< 1 Nyakati 15 >

1 Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
And he made for himself houses in [the] city of David and he prepared a place for [the] ark of God and he pitched for it a tent.
2 Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
Then he said David not to carry [the] ark of God that except the Levites for them - he had chosen Yahweh to carry [the] ark of Yahweh and to serve him until perpetuity.
3 Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
And he assembled David all Israel to Jerusalem to bring up [the] ark of Yahweh to place its which he had prepared for it.
4 Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
And he gathered David [the] descendants of Aaron and the Levites.
5 Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
Of [the] descendants of Kohath Uriel the leader and relatives his one hundred and twenty.
6 Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
Of [the] descendants of Merari Asaiah the leader and relatives his two hundred and twenty.
7 Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
Of [the] descendants of Gershom Joel the leader and relatives his one hundred and thirty.
8 Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
Of [the] descendants of Elizaphan Shemaiah the leader and relatives his two hundred.
9 Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
Of [the] descendants of Hebron Eliel the leader and relatives his eighty.
10 Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
Of [the] descendants of Uzziel Amminadab the leader and relatives his one hundred and two [plus] ten.
11 Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
And he summoned David Zadok and Abiathar the priests and the Levites Uriel Asaiah and Joel Shemaiah and Eliel and Amminadab.
12 Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
And he said to them you [are] [the] chiefs of the fathers of the Levites consecrate yourselves you and relatives your and you will bring up [the] ark of Yahweh [the] God of Israel to [where] I have prepared for it.
13 Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
For to what? at the first [time] not you he burst out Yahweh God our against us for not we sought him according to the ordinance.
14 Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
And they consecrated themselves the priests and the Levites to bring up [the] ark of Yahweh [the] God of Israel.
15 Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
And they carried [the] descendants of the Levites [the] ark of God just as he had commanded Moses according to [the] word of Yahweh on shoulders their with poles on them.
16 Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
And he said David to [the] leaders of the Levites to appoint relatives their the singers with instruments of song lyres and harps and cymbals sounding aloud to raise a sound of joy.
17 Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
And they appointed the Levites Heman [the] son of Joel and of relatives his Asaph [the] son of Berekiah. And of [the] descendants of Merari relatives their Ethan [the] son of Kushaiah.
18 hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
And with them relatives their the second in rank Zechariah Ben and Jaaziel and Shemiramoth and Jehiel - and Unni Eliab and Benaiah and Maaseiah and Mattithiah and Eliphelehu and Mikneiah and Obed-Edom and Jeiel the gatekeepers.
19 Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
And the singers Heman Asaph and Ethan with cymbals bronze [were] to sound aloud.
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
And Zechariah and Aziel and Shemiramoth and Jehiel and Unni and Eliab and Maaseiah and Benaiah with lyres on alamoth.
21 na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
And Mattithiah and Eliphelehu and Mikneiah and Obed-Edom and Jeiel and Azaziah with harps on the sheminith to act as overseers.
22 Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
And Kenaniah [the] leader of the Levites in a lifting up an instructor in the lifting up for [was] a teacher he.
23 Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
And Berekiah and Elkanah [were] gatekeepers for the ark.
24 Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
And Shebaniah and Joshaphat and Nethanel and Amasai and Zechariah and Benaiah and Eliezer the priests ([were] blowing a trumpet *Q(k)*) on trumpets before [the] ark of God and Obed-Edom and Jehiah [were] gatekeepers for the ark.
25 Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
And it was David and [the] elders of Israel and [the] leaders of the thousands [were] the [ones who] went to bring up [the] ark of [the] covenant of Yahweh from [the] house of Obed-Edom with joy.
26 Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
And it was because helped God the Levites [the] bearers of [the] ark of [the] covenant of Yahweh and they sacrificed seven young bulls and seven rams.
27 Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
And David [was] wrapped - in a robe of fine linen and all the Levites who were carrying the ark and the singers and Kenaniah the leader the lifting up the singers and [was] on David an ephod of linen.
28 Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
And all Israel [was] bringing up [the] ark of [the] covenant of Yahweh with a shout and with [the] sound of a ram's horn and with trumpets and with cymbals sounding aloud with lyres and harps.
29 Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.
And it was [the] ark of [the] covenant of Yahweh [was] coming to [the] city of David and Michal [the] daughter of Saul she looked down - through the window and she saw the king David dancing and making merry and she despised him in heart her.

< 1 Nyakati 15 >