< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
So they brought the ark of God, and set it in the midst of the tent, which David had pitched for it: and they offered holocausts, and peace offerings before God.
2 Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
And when David had made an end of offering holocausts, and peace offerings, he blessed the people in the name of the Lord.
3 Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
And he divided to all and every one, both men and women, a loaf of bread, and a piece of roasted beef, and flour fried with oil.
4 Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
And he appointed Levites to minister before the ark of the Lord, and to remember his works, and to glorify, and praise the Lord God of Israel.
5 Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
Asaph the chief, and next after him Zacharias: moreover Jahiel, and Semiramoth, and Jehiel, and Mathathias, and Eliab, and Banaias, and Obededom: and Jehiel over the instruments of psaltery, and harps: and Asaph sounded with cymbals:
6 nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
But Banaias, and Jaziel the priests, to sound the trumpet continually before the ark of the covenant of the Lord.
7 Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
In that day David made Asaph the chief to give praise to the Lord with his brethren.
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
Praise ye the Lord, and call upon his name: make known his doings among the nations.
9 Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Sing to him, yea, sing praises to him: and relate all his wondrous works.
10 Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
Praise ye his holy name: let the heart I of them rejoice, that seek the Lord.
11 Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
Seek ye the Lord, and his power: seek ye his face evermore.
12 Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
Remember his wonderful works, which he hath done: his signs, and the judgments of his mouth.
13 enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
O ye seed of Israel his servants, ye children of Jacob his chosen.
14 Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
He is the Lord our God: his judgments are in all the earth.
15 Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
Remember for ever his covenant: the word, which he commanded to a thousand generations.
16 agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
The covenant which he made with Abraham: and his oath to Isaac.
17 Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
And he appointed the same to Jacob for a precept: and to Israel for an everlasting covenant:
18 “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
Saying: To thee will I give the land of Chanaan: the lot of your inheritance.
19 Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
When they were but a small number: very few and sojourners in it.
20 walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
And they passed from nation to nation: and from a kingdom to another people.
21 Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
He suffered no man to do them wrong: and reproved kings for their sake.
22 “Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
Touch not my anointed: and do no evil to my prophets.
23 Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Sing ye to the Lord, all the earth: shew forth from day to day his salvation.
24 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Declare his glory among the Gentiles: his wonders among all people.
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For the Lord is great and exceedingly to be praised: and he is to be feared above all gods.
26 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For all the gods of the nations are idols: but the Lord made the heavens.
27 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Praise and magnificence are before him: strength and joy in his place.
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
Bring ye to the Lord, O ye families of the nations: bring ye to the Lord glory and empire.
29 mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Give to the Lord glory to his name, bring up sacrifice, and come ye in his sight: and adore the Lord in holy becomingness.
30 Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
Let all the earth be moved at his presence: for he hath founded the world immoveable.
31 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
Let the heavens rejoice, and the earth be glad: and let them say among the nations: The Lord hath reigned.
32 Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
Let the sea roar, and the fulness thereof: let the fields rejoice, and all things that are in them.
33 Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
Then shall the trees of the wood give praise before the Lord: because he is come to judge the earth.
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Give ye glory to the Lord, for he is good: for his mercy endureth for ever.
35 Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
And say ye: Save us, O God our saviour: and gather us together, and deliver us from the nations, that we may give glory to thy holy name, and may rejoice in singing thy praises.
36 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
Blessed be the Lord the God of Israel from eternity to eternity: and let all the people say Amen, and a hymn to God.
37 Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
So he left there before the ark of the covenant of the Lord, Asaph and his brethren to minister in the presence of the ark continually day by day, and in their courses.
38 Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
And Obededom, with his brethren sixty-eight: and Obededom the son of Idithun, and Hosa he appointed to be porters.
39 Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
And Sadoc the priest, and his brethren priests, before the tabernacle of the Lord in the high place, which was in Gabaon.
40 ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
That they should offer holocausts to the Lord upon the altar of holocausts continually, morning and evening, according to all that is written in the law of the Lord, which he commanded Israel.
41 Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
And after him Heman, and Idithun, and the rest that were chosen, every one by his name to give praise to the Lord: because his mercy endureth for ever.
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
And Heman and Idithun sounded the trumpet, and played on the cymbals, and all kinds of musical instruments to sing praises to God: and the sons of Idithun he made porters.
43 Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.
And all the people returned to their houses: and David to bless also his own house.

< 1 Nyakati 16 >