< 1 Nyakati 15 >

1 Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
And he makes houses for himself in the City of David, and prepares a place for the Ark of God, and stretches out a tent for it.
2 Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
Then David said, “None [are] to carry the Ark of God, except the Levites, for YHWH has fixed on them to carry the Ark of God and to serve Him for all time.”
3 Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
And David assembles all Israel to Jerusalem, to bring up the Ark of YHWH to its place that he had prepared for it.
4 Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
And David gathers the sons of Aaron and the Levites—
5 Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
of sons of Kohath: Uriel the chief and one hundred and twenty of his brothers;
6 Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
of sons of Merari: Asaiah the chief and two hundred and twenty of his brothers;
7 Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
of sons of Gershom: Joel the chief and one hundred and thirty of his brothers;
8 Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
of sons of Elizaphan: Shemaiah the chief and two hundred of his brothers;
9 Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
of sons of Hebron: Eliel the chief and eighty of his brothers;
10 Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
of sons of Uzziel: Amminadab the chief and one hundred and twelve of his brothers.
11 Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
And David calls to Zadok and to Abiathar the priests, and to the Levites, to Uriel, Asaiah, and Joel, Shemaiah, and Eliel, and Amminadab,
12 Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
and says to them, “You [are] heads of the fathers of the Levites; sanctify yourselves, you and your brothers, and you have brought up the Ark of YHWH, God of Israel, to [the place] I have prepared for it;
13 Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
because you [did] not [do it] at the first, our God YHWH made a breach on us, because we did not seek Him according to the ordinance.”
14 Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
And the priests and the Levites sanctify themselves to bring up the Ark of YHWH, God of Israel;
15 Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
and sons of the Levites carry the Ark of God, as Moses commanded, according to the word of YHWH, above them with poles on their shoulder.
16 Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
And David says to the heads of the Levites to appoint their brothers the singers, with instruments of song, psalteries, and harps, and cymbals, sounding, to lift up with the voice for joy.
17 Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
And the Levites appoint Heman son of Joel, and of his brothers, Asaph son of Berechiah, and of the sons of Merari their brothers, Ethan son of Kushaiah;
18 hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
and with them their brothers, the seconds [in rank]: Zechariah, Ben, and Jaaziel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Unni, Eliab, and Benaiah, and Maaseiah, and Mattithiah, and Elipheleh, and Mikneiah; and Obed-Edom and Jeiel the gatekeepers;
19 Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
and the singers, Heman, Asaph, and Ethan, [are] to sound with cymbals of bronze;
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
and Zechariah, and Aziel, and Shemiramoth, and Jeheil, and Unni, and Eliab, and Maaseiah, and Benaiah, with psalteries over the girls’ [voices],
21 na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
and Mattithiah, and Elipheleh, and Mikneiah, and Obed-Edom, and Jeiel, and Azaziah, to oversee with harps on the eighth.
22 Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
And Chenaniah, head of the Levites, [is] over the burden; he instructs about the burden, for he [is] intelligent.
23 Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
And Berechiah and Elkanah [are] gatekeepers for the Ark.
24 Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
And Shebaniah, and Joshaphat, and Nethaneel, and Amasai, and Zechariah, and Benaiah, and Eliezer the priests, are blowing with trumpets before the Ark of God; and Obed-Edom and Jehiah [are] gatekeepers for the Ark.
25 Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
And it is David, and [the] elderly of Israel, and the heads of the thousands, who are going to bring up the Ark of the Covenant of YHWH from the house of Obed-Edom with joy;
26 Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
and it comes to pass, in God’s helping the Levites carrying the Ark of the Covenant of YHWH, that they sacrifice seven bullocks and seven rams.
27 Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
And David is wrapped in an upper robe of fine linen, and all the Levites who are carrying the Ark, and the singers, and Chenaniah head of the burden of the singers; and an Ephod of linen [is] on David.
28 Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
And all of Israel is bringing up the Ark of the Covenant of YHWH with shouting, and with the sound of a horn, and with trumpets, and with cymbals, sounding with psalteries and harps,
29 Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.
and it comes to pass, the Ark of the Covenant of YHWH is entering into the City of David, and Michal daughter of Saul is looking through the window, and sees King David dancing and playing, and despises him in her heart.

< 1 Nyakati 15 >