< 1 Nyakati 13 >

1 Daudi alishauriana na kila afisa wake, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia.
داوود پس از مشورت با فرماندهان سپاه،
2 Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote la Israeli, “Kama mkiona ni vyema, na kama ni mapenzi ya Bwana Mungu wetu, tupeleke ujumbe kwa ndugu zetu wengine walio mbali na walio karibu katika nchi yote ya Israeli, pia kwa makuhani na Walawi walio pamoja nao katika miji yao na katika sehemu zao za malisho yao, waje waungane na sisi.
خطاب به مردان اسرائیل که در حبرون جمع شده بودند چنین گفت: «حال که شما قصد دارید مرا پادشاه خود سازید و خداوند، خدای ما نیز پادشاهی مرا قبول فرموده است، بیایید برای تمام برادرانمان در سراسر اسرائیل پیغام بفرستیم و آنها را با کاهنان و لاویان دعوت کنیم که بیایند و به جمع ما ملحق شوند.
3 Sisi na tulirudishe Sanduku la Mungu wetu kwetu kwa maana hatukujali wakati wa utawala wa Sauli.”
بیایید برویم و صندوق عهد خدا را باز آوریم، زیرا از وقتی که شائول پادشاه شد به آن توجه نکرده‌ایم.»
4 Kusanyiko lote likakubaliana kufanya hivyo, kwa sababu ilionekana vyema kwa watu wote.
همه این پیشنهاد را پسندیدند و با آن موافقت کردند.
5 Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia Mto Shihori ulioko Misri hadi Lebo-Hamathi, ili kulileta Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu.
پس داوود تمام مردم را از سراسر خاک اسرائیل احضار نمود تا وقتی که صندوق عهد خداوند را از قریهٔ یعاریم می‌آورند، حضور داشته باشند.
6 Daudi akiwa pamoja na Waisraeli wote wakaenda Baala ya Yuda (yaani Kiriath-Yearimu) kulipandisha Sanduku la Mungu Bwana, yeye anayeketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi: Sanduku linaloitwa kwa Jina lake, kutoka huko.
آنگاه داوود و تمام قوم اسرائیل به بعله (که همان قریه یعاریم در یهوداست) رفتند تا صندوق خدا را که نام خداوند بر آن است از آنجا بیاورند، خداوندی که میان کروبیانِ روی صندوق جلوس می‌کند.
7 Wakalisafirisha Sanduku la Mungu kwa gari jipya la kukokotwa na maksai kutoka nyumba ya Abinadabu, Uza na Ahio wakiliongoza gari hilo.
پس آن را از خانهٔ ابیناداب برداشتند و بر ارابه‌ای نو گذاشتند. عزا و اخیو، گاوهای ارابه را می‌راندند.
8 Daudi pamoja na Waisraeli wote walikuwa wanasifu kwa nguvu zao zote mbele za Mungu, kwa nyimbo na kwa vinubi, zeze, matari, matoazi na tarumbeta.
آنگاه داوود و تمام قوم با سرود همراه با صدای بربط و عود، دف و سنج، و شیپور در حضور خدا با تمام قدرت به شادی پرداختند.
9 Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Kidoni, Uza akaunyoosha mkono wake ili kulizuia Sanduku, kwa sababu maksai walijikwaa.
اما وقتی به خرمنگاه کیدون رسیدند، پای گاوها لغزید و عزا دست خود را دراز کرد تا صندوق عهد را بگیرد.
10 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza, akampiga kwa sababu aliuweka mkono wake kwenye Sanduku. Kwa hiyo akafa pale mbele za Mungu.
در این موقع خشم خداوند بر عزا افروخته شد و او را کشت، چون به صندوق عهد دست زده بود. پس عزا همان جا در حضور خدا مرد.
11 Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, mahali pale pakaitwa Peres-Uza hadi leo.
داوود از این عمل خداوند غمگین شد و آن مکان را «مجازات عزا» نامید که تا به امروز هم به این نام معروف است.
12 Siku ile Daudi akamwogopa Mungu naye akauliza. “Nitawezaje kulichukua Sanduku la Mungu kwangu?”
آن روز، داوود از خدا ترسید و گفت: «چطور می‌توانم صندوق عهد خدا را به خانه ببرم؟»
13 Hakulichukua hilo Sanduku akae nalo katika Mji wa Daudi. Badala yake, akalipeleka nyumbani kwa Obed-Edomu, Mgiti.
بنابراین تصمیم گرفت به جای شهر داوود، آن را به خانهٔ عوبید ادوم که از جت آمده بود، ببرد.
14 Sanduku la Mungu likabaki pamoja na jamaa ya Obed-Edomu, nyumbani kwake kwa miezi mitatu, naye Bwana akaibariki nyumba yake pamoja na kila kitu alichokuwa nacho.
صندوق عهد سه ماه در خانهٔ عوبید ماند و خداوند عوبید و تمام اهل خانهٔ او را برکت داد.

< 1 Nyakati 13 >