< 1 Nyakati 15 >

1 Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
Onda je David sazidao dvore u Davidovu gradu, pripravio mjesto za Kovčeg Božji i razapeo mu Šator.
2 Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
Potom je rekao David: “Ne smije nositi Kovčeg Božji nitko osim levita, jer je njih izabrao Jahve da nose Kovčeg Jahvin i da mu služe dovijeka.”
3 Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
David je sakupio sav Izrael u Jeruzalem da prenesu Kovčeg Jahvin gore na njegovo mjesto koje mu bijaše pripravio.
4 Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
Skupio je David i Aronove sinove i levite.
5 Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
Od Kehatovih sinova: kneza Uriela i sto dvadeset njegove braće;
6 Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
od Merarijevih sinova: kneza Asaju i dvjesta dvadeset njegove braće;
7 Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
od Geršomovih sinova: kneza Joela i sto trideset njegove braće.
8 Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
Od Elisafanovih sinova: kneza Šemaju i dvjesta njegove braće.
9 Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
Od Hebronovih sinova: kneza Eliela i osamdeset njegove braće;
10 Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
od Uzielovih sinova: kneza Aminadaba i sto dvanaest njegove braće.
11 Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
Tada David pozva svećenike Sadoka i Ebjatara i levite Uriela, Asaju, Joela, Šemaju, Eliela i Aminadaba,
12 Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
pa im reče: “Vi ste glavari levitskih porodica; posvetite sebe i svoju braću da prenesete gore Kovčeg Jahve, Izraelova Boga, na mjesto koje sam mu pripravio.
13 Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
Jer nas je pobio Jahve, Bog naš, zato što prvi put vi niste bili nazočni i što ga nismo tražili onako kako je trebalo.”
14 Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
Posvetiše se tada svećenici i leviti da prenesu gore Kovčeg Jahve, Izraelova Boga.
15 Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
Levitski su sinovi ponijeli Božji Kovčeg, na svojim ramenima, o motkama, kako je zapovjedio Mojsije po Jahvinoj riječi.
16 Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
Tada David reče levitskim knezovima da između svoje braće postave pjevače s glazbalima, s harfama, citrama i cimbalima da se čuje i da gromko odjekuje radosno pjevanje.
17 Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
Leviti su postavili Joelova sina Hemana, a od njegove braće Berekjina sina Asafa, i od njihove braće, Merarijevih sinova, Kušajina sina Etana.
18 hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
S njima njihovu braću drugoga reda: Zahariju, sina Jaazielova, Šemiramota, Jehiela, Unija, Eliaba, Benaju, Maaseju, Matitju, Eliflehua, Mikneju, Obed Edoma i Jeiela, vratare.
19 Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
A pjevači, Heman, Asaf i Etan gromko su udarali u mjedene cimbale.
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
A Zaharija, Uziel, Šemiramot, Jehiel, Uni, Eliab, Maaseja i Benaja u harfe s visokim zvucima;
21 na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
a Matitja, Eliflehu, Mikneja, Obed Edom, Jeiel i Azazja u citre, u osminskoj pratnji.
22 Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
Kenanja, knez onih levita koji su nosili Kovčeg, upravljao je prenošenjem jer je bio vješt u tome.
23 Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
Berekja i Elkana bili su vratari kod Kovčega.
24 Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
Šebanija, Jošafat, Netanel, Amasaj, Zaharija, Benaja i Eliezer, svećenici, trubili su u trube pred Božjim Kovčegom; Obed Edom i Jehija bili su vratari kod Kovčega.
25 Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
Tako je David s izraelskim starješinama i tisućnicima radosno išao prenoseći gore Kovčeg saveza Jahvina iz Obed-Edomove kuće.
26 Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
Kad je Bog pomogao levitima koji su nosili Kovčeg saveza Jahvina, žrtvovali su sedam junaca i sedam ovnova.
27 Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
David bijaše ogrnut plaštem od tanka platna, a tako i svi leviti što su nosili Kovčeg, kao i pjevači i Kenanija koji je upravljao pjevačima. David je imao na sebi lanen oplećak.
28 Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
Tako je sav Izrael prenosio gore Kovčeg saveza Jahvina, radosno kličući uz jeku rogova, truba i cimbala, igrajući uza zvuke harfe i citre.
29 Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.
Kad je Kovčeg saveza Jahvina ulazio u Davidov grad, Šaulova kći Mikala, gledajući s prozora, vidje kralja Davida kako skače i igra i prezre ga ona u svom srcu.

< 1 Nyakati 15 >