< 1 Nyakati 13 >

1 Daudi alishauriana na kila afisa wake, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia.
And David consulted with the captains of thousands and of hundreds, and with every leader.
2 Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote la Israeli, “Kama mkiona ni vyema, na kama ni mapenzi ya Bwana Mungu wetu, tupeleke ujumbe kwa ndugu zetu wengine walio mbali na walio karibu katika nchi yote ya Israeli, pia kwa makuhani na Walawi walio pamoja nao katika miji yao na katika sehemu zao za malisho yao, waje waungane na sisi.
And David said to all the congregation of Israel, If it seemeth good to you, and that it is of the LORD our God, let us send abroad to our brethren every where, that are left in all the land of Israel, and with them also to the priests and Levites who are in their cities and common lands, that they may assemble to us:
3 Sisi na tulirudishe Sanduku la Mungu wetu kwetu kwa maana hatukujali wakati wa utawala wa Sauli.”
And let us bring again to us the ark of our God: for we enquired not at it in the days of Saul.
4 Kusanyiko lote likakubaliana kufanya hivyo, kwa sababu ilionekana vyema kwa watu wote.
And all the congregation said that they would do so: for the thing was right in the eyes of all the people.
5 Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia Mto Shihori ulioko Misri hadi Lebo-Hamathi, ili kulileta Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu.
So David gathered all Israel together, from Shihor of Egypt even to the entrance of Hemath, to bring the ark of God from Kirjathjearim.
6 Daudi akiwa pamoja na Waisraeli wote wakaenda Baala ya Yuda (yaani Kiriath-Yearimu) kulipandisha Sanduku la Mungu Bwana, yeye anayeketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi: Sanduku linaloitwa kwa Jina lake, kutoka huko.
And David went up, and all Israel, to Baalah, that is, to Kirjathjearim, which belonged to Judah, to bring up from there the ark of God the LORD, that dwelleth between the cherubim, whose name is called on it.
7 Wakalisafirisha Sanduku la Mungu kwa gari jipya la kukokotwa na maksai kutoka nyumba ya Abinadabu, Uza na Ahio wakiliongoza gari hilo.
And they carried the ark of God in a new cart out of the house of Abinadab: and Uzza and Ahio drove the cart.
8 Daudi pamoja na Waisraeli wote walikuwa wanasifu kwa nguvu zao zote mbele za Mungu, kwa nyimbo na kwa vinubi, zeze, matari, matoazi na tarumbeta.
And David and all Israel played before God with all their might, and with singing, and with harps, and with psalteries, and with timbrels, and with cymbals, and with trumpets.
9 Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Kidoni, Uza akaunyoosha mkono wake ili kulizuia Sanduku, kwa sababu maksai walijikwaa.
And when they came to the threshingfloor of Chidon, Uzza put forth his hand to hold the ark; for the oxen stumbled.
10 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza, akampiga kwa sababu aliuweka mkono wake kwenye Sanduku. Kwa hiyo akafa pale mbele za Mungu.
And the anger of the LORD was kindled against Uzza, and he smote him, because he put his hand to the ark: and there he died before God.
11 Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, mahali pale pakaitwa Peres-Uza hadi leo.
And David was displeased, because the LORD had broken forth upon Uzza: therefore that place is called Perezuzza to this day.
12 Siku ile Daudi akamwogopa Mungu naye akauliza. “Nitawezaje kulichukua Sanduku la Mungu kwangu?”
And David was afraid of God that day, saying, How shall I bring the ark of God home to me?
13 Hakulichukua hilo Sanduku akae nalo katika Mji wa Daudi. Badala yake, akalipeleka nyumbani kwa Obed-Edomu, Mgiti.
So David brought not the ark to himself to the city of David, but carried it aside into the house of Obededom the Gittite.
14 Sanduku la Mungu likabaki pamoja na jamaa ya Obed-Edomu, nyumbani kwake kwa miezi mitatu, naye Bwana akaibariki nyumba yake pamoja na kila kitu alichokuwa nacho.
And the ark of God remained with the family of Obededom in his house three months. And the LORD blessed the house of Obededom, and all that he had.

< 1 Nyakati 13 >