< 1 Nyakati 16 >
1 Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
A gdy przynieśli arkę Boga i umieścili ją pośrodku namiotu wzniesionego przez Dawida, złożyli całopalenia i ofiary pojednawcze przed Bogiem.
2 Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
A gdy Dawid skończył składanie całopaleń i ofiar pojednawczych, błogosławił lud w imię PANA.
3 Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
I rozdał wszystkim Izraelitom, tak mężczyźnie, jak i kobiecie, po bochenku chleba i po kawałku mięsa oraz po bukłaku [wina].
4 Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
Ustanowił też niektórych Lewitów sługami przed arką PANA, aby wspominali i chwalili [go], i dziękowali PANU, Bogu Izraela:
5 Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
Asafa, naczelnika, a po nim Zachariasza, Jejela, Szemiramota, Jechiela, Mattitiasza, Eliaba, Benajasza i Obed-Edoma: Jejela [do gry] na instrumentach: cytrach i harfach, a Asafa – na cymbałach;
6 nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
A kapłanów Benajasza i Jachaziela, aby [stali] nieustannie z trąbami przed arką przymierza Boga.
7 Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
Wtedy w tym dniu Dawid postanowił po raz pierwszy, aby Asaf i jego bracia chwalili PANA [tym psalmem]:
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Wysławiajcie PANA, wzywajcie jego imienia, opowiadajcie między narodami sprawy jego.
9 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Śpiewajcie mu, śpiewajcie mu psalmy, rozmawiajcie o wszystkich jego cudach.
10 Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Chlubcie się jego świętym imieniem, niech się raduje serce szukających PANA.
11 Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
Szukajcie PANA i jego mocy, szukajcie zawsze jego oblicza.
12 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
Przypominajcie sobie dzieła, które czynił, jego cuda i wyroki jego ust.
13 enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Wy, potomkowie Izraela, jego sługi; wy, synowie Jakuba, jego wybrańcy!
14 Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
On [jest] PANEM, naszym Bogiem, jego sądy na całej ziemi.
15 Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
Pamiętajcie zawsze o jego przymierzu, o słowie, które nakazał po tysiąc pokoleń;
16 agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
[O przymierzu], które zawarł z Abrahamem, i o przysiędze złożonej Izaakowi.
17 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
Ustanowił je jako prawo dla Jakuba, jako wieczne przymierze dla Izraela;
18 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
Mówiąc: Tobie dam ziemię Kanaan jako dział waszego dziedzictwa;
19 Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
Kiedy było was niewielu, [byliście] nieliczni i obcy w niej.
20 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
I wędrowali od narodu do narodu, z jednego królestwa do innego ludu;
21 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
Nikomu nie pozwolił ich krzywdzić, nawet karcił królów z ich powodu, [mówiąc];
22 “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
Nie dotykajcie moich pomazańców, a moim prorokom nie czyńcie [nic] złego.
23 Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Śpiewaj PANU, cała ziemio, opowiadajcie dzień po dniu o jego zbawieniu.
24 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Głoście wśród narodów jego chwałę, pośród wszystkich ludów – jego cudowne dzieła;
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Wielki bowiem [jest] PAN i godny wszelkiej chwały, straszliwszy nad wszystkich bogów;
26 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Gdyż wszyscy bogowie narodów [są] bożkami, a PAN uczynił niebiosa.
27 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Chwała i cześć przed nim, moc i radość w jego przybytku.
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
Oddajcie PANU, rodziny narodów, oddajcie PANU chwałę i moc.
29 mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Oddajcie PANU chwałę jego imienia. Przynoście dary i przychodźcie przed jego oblicze. Oddajcie PANU pokłon w ozdobie świętości.
30 Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
Zadrżyj przed nim, cała ziemio. Świat będzie utwierdzony, aby się nie poruszył.
31 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
Niech się weselą niebiosa i niech się raduje ziemia, niech mówią wśród narodów: PAN króluje!
32 Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
Niech zaszumi morze i to, co je napełnia, niech radują się pola i wszystko, co [jest] na nich.
33 Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
Wtedy radośnie wykrzykną leśne drzewa przed PANEM, bo idzie, aby sądzić ziemię.
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Wysławiajcie PANA, bo jest dobry, bo jego miłosierdzie [trwa] na wieki.
35 Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
I mówcie: Zbaw nas, BOŻE naszego zbawienia, i zgromadź nas, i wybaw nas od pogan, abyśmy wielbili twoje święte imię i chlubili się twoją chwałą.
36 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
Błogosławiony PAN, Bóg Izraela, na wieki wieków. I cały lud powiedział: Amen i chwalił PANA.
37 Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
I [Dawid] zostawił tam przed arką przymierza PANA Asafa i jego braci, aby nieustannie pełnili służbę przed arką, według potrzeby każdego dnia;
38 Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
Także Obed-Edoma i ich braci, sześćdziesięciu ośmiu; a Obed-Edoma, syna Jedutuna, i Chosę [uczynił] odźwiernymi.
39 Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
Kapłana Sadoka i jego braci kapłanów [pozostawił] przed przybytkiem PANA na wyżynie w Gibeonie;
40 ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
Aby składali PANU nieustannie, rano i wieczorem, całopalenia na ołtarzu całopaleń, zgodnie ze wszystkim, co jest napisane w Prawie PANA, które nadał on Izraelowi;
41 Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
A z nimi [pozostawił] Hemana i Jedutuna oraz resztę wybranych, imiennie wyznaczonych, aby chwalili PANA, bo jego miłosierdzie [trwa] na wieki.
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
I u nich, u Hemana i Jedutuna, [pozostawił] trąby i cymbały dla grających na tych i na [innych] instrumentach muzycznych dla Boga. Synowie zaś Jedutuna [byli] odźwiernymi.
43 Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.
Potem cały lud się rozszedł, każdy do swego domu. Dawid też wrócił, aby błogosławić swojemu domowi.