< 1 Nyakati 14 >

1 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
Now Hiram king of Tyre sent messengers to David, and timber of cedars, with masons and carpenters, to build him a house.
2 Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
And David perceived that the LORD had confirmed him king over Israel, for his kingdom was exalted on high, because of his people Israel.
3 Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
And David took more wives at Jerusalem: and David begat more sons and daughters.
4 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
Now these [are] the names of [his] children which he had in Jerusalem; Shammua, and Shobab, Nathan, and Solomon,
5 Ibihari, Elishua, Elpeleti,
And Ibhar, and Elishua, and Elpalet,
6 Noga, Nefegi, Yafia,
And Nogah, and Nepheg, and Japhia,
7 Elishama, Beeliada na Elifeleti.
And Elishama, and Beeliada, and Eliphalet.
8 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
And when the Philistines heard that David was anointed king over all Israel, all the Philistines went up to seek David. And David heard [of it], and went out against them.
9 Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
And the Philistines came and spread themselves in the valley of Rephaim.
10 Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
And David inquired of God, saying, Shall I go up against the Philistines? and wilt thou deliver them into my hand? And the LORD said to him, Go up; for I will deliver them into thy hand.
11 Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
So they came up to Baal-perazim; and David smote them there. Then David said, God hath broken in upon my enemies by my hand like the breaking forth of waters: therefore they called the name of that place Baal-perazim.
12 Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
And when they had left their gods there, David gave a commandment, and they were burned with fire.
13 Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
And the Philistines yet again spread themselves abroad in the valley.
14 hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
Therefore David inquired again of God: and God said to him, Go not up after them; turn away from them, and come upon them over against the mulberry trees.
15 Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
And it shall be, when thou shalt hear a sound of going in the tops of the mulberry trees, then thou shalt go out to battle: for God hath gone forth before thee to smite the host of the Philistines.
16 Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
David therefore did as God commanded him: and they smote the host of the Philistines from Gibeon even to Gazer.
17 Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.
And the fame of David went out into all lands; and the LORD brought the fear of him upon all nations.

< 1 Nyakati 14 >