< 1 Nyakati 15 >

1 Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
След това Давид си построи и други къщи в Давидовия град; приготви и място за Божия ковчег, и постави шатър за него.
2 Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
Тогава рече Давид: Не бива да дигат Божия ковчег други освен левитите, защото тях избра Господ да носят Божия ковчег и да Му слугуват винаги.
3 Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
И Давид събра целия Израил в Ерусалим за да принесат Господния ковчег на мястото, което беше ковчег на мястото, което беше приготвил за него.
4 Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
Давид събра Аароновите потомци и левитите;
5 Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
от Каатовите потомци, началника Уриил и братята му, сто и двадесет души;
6 Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
от Марариевите потомци началника Асаия и братята му, двеста и двадесет души;
7 Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
от Гирсоновите потомци, началника Иоил и братята му, сто и тридесет души;
8 Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
от Елисафановите потомци, началника Семаия и братята му, двеста души;
9 Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
от Хевроновите потомци, началника Семаия и братята му, двеста души;
10 Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
от Озииловите потомци, началника Аминадав и братята му, сто и двадесет души.
11 Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
И Давид повика свещениците Садок и Авиатар и левитите Уриил, Асаия, Иоил, Семаия, Емиил и Аминадав, та им рече:
12 Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
Вие сте началници на бащините домове на левитите, осветете се вие и братята ви за да пренесете ковчега на Господа Израилевия Бог на мястото, което съм приготвил за него.
13 Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
Защото, понеже първия път вие не го дигнахте, Господ нашият Бог нанесе поражение върху нас, защото не Го потърсихме според както е заповядано.
14 Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
И той, свещениците и левитите осветиха себе си за да пренесат ковчега на Господа Израилевия Бог.
15 Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
(Левийците бяха, които носеха Божия ковчег с върлините горе на рамената си, както заповяда Моисей, според Господното слово).
16 Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
И Давид каза на левитските началници да поставят братята си певците с музикалните инструменти, псалтири и арфи и кимвали, за да свирят весело със силен глас.
17 Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
И така левитите поставиха Емана, Иоилевия син, а от братята му Асафа Варахииния син; а от братята им, Мерариевите потомци, Етана Кисиевия син;
18 hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
и с тях братята им от втория чин, вратарите Захария, Вена, Яазиил, Семирамот, Ехиил, Уний, Елиав, Ванаия, Маасия, Мататия, Елифалей, Микнеия, Овид-едом и Еиил.
19 Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
Така певците Еман, Асаф и Етан се определиха да дрънкат с медни кимвали;
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
а Захария, Азиил, Семирамот, Ехиил, Уний, Елиав, Маасия и Ванаия с псалтири по Аламот;
21 na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
а Мататия, Елифалей, Минеия, Авид-едом, Еиил и Азазия, с арфи по Семинит, за да ръководят пеенето.
22 Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
А Ханания, главен певец на левитите, ръководеше пеенето, понеже бе изкусен.
23 Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
А Варахия и Елкана бяха вратари за ковчега.
24 Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
А свещениците на Севания, Иосафата, Натанаил, Амасий, Захария, Ванаия и Елиезер свиреха с тръбите пред Божия ковчег; а Овид-едом и Ехия бяха вратари за ковчега.
25 Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
И тъй, Давид и Израилевите старейшини и хилядниците отидоха да дигнат с веселие ковчега на Господния завет от Овид-едомовата къща.
26 Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
И понеже Бог помагаше на левитите, които носеха ковчега на Господния завет, те пожертвуваха седем юнеца и седем овена.
27 Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
И Давид бе облечен с одежда от висон както и всичките левити, които носеха ковчега и певците, и Ханания ръководител на певците; а Давид носеше ленен ефод.
28 Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
Така целият Израил възвеждаше ковчега на Господния завет с възклицание с глас от рог, с тръби и с кимвали, като свиреха с псалтири и с арфи.
29 Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.
А когато ковчегът на Господния завет влизаше в Давидовия град, Михала, Сауловата дъщеря, погледна от прозореца, и като видя, че цар Давид скачаше и играеше, презря го в сърцето си.

< 1 Nyakati 15 >