< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
به این ترتیب بنی‌اسرائیل صندوق عهد را به خیمه‌ای که داوود برایش بر پا کرده بود، آوردند و در حضور خدا قربانیهای سوختنی و سلامتی تقدیم کردند.
2 Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
در پایان مراسم قربانی، داوود بنی‌اسرائیل را به نام خداوند برکت داد.
3 Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
سپس او به هر یک از زنان و مردان یک قرص نان، یک نان خرما و یک نان کشمشی داد.
4 Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
داوود بعضی از لاویان را تعیین کرد تا در جلوی صندوق عهد قرار گیرند و خداوند، خدای اسرائیل را با سرود شکر و سپاس بگویند. آنانی که برای این خدمت تعیین شدند اینها بودند:
5 Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
آساف (سرپرست این عده که سنج هم می‌نواخت)، زکریا، یعی‌ئیل، شمیراموت، یحی‌ئیل، مَتّیتیا، الی‌آب، بنایا، عوبید ادوم و یعی‌ئیل. این افراد عود و بربط می‌نواختند.
6 nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
بنایا و یحزی‌ئیل که کاهن بودند، همیشه در جلوی صندوق عهد شیپور می‌نواختند.
7 Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
در آن روز، داوود گروه سرایندگان را تشکیل داد تا در خیمهٔ عبادت برای شکر و سپاس خداوند سرود خوانند. آساف رهبر گروه سرایندگان بود. سرودی که آنها می‌خواندند این بود:
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
خداوند را شکر کنید و نام او را بخوانید؛ کارهای او را به تمام قومهای جهان اعلام نمایید.
9 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
در وصف او بسرایید و او را ستایش کنید؛ از کارهای شگفت‌انگیز او سخن بگویید.
10 Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
ای طالبان خداوند شادی نمایید و به نام مقدّس او فخر کنید!
11 Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
خداوند و قوت او را طالب باشید و پیوسته حضور او را بخواهید.
12 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
آیات و عجایبی را که به عمل آورده و فرامینی را که صادر کرده، به یاد آورید.
13 enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
ای فرزندان خادم او ابراهیم، ای پسران یعقوب، که برگزیدۀ او هستید.
14 Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
اوست یهوه، خدای ما! و عدالتش در تمام دنیا نمایان است.
15 Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
عهد او را همیشه به یاد داشته باشید عهدی که با هزاران پشت بسته است؛
16 agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
عهد او را با ابراهیم، و وعدهٔ او را به اسحاق!
17 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
او با یعقوب عهد بست و به اسرائیل وعده‌ای جاودانی داد.
18 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
او گفت: «سرزمین کنعان را به شما می‌بخشم تا ملک و میراثتان باشد.»
19 Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
بنی‌اسرائیل قومی کوچک بودند و در آن دیار غریب؛
20 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
میان قومها سرگردان بودند و از مملکتی به مملکتی دیگر رانده می‌شدند.
21 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
اما خداوند نگذاشت کسی به آنها صدمه برساند، و به پادشاهان هشدار داد که بر ایشان ظلم نکنند:
22 “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
«برگزیدگان مرا آزار ندهید! بر انبیای من دست ستم دراز نکنید!»
23 Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
ای مردم روی زمین، در وصف خداوند بسرایید! هر روز به مردم بشارت دهید که خداوند نجات می‌بخشد.
24 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
شکوه و جلال او را در میان ملتها ذکر کنید، و از معجزات او در میان قومها سخن بگویید.
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
زیرا خداوند بزرگ است و سزاوار ستایش! از او باید ترسید، بیش از همۀ خدایان.
26 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
خدایان سایر قومها بتهایی بیش نیستند، اما خداوند ما آسمانها را آفریده است.
27 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
شکوه و جلال در حضور اوست، و قدرت و شادمانی در خانه او.
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
ای تمام قومهای روی زمین، خداوند را توصیف نمایید؛ قدرت و شکوه او را توصیف نمایید؛
29 mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
عظمت نام خداوند را توصیف نمایید! با هدایا به حضورش بیایید. خداوند را در شکوه قدوسیتش بپرستید!
30 Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
ای تمام مردم روی زمین، در حضور او بلرزید. جهان پایدار است و تکان نخواهد خورد.
31 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
آسمان شادی کند و زمین به وجد آید. به همۀ قومها بگویید: «خداوند سلطنت می‌کند!»
32 Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
دریا و هر چه آن را پر می‌سازد غرش کند، صحرا و هر چه در آن است، به وجد آید.
33 Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
درختان جنگل با شادی بسرایند، در حضور خداوند که برای داوری جهان می‌آید.
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
خداوند را سپاس گویید، زیرا او نیکوست و محبتش ابدی.
35 Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
بگویید: «ای خدای نجات ما، ما را نجات ده. ما را از میان قومها جمع کن و برهان، تا نام مقدّس تو را سپاس گوییم و در ستایش تو فخر کنیم.»
36 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
متبارک باد یهوه، خدای اسرائیل، از ازل تا ابد. آنگاه همۀ قوم گفتند: «آمین» و خداوند را ستایش کردند.
37 Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
داوود ترتیبی داد که آساف و همکاران لاوی او به طور مرتب پیش صندوق عهد خداوند نگهداری می‌شد خدمت کنند و کارهای روزانهٔ آنجا را انجام دهند.
38 Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
عوبید ادوم (پسر یِدوتون) با شصت و هشت همکارش نیز به ایشان کمک می‌کردند. عوبید ادوم و حوسه مسئول نگهبانی از دروازه‌ها بودند.
39 Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
در ضمن خیمهٔ عبادت قدیمی که در بالای تپهٔ جبعون بود به همان صورت باقی ماند. داوود، صادوق کاهن و همکاران کاهن او را در آن خیمه گذاشت تا خداوند را در آنجا خدمت کنند.
40 ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
آنها هر روز صبح و عصر، روی مذبح، قربانیهای سوختنی به خداوند تقدیم می‌کردند، همان‌طور که خداوند در تورات به بنی‌اسرائیل فرموده بود.
41 Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
داوود هیمان و یِدوتون و چند نفر دیگر را هم که انتخاب شده بودند تعیین کرد تا خداوند را به خاطر محبت ابدی‌اش ستایش کنند.
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
آنها با نواختن شیپور و سنج و سایر آلات موسیقی، خدا را ستایش می‌کردند. پسران یِدوتون کنار دروازه می‌ایستادند.
43 Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.
پس از پایان مراسم، مردم به خانه‌هایشان رفتند و داوود بازگشت تا خانهٔ خود را تبرک نماید.

< 1 Nyakati 16 >