< 1 Nyakati 15 >

1 Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
David se fit des maisons dans la cité de David; il prépara un emplacement pour l'arche de Dieu et dressa une tente pour elle.
2 Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
David dit alors: « Personne ne doit porter l'arche de Dieu, sinon les Lévites. Car Yahvé les a choisis pour porter l'arche de Dieu et pour le servir à jamais. »
3 Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
David rassembla tout Israël à Jérusalem, pour faire monter l'arche de l'Éternel à la place qu'il lui avait préparée.
4 Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
David rassembla les fils d'Aaron et les Lévites:
5 Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
des fils de Kehath, Uriel le chef, et ses frères, cent vingt;
6 Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
des fils de Merari, Asaja le chef, et ses frères, deux cent vingt;
7 Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
des fils de Guershom, Joël le chef, et ses frères, cent trente;
8 Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
des fils d'Elizaphan, Schemaeja, le chef, et ses frères, deux cents;
9 Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
des fils d'Hébron, Éliel, le chef, et ses frères, quatre-vingts;
10 Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
des fils d'Uzziel, Amminadab, le chef, et ses frères, cent douze.
11 Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
David appela les prêtres Tsadok et Abiathar, et les Lévites: Uriel, Asaja, Joël, Schemaeja, Éliel et Amminadab,
12 Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
et leur dit: « Vous êtes les chefs de famille des Lévites. Sanctifiez-vous, vous et vos frères, afin que vous puissiez porter l'arche de Yahvé, le Dieu d'Israël, jusqu'au lieu que j'ai préparé pour elle.
13 Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
Car, parce que vous ne l'avez pas portée d'abord, Yahvé notre Dieu s'est mis en colère contre nous, parce que nous ne l'avons pas cherché selon l'ordonnance. »
14 Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
Ainsi, les prêtres et les lévites se sanctifièrent pour faire monter l'arche de l'Yahvé, le Dieu d'Israël.
15 Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
Les fils des lévites portèrent l'arche de Dieu sur leurs épaules avec ses barres, comme Moïse l'avait ordonné, selon la parole de l'Éternel.
16 Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
David dit au chef des Lévites de désigner leurs frères comme chanteurs avec des instruments de musique, des instruments à cordes, des harpes et des cymbales, pour qu'ils sonnent à haute voix et élèvent la voix avec joie.
17 Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
Les Lévites nommèrent Héman, fils de Joël, et, parmi ses frères, Asaph, fils de Bérékia, et parmi les fils de Merari, leurs frères, Ethan, fils de Kushaïa,
18 hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
et avec eux leurs frères de second rang: Zacharie, Ben, Jaaziel, Shemiramoth, Jehiel, Unni, Eliab, Benaja, Maaséja, Mattithia, Eliphelehu, Miknéja, Obed-Edom et Jeiel, les portiers.
19 Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
Les chantres, Héman, Asaph et Éthan, reçurent des cymbales d'airain pour sonner à haute voix;
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
Zacharie, Aziel, Schemiramoth, Jehiel, Unni, Éliab, Maaséja et Benaja, avec des instruments à cordes accordés sur Alamoth;
21 na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
et Mattithia, Élipheléhu, Miknéja, Obed-Édom, Jeiel et Azazia, avec des harpes accordées sur la lyre à huit cordes, pour diriger.
22 Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
Chenania, chef des lévites, dirigeait les chants. Il enseignait les chanteurs, car il était habile.
23 Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
Bérékia et Elkana étaient portiers de l'arche.
24 Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
Les prêtres, Schebania, Josaphat, Nethaneel, Amasaï, Zacharie, Benaja et Eliezer, sonnaient des trompettes devant l'arche de Dieu; Obed-Edom et Jehia étaient portiers de l'arche.
25 Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
David, les anciens d'Israël et les chefs de milliers allèrent faire monter l'arche de l'alliance de l'Yahvé de la maison d'Obed-Edom avec joie.
26 Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
Lorsque Dieu aida les Lévites qui portaient l'arche de l'alliance de Yahvé, ils sacrifièrent sept taureaux et sept béliers.
27 Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
David était revêtu d'une robe de fin lin, ainsi que tous les Lévites qui portaient l'arche, les chantres, et Chenania, le chef de chœur, avec les chantres; et David avait sur lui un éphod de lin.
28 Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
Tout Israël fit monter l'arche de l'alliance de Yahvé en poussant des cris de joie, au son de la cornemuse, des trompettes et des cymbales, et en faisant retentir à haute voix les instruments à cordes et les harpes.
29 Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.
Comme l'arche de l'alliance de Yahvé arrivait à la ville de David, Mical, fille de Saül, regarda par la fenêtre et vit le roi David danser et jouer; elle le méprisa dans son cœur.

< 1 Nyakati 15 >