< 1 Nyakati 15 >

1 Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
Ja hän rakensi itsellensä taloja Daavidin kaupunkiin ja valmisti paikan Jumalan arkille ja pystytti sille majan.
2 Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
Silloin Daavid käski: "Älkööt muut kuin leeviläiset kantako Jumalan arkkia; sillä heidät on Herra valinnut kantamaan Jumalan arkkia ja palvelemaan häntä ikuisesti".
3 Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
Ja Daavid kokosi kaiken Israelin Jerusalemiin, tuomaan Herran arkkia siihen paikkaan, jonka hän oli sille valmistanut.
4 Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
Daavid kokosi Aaronin jälkeläiset ja leeviläiset;
5 Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
Kehatin jälkeläisistä: Uurielin, päämiehen, ja hänen veljensä, sata kaksikymmentä;
6 Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
Merarin jälkeläisistä: Asajan, päämiehen, ja hänen veljensä, kaksisataa kaksikymmentä;
7 Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
Geersomin jälkeläisistä: Jooelin, päämiehen, ja hänen veljensä, sata kolmekymmentä;
8 Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
Elisafanin jälkeläisistä: Semajan, päämiehen, ja hänen veljensä, kaksisataa;
9 Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
Hebronin jälkeläisistä: Elielin, päämiehen, ja hänen veljensä, kahdeksankymmentä;
10 Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
Ussielin jälkeläisistä: Amminadabin, päämiehen, ja hänen veljensä, sata kaksitoista.
11 Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
Ja Daavid kutsui papit Saadokin ja Ebjatarin sekä leeviläiset Uurielin, Asajan, Jooelin, Semajan, Elielin ja Amminadabin
12 Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
ja sanoi heille: "Te olette leeviläisten perhekuntien päämiehet. Pyhittäkää itsenne ja veljenne ja tuokaa Herran, Israelin Jumalan, arkki siihen paikkaan, jonka minä olen sille valmistanut.
13 Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
Sillä sentähden, ettette ensimmäisellä kerralla olleet läsnä, mursi Herra, meidän Jumalamme, meidät; sillä me emme etsineet häntä, niinkuin olisi pitänyt."
14 Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
Silloin papit ja leeviläiset pyhittäytyivät tuomaan Herran, Israelin Jumalan, arkkia.
15 Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
Ja leeviläiset kantoivat Jumalan arkkia korennoilla olallansa, niinkuin Mooses oli Herran sanan mukaan käskenyt.
16 Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
Ja Daavid käski leeviläisten päämiesten asettaa veljensä, veisaajat, soittimilla, harpuilla, kanteleilla ja kymbaaleilla kaiuttamaan riemuvirsiä.
17 Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
Niin leeviläiset asettivat soittamaan Heemanin, Jooelin pojan, ja hänen heimolaisistaan Aasafin, Berekjan pojan, ja heidän heimolaisistaan, Merarin jälkeläisistä, Eetanin, Kuusajan pojan,
18 hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
ja heidän kanssaan heidän arvossa lähinnä olevista heimolaisistaan: Sakarjan, Benin ja Jaasielin, Semiramotin, Jehielin, Unnin, Eliabin, Benajan, Maasejan, Mattitjan, Elifelehun, Miknejan, Oobed-Edomin ja Jegielin, ovenvartijat.
19 Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
Ja veisaajista oli Heemanin, Aasafin ja Eetanin soitettava vaskikymbaaleilla,
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
Sakarjan, Ussielin, Semiramotin, Jehielin, Unnin, Eliabin, Maasejan ja Benajan harpuilla korkeassa äänialassa,
21 na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
Mattitjan, Elifelehun, Miknejan, Oobed-Edomin, Jegielin ja Asasjan kanteleilla matalassa äänialassa, veisuuta johtaaksensa.
22 Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
Kenanja, leeviläisten johtaja kantajatehtävässä, valvoi kantamista, sillä hän oli taitava siihen.
23 Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
Berekja ja Elkana olivat arkin ovenvartijat.
24 Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
Ja papit Sebanja, Joosafat, Netanel, Amasai, Sakarja, Benaja ja Elieser puhalsivat torviin Jumalan arkin edellä, ja Oobed-Edom ja Jehia olivat arkin ovenvartijat.
25 Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
Sitten Daavid, Israelin vanhimmat ja tuhannenpäämiehet menivät ja toivat riemuiten Herran liitonarkin Oobed-Edomin talosta.
26 Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
Ja kun Jumala auttoi leeviläisiä, jotka kantoivat Herran liitonarkkia, uhrattiin seitsemän härkää ja seitsemän oinasta.
27 Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
Daavid oli puettu hienosta pellavakankaasta tehtyyn viittaan ja samoin kaikki leeviläiset, jotka kantoivat arkkia, sekä veisaajat ja kantamisen johtaja Kenanja veisaajain kanssa; ja Daavidilla oli yllään pellavakasukka.
28 Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
Niin koko Israel toi Herran liitonarkin riemun raikuessa ja pasunain pauhatessa, torvien, kymbaalien, harppujen ja kannelten soidessa.
29 Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.
Kun Herran liitonarkki tuli Daavidin kaupunkiin, katseli Miikal, Saulin tytär, ikkunasta, ja nähdessään kuningas Daavidin hyppivän ja karkeloivan halveksi hän häntä sydämessään.

< 1 Nyakati 15 >