< 1 Nyakati 14 >

1 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
Hiram, roi de Tyr, envoya une députation à David, avec du bois de cèdre, des maçons et des charpentiers pour lui bâtir une maison.
2 Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
Et David reconnut que le Seigneur l’avait destiné à régner sur Israël, et lui avait accordé une royauté glorieuse en faveur de son peuple Israël.
3 Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
David prit encore des épouses dans Jérusalem, et il engendra encore des fils et des filles.
4 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
Voici les noms de ceux qui lui naquirent à Jérusalem: Chammoua, Chobab, Nathan et Salomon;
5 Ibihari, Elishua, Elpeleti,
Yibhar, Elichoua, Elpélet;
6 Noga, Nefegi, Yafia,
Nogah, Néfeg et Yafia;
7 Elishama, Beeliada na Elifeleti.
Elichama, Beélyada et Elifélet.
8 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
Les Philistins, ayant su que David avait été oint comme roi de tout Israël, montèrent tous pour chercher à le prendre; David l’apprit et sortit à leur rencontre.
9 Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
Les Philistins étaient arrivés et s’étaient déployés dans la vallée de Refaïm.
10 Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
Alors David consulta Dieu en disant: "Dois-je monter vers les Philistins? Les livreras-tu entre mes mains?" Le Seigneur répondit à David: "Monte, je les livrerai entre tes mains.
11 Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
On monta à Baal-Peraçim, et David les y battit. Et il dit: "Dieu a dispersé mes ennemis par ma main, comme une eau débordée." C’Est pour cela que cet endroit fut nommé Baal-Peracim.
12 Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
Ils laissèrent là leurs idoles, qui furent brûlées sur l’ordre de David.
13 Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
Mais de nouveau les Philistins se déployèrent dans la vallée.
14 hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
David consulta encore Dieu, et Dieu lui répondit: "Ne monte pas à leur suite: fais un demi-tour et marche sur eux du côté des bekhaïm.
15 Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
Or, lorsque tu entendras un bruit de pas sur les cimes des bekhaïm, engage le combat, car alors Dieu sera venu à ton secours, pour que tu battes l’armée des Philistins."
16 Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
David se conforma aux instructions de Dieu, et ils battirent l’armée des Philistins depuis Ghibôn jusqu’à Ghézer.
17 Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.
Et la renommée de David se répandit dans tous les pays, et l’Eternel imprima sa terreur à toutes les nations.

< 1 Nyakati 14 >