< 1 Nyakati 15 >

1 Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
Or [David] bâtit pour lui des maisons dans la Cité de David, et prépara un lieu pour l'Arche de Dieu; et lui tendit un tabernacle.
2 Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
Et David dit: L'Arche de Dieu ne doit être portée que par les Lévites; car l'Eternel les a choisis pour porter l'Arche de Dieu, et pour faire le service à toujours.
3 Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
David donc assembla tous ceux d'Israël à Jérusalem, pour amener l'Arche de l'Eternel dans le lieu qu'il lui avait préparé.
4 Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
David assembla aussi les enfants d'Aaron, et les Lévites.
5 Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
Des enfants de Kéhath, Uriël le Chef, et ses frères, six vingts.
6 Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
Des enfants de Mérari, Hasaïa le Chef, et ses frères, deux cent et vingt.
7 Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
Des enfants de Guersom, Joël le Chef, et ses frères, cent trente.
8 Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
Des enfants d'Elitsaphan, Sémahja le chef, et ses frères, deux cents.
9 Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
Des enfants de Hébron, Eliël le Chef, et ses frères, quatre-vingts.
10 Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
Des enfants de Huziël, Hamminadab le Chef et ses frères, cent et douze.
11 Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
David donc appela Tsadoc et Abiathar les Sacrificateurs, et ces Lévites-là, [savoir], Uriël, Hasaïa, Joël, Sémahja, Eliël, et Hamminadab;
12 Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
Et il leur dit: Vous qui êtes les Chefs des pères des Lévites, sanctifiez-vous, vous et vos frères; et transportez l'Arche de l'Eternel le Dieu d'Israël, au lieu que je lui ai préparé.
13 Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
Parce que vous n'y avez pas été la première fois, l'Eternel notre Dieu a fait une brèche entre nous; car nous ne l'avons pas recherché comme il est ordonné.
14 Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
Les Sacrificateurs donc et les Lévites se sanctifièrent pour amener l'Arche de l'Eternel, le Dieu d'Israël.
15 Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
Et les enfants des Lévites portèrent l'Arche de Dieu sur leurs épaules, avec les barres qu'ils avaient sur eux, comme Moïse l'avait commandé suivant la parole de l'Eternel.
16 Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
Et David dit aux Chefs des Lévites, d'établir quelques-uns de leurs frères qui chantassent avec des instruments de musique, [savoir] des musettes, des violons, et des cymbales, [et] qui fissent retentir leur voix avec joie.
17 Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
Les Lévites donc établirent Héman fils de Joël, et d'entre ses frères, Asaph fils de Bérécia; et des enfants de Mérari, qui étaient leurs frères, Ethan fils de Kusaïa;
18 hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
Et avec eux leurs frères pour être au second rang, Zacharie, Ben, Jahaziël, Sémiramoth, Jéhiël, Hunni, Eliab, Bénéja, Mahaséïa, Mattitia, et Eliphaléhu, Miknéïa, Hobed-Edom, et Jéhiël, portiers.
19 Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
Et quant à Héman, Asaph, et Ethan chantres, [ils sonnaient] des cymbales d'airain, en faisant retentir [leur voix].
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
Et Zacharie, Haziël, Sémiramoth, Jéhiël, Hunni, Eliab, Mahaséïa, et Bénéja jouaient de la musette, sur Halamoth.
21 na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
Et Mattitia, Eliphaléhu, Miknéja, Hobed-Edom, Jéhiël, [et] Hazaria jouaient des violons sur l'octave, pour renforcer le ton.
22 Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
Mais Kénaïa, le principal des Lévites avait la charge de faire porter l'Arche, enseignant comment il la fallait porter; car il était homme fort intelligent.
23 Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
Et Bérécia et Elkana, étaient portiers pour l'Arche.
24 Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
Et Sébania, Jéhosaphat, Nathanaël, Hamasaï, Zacharie, Bénéja, Elihézer, Sacrificateurs, sonnaient des trompettes devant l'Arche de Dieu, et Hobed-Edom et Jéhïa étaient portiers pour l'Arche.
25 Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
David donc et les Anciens d'Israël, avec les Gouverneurs de milliers, marchaient, amenant avec joie l'Arche de l'alliance de l'Eternel, de la maison d'Hobed-Edom.
26 Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
Et selon que Dieu soulageait les Lévites qui portaient l'Arche de l'alliance de l'Eternel, on sacrifiait sept veaux et sept béliers.
27 Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
Et David était vêtu d'un éphod de fin lin; et tous les Lévites aussi qui portaient l'Arche, et les chantres; et Kénaïa, qui avait la principale charge de faire porter l'Arche, était avec les chantres; et David avait un éphod de lin.
28 Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
Ainsi tout Israël amena l'Arche de l'alliance de l'Eternel, avec de grands cris de joie, et au son du cor, des trompettes et des cymbales, faisant retentir [leur voix] avec des musettes et des violons.
29 Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.
Mais il arriva, comme l'Arche de l'alliance de l'Eternel entrait dans la Cité de David, que Mical fille de Saül, regardant par la fenêtre, vit le Roi David sautant et jouant, et elle le méprisa dans son cœur.

< 1 Nyakati 15 >