< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
Attulerunt igitur arcam Dei, et constituerunt eam in medio tabernaculi, quod tetenderat ei David: et obtulerunt holocausta, et pacifica coram Deo.
2 Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
Cumque complesset David offerens holocausta, et pacifica, benedixit populo in nomine Domini.
3 Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
Et divisit universis per singulos, a viro usque ad mulierem tortam panis, et partem assæ carnis bubalæ, et frixam oleo similam.
4 Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
Constituitque coram arca Domini de Levitis, qui ministrarent, et recordarentur operum eius, et glorificarent, atque laudarent Dominum Deum Israel:
5 Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
Asaph principem, et secundum eius Zachariam: Porro Iahiel, et Semiramoth, et Iehiel, et Mathathiam, et Eliab, et Banaiam, et Obededom: Iehiel super organa psalterii, et lyras: Asaph autem ut cymbalis personaret;
6 nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
Banaiam vero, et Iaziel sacerdotes, canere tuba iugiter coram arca fœderis Domini.
7 Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
In illo die fecit David principem ad confitendum Domino Asaph, et fratres eius.
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Confitemini Domino, et invocate nomen eius: notas facite in populis adinventiones eius.
9 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Cantate ei, et psallite ei: et narrate omnia mirabilia eius.
10 Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Laudate nomen sanctum eius: lætetur cor quærentium Dominum.
11 Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
Quærite Dominum, et virtutem eius: quærite faciem eius semper.
12 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
Recordamini mirabilium eius quæ fecit: signorum illius, et iudiciorum oris eius.
13 enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Semen Israel servi eius: filii Iacob electi eius.
14 Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
Ipse Dominus Deus noster: in universa terra iudicia eius.
15 Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
Recordamini in sempiternum pacti eius: sermonis, quem præcepit in mille generationes.
16 agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
Quem pepigit cum Abraham: et iuramenti illius cum Isaac.
17 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
Et constituit illud Iacob in præceptum: et Israel in pactum sempiternum,
18 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
dicens: Tibi dabo Terram Chanaan, funiculum hereditatis vestræ.
19 Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
Cum essent pauci numero, parvi et coloni eius.
20 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
Et transierunt de gente in gentem, et de regno ad populum alterum.
21 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
Non dimisit quemquam calumniari eos, sed increpavit pro eis reges.
22 “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
Nolite tangere Christos meos: et in prophetis meis nolite malignari.
23 Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Cantate Domino omnis terra, annunciate ex die in diem salutare eius.
24 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Narrate in gentibus gloriam eius: in cunctis populis mirabilia eius.
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Quia magnus Dominus, et laudabilis nimis: et horribilis super omnes deos.
26 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
Omnes enim dii populorum, idola: Dominus autem cælos fecit.
27 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Confessio et magnificentia coram eo: fortitudo et gaudium in loco eius.
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
Afferte Domino familiæ populorum: afferte Domino gloriam et imperium.
29 mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Date Domino gloriam, nomini eius, levate sacrificium, et venite in conspectu eius: et adorate Dominum in decore sancto.
30 Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
Commoveatur a facie eius omnis terra: ipse enim fundavit orbem immobilem.
31 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
Lætentur cæli, et exultet terra: et dicant in nationibus, Dominus regnavit.
32 Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
Tonet mare, et plenitudo eius: exultent agri, et omnia quæ in eis sunt.
33 Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
Tunc laudabunt ligna saltus coram Domino: quia venit iudicare terram.
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Confitemini Domino, quoniam bonus: quoniam in æternum misericordia eius.
35 Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
Et dicite: Salva nos Deus salvator noster; et congrega nos, et erue de gentibus, ut confiteamur nomini sancto tuo, et exultemus in carminibus tuis.
36 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
Benedictus Dominus Deus Israel ab æterno usque in æternum: et dicat omnis populo: Amen, et hymnum Domino.
37 Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
Reliquit itaque ibi coram arca fœderis Domini Asaph, et fratres eius, ut ministrarent in conspectu arcæ iugiter per singulos dies, et vices suas.
38 Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
Porro Obededom, et fratres eius sexaginta octo; et Obededom filium Idithun, et Hosa constituit ianitores.
39 Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
Sadoc autem sacerdotem, et fratres eius sacerdotes, coram tabernaculo Domini in excelso, quod erat in Gabaon,
40 ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
ut offerrent holocausta Domino super altare holocautomatis iugiter, mane et vespere, iuxta omnia quæ scripta sunt in lege Domini, quam præcepit Israeli.
41 Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
Et post eum Heman, et Idithun, et reliquos electos, unumquemque vocabulo suo ad confitendum Domino: Quoniam in æternum misericordia eius.
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
Heman quoque, et Idithun canentes tuba, et quatientes cymbala, et omnia musicorum organa ad canendum Deo; filios autem Idithun fecit esse portarios.
43 Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.
Reversusque est omnis populus in domum suam: et David, ut benediceret etiam domui suæ.

< 1 Nyakati 16 >