< 1 Nyakati 14 >

1 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
and to send: depart (Hiram *Q(K)*) king Tyre messenger to(wards) David and tree cedar and artificer wall and artificer tree: wood to/for to build to/for him house: home
2 Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
and to know David for to establish: establish him LORD to/for king upon Israel for to lift: exalt to/for above [to] royalty his in/on/with for the sake of people his Israel
3 Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
and to take: take David still woman: wife in/on/with Jerusalem and to beget David still son: child and daughter
4 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
and these name [the] to beget which to be to/for him in/on/with Jerusalem Shammua and Shobab Nathan and Solomon
5 Ibihari, Elishua, Elpeleti,
and Ibhar and Elishua and Elpelet
6 Noga, Nefegi, Yafia,
and Nogah and Nepheg and Japhia
7 Elishama, Beeliada na Elifeleti.
and Elishama and Beeliada and Eliphelet
8 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
and to hear: hear Philistine for to anoint David to/for king upon all Israel and to ascend: rise all Philistine to/for to seek [obj] David and to hear: hear David and to come out: come to/for face: before their
9 Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
and Philistine to come (in): come and to strip in/on/with Valley (of Rephaim) (Valley of) Rephaim
10 Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
and to ask David in/on/with God to/for to say to ascend: rise upon (Philistine *Q(k)*) and to give: give them in/on/with hand: power my and to say to/for him LORD to ascend: rise and to give: give them in/on/with hand: power your
11 Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
and to ascend: rise in/on/with Baal-perazim Baal-perazim and to smite them there David and to say David to break through [the] God [obj] enemy my in/on/with hand: power my like/as breach water upon so to call: call by name [the] place [the] he/she/it Baal-perazim Baal-perazim
12 Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
and to leave: forsake there [obj] God their and to say David and to burn in/on/with fire
13 Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
and to add: again still Philistine and to strip in/on/with valley
14 hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
and to ask still David in/on/with God and to say to/for him [the] God not to ascend: rise after them to turn: surround from upon them and to come (in): come to/for them from opposite [the] balsam
15 Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
and to be like/as to hear: hear you [obj] voice: sound [the] marching in/on/with head: top [the] balsam then to come out: come in/on/with battle for to come out: come [the] God to/for face: before your to/for to smite [obj] camp Philistine
16 Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
and to make: do David like/as as which to command him [the] God and to smite [obj] camp Philistine from Gibeon and till Gezer [to]
17 Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.
and to come out: come name David in/on/with all [the] land: country/planet and LORD to give: give [obj] dread his upon all [the] nation

< 1 Nyakati 14 >