< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
Therfor thei brouyten the arke of God, and settiden it in the myddis of the tabernacle, that Dauid hadde araied therto; and thei offriden brent sacrifices and pesible sacrifices bifor the Lord.
2 Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
And whanne Dauid offrynge brent sacrifices and pesible sacrifices hadde fillid, he blesside the puple in the name of the Lord;
3 Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
and departide to alle to ech bi hym silf fro a man til to a womman o cake of breed, and a part of rostid fleisch of a bugle, and flour fried in oile.
4 Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
And he ordeynede bifor the arke of the Lord, of the Leuytis, that schulden mynystre, and haue mynde of the werkis of the Lord, and glorifie and preyse the Lord God of Israel;
5 Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
`he ordeynede Asaph the prince, and Zacharie his secounde; forsothe `he ordeynede Jahiel, and Semiramoth, and Jahel, and Mathathie, and Eliab, and Banaye, and Obededom, and Jehiel, on the orguns, on the sautrie, and on the harpis; but he ordeynede Asaph to sowne with cymbalis;
6 nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
sotheli he ordeynede Banaye and Aziel, preestis, bifor the arke of the boond of pees of the Lord, for to trumpe contynueli.
7 Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
In that dai Dauid made Asaph prince, and hise britheren, for to knowleche `to the Lord.
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Knowleche ye to the Lord, and inwardli clepe ye his name; make ye hise fyndyngis knowun among puplis.
9 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Synge ye to hym, and seie ye salm to hym, and telle ye alle his merueylis.
10 Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Preise ye his hooli name; the herte of men sekynge the Lord be glad.
11 Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
Seke ye the Lord and his vertu; seke ye euere his face.
12 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
Haue ye mynde of hise merueilis whiche he dide; of hise signes, and of the domes of his mouth.
13 enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
The seed of Israel, his seruaunt, preise thou God; the sones of Jacob, his chosun, preise ye God.
14 Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
He is `oure Lord God; hise domes ben in ech lond.
15 Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
Haue ye mynde with outen ende of his couenaunt; of the word whiche he couenauntide `in to a thousynde generaciouns.
16 agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
Which word he couenauntide with Abraham; and of his ooth to Ysaac.
17 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
And he ordeynede that to Jacob in to a comaundement; and to Israel in to euerlastynge couenaunt.
18 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
And seide, To thee Y schal yyue the lond of Canaan; the part of youre erytage.
19 Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
Whanne thei weren fewe in noumbre; litle, and pilgrims therof.
20 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
And thei passiden fro folk in to the folk; and fro a rewme to another puple.
21 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
He suffride not ony man falseli chalenge hem; but he blamyde kyngis for hem.
22 “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
Nyle ye touche my cristis; and nyle ye do wickidli ayens my prophetis.
23 Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Al erthe, singe ye to the Lord; telle ye fro dai into dai his helthe.
24 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Telle ye among hethen men his glorie; hise merueylis among alle puplis.
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For the Lord is greet, and worthi to be preisid ful myche; and he is orible, `ethir griseful, ouer alle goddis.
26 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For alle the goddis of puplis ben idols; but the Lord made heuenes.
27 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Knoulechyng and greet doyng ben bifor hym; strengthe and ioy ben in the place of hym.
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
Ye meynees of puplis, `bringe ye to the Lord; brynge ye to the Lord glorie and empire.
29 mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Yyue ye glorie to his name, reise ye sacrifice, and come ye in his siyt; and worschipe ye the Lord in hooli fairnesse.
30 Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
Al erthe be mouyd fro his face; for he foundide the world vnmouable.
31 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
Heuenes be glad, and the erthe `ioy fulli; and seie thei among naciouns, The Lord schal regne.
32 Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
The see thundre, and his fulnesse; the feeldis fulli ioye, and alle thingis that ben in tho.
33 Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
Thanne the trees of the forest schulen preyse bifor the Lord; for he cometh to deme the erthe.
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Knouleche ye to the Lord, for he is good; for his mersi is withouten ende.
35 Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
And seie ye, Thou God oure sauyour, saue vs, and gadere vs, and delyuere vs fro hethen men; that we knowleche to thin hooli name, and be fulli glade in thi songis.
36 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
Blessid be the Lord God of Israel fro with oute bigynnyng and til `in to with outen ende; and al the puple seie, Amen, and seie heriyng to God.
37 Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
Therfor Dauid lefte there, bifor the arke of boond of pees of the Lord, Asaph and hise britheren, for to mynystre in the siyt of the arke contynueli bi alle daies and her whilis.
38 Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
Forsothe he ordeynede porteris, Obededom and hise britheren, eiyte and sixti, and Obededom, the sone of Idithum, and Oza.
39 Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
Sotheli `he ordeynede Sadoch preest, and hise britheren, preestis bifor the tabernacle of the Lord, in the hiy place that was in Gabaon,
40 ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
for to offre brent sacrifices to the Lord on the auter of brent sacrifice contynueli, in the morwetid and euentid, bi alle thingis that ben writun in the lawe of the Lord, which he comaundide to Israel.
41 Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
And aftir hym Dauyd ordeynede Eman, and Idithum, and other chosene, ech man bi his name, for to knowleche to the Lord; for his mercy is withouten ende.
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
Also he ordeynede Eman, and Idithum, trumpynge, and schakynge cymbalis, and alle orguns of musikis, for to synge to God; forsothe he made the sones of Idithum to be portours, `ether bereris.
43 Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.
And al the puple turnede ayen in to her hows, and Dauid turnede ayen, to blesse also his hows.

< 1 Nyakati 16 >