< 1 Nyakati 14 >
1 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
Hiram, roi de Tyr, envoya des messagers à David avec des cèdres, des maçons et des charpentiers, pour lui construire une maison.
2 Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
David s'aperçut que Yahvé l'avait établi roi sur Israël, car son royaume était très élevé, à cause de son peuple Israël.
3 Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
David prit d'autres femmes à Jérusalem, et il engendra d'autres fils et d'autres filles.
4 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
Voici les noms des enfants qu'il eut à Jérusalem: Shammua, Shobab, Nathan, Salomon,
5 Ibihari, Elishua, Elpeleti,
Ibhar, Elishua, Elpelet,
7 Elishama, Beeliada na Elifeleti.
Elishama, Beeliada et Eliphelet.
8 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
Lorsque les Philistins apprirent que David avait été oint roi sur tout Israël, tous les Philistins montèrent à la recherche de David; David l'apprit et sortit à leur rencontre.
9 Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
Les Philistins étaient venus et avaient fait un raid dans la vallée des Rephaïm.
10 Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
David consulta Dieu, en disant: Monterai-je contre les Philistins? Les livreras-tu entre mes mains? » Yahvé lui dit: « Monte, car je vais les livrer entre tes mains. »
11 Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
Ils montèrent donc à Baal Perazim, et David les battit là. David dit: Dieu a brisé mes ennemis par ma main, comme des eaux qui jaillissent. C'est pourquoi on donna à ce lieu le nom de Baal Perazim.
12 Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
Ils y laissèrent leurs dieux; David donna un ordre, et ils furent brûlés par le feu.
13 Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
Les Philistins firent un autre raid dans la vallée.
14 hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
David consulta de nouveau Dieu, et Dieu lui dit: « Tu ne monteras pas après eux. Détourne-toi d'eux, et tombe sur eux en face des mûriers.
15 Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
Quand tu entendras le bruit de la marche dans les cimes des mûriers, alors tu sortiras pour combattre, car Dieu est sorti devant toi pour frapper l'armée des Philistins. »
16 Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
David fit ce que Dieu lui avait ordonné, et ils attaquèrent l'armée des Philistins depuis Gabaon jusqu'à Guézer.
17 Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.
La renommée de David se répandit dans tous les pays, et Yahvé fit craindre sa présence à toutes les nations.