazón de los que buscan á Jehová.
11 Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
Buscad á Jehová y su fortaleza; buscad su rostro continuamente.
12 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
Haced memoria de sus maravillas que ha obrado, de sus prodigios, y de los juicios de su boca,
13 enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Oh vosotros, simiente de Israel su siervo, hijos de Jacob, sus escogidos.
14 Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
Jehová, él es nuestro Dios; sus juicios en toda la tierra.
15 Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
Haced memoria de su alianza perpetuamente, y de la palabra que él mandó en mil generaciones;
16 agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
[Del pacto] que concertó con Abraham, y de su juramento á Isaac;
17 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
El cual confirmó á Jacob por estatuto, y á Israel por pacto sempiterno,
18 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
Diciendo: A ti daré la tierra de Canaán, suerte de vuestra herencia;
19 Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
Cuando erais pocos en número, pocos y peregrinos en ella;
20 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
Y andaban de nación en nación, y de un reino á otro pueblo.
21 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
No permitió que nadie los oprimiese: antes por amor de ellos castigó á los reyes.
22 “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
No toquéis, [dijo], á mis ungidos, ni hagáis mal á mis profetas.
23 Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Cantad á Jehová, toda la tierra, anunciad de día en día su salud.
24 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Cantad entre las gentes su gloria, y en todos los pueblos sus maravillas.
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Porque grande es Jehová, y digno de ser grandemente loado, y de ser temido sobre todos los dioses.
26 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Porque todos los dioses de los pueblos son nada: mas Jehová hizo los cielos.
27 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Poderío y hermosura delante de él; fortaleza y alegría en su morada.
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
Atribuid á Jehová, oh familias de los pueblos, atribuid á Jehová gloria y potencia.
29 mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Tributad á Jehová la gloria debida á su nombre: traed ofrenda, y venid delante de él; postraos delante de Jehová en la hermosura de su santidad.
30 Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
Temed en su presencia, toda la tierra: el mundo será aún establecido, para que no se conmueva.
31 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
Alégrense los cielos, y gócese la tierra, y digan en las naciones: Reina Jehová.
32 Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
Resuene la mar, y la plenitud de ella: alégrese el campo, y todo lo que contiene.
33 Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
Entonces cantarán los árboles de los bosques delante de Jehová, porque viene á juzgar la tierra.
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Celebrad á Jehová, porque es bueno; porque su misericordia es eterna.
35 Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
Y decid: Sálvanos, oh Dios, salud nuestra: júntanos, y líbranos de las gentes, para que confesemos tu santo nombre, y nos gloriemos en tus alabanzas.
36 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
Bendito sea Jehová Dios de Israel, de eternidad á eternidad. Y dijo todo el pueblo, Amén: y alabó á Jehová.
37 Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
Y dejó allí, delante del arca del pacto de Jehová, á Asaph y á sus hermanos, para que ministrasen de continuo delante del arca, cada cosa en su día:
38 Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
Y á Obed-edom y á sus hermanos, sesenta y ocho; y á Obed-edom hijo de Jeduthún, y á Asa, por porteros:
39 Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
Asimismo á Sadoc el sacerdote, y á sus hermanos los sacerdotes, delante del tabernáculo de Jehová en el alto que estaba en Gabaón,
40 ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
Para que sacrificasen continuamente, á mañana y tarde, holocaustos á Jehová en el altar del holocausto, conforme á todo lo que está escrito en la ley de Jehová, que él prescribió á Israel;
41 Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
Y con ellos á Hemán y á Jeduthún, y los otros escogidos declarados por sus nombres, para glorificar á Jehová, porque es eterna su misericordia;
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
Con ellos á Hemán y á Jeduthún con trompetas y címbalos para tañer, y con [otros] instrumentos de música de Dios; y á los hijos de Jeduthún, por porteros.
43 Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.
Y todo el pueblo se fué cada uno á su casa; y David se volvió para bendecir su casa.

< 1 Nyakati 16 >