< 1 Nyakati 13 >
1 Daudi alishauriana na kila afisa wake, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia.
And David consults with the heads of the thousands and of the hundreds, [and] with every leader,
2 Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote la Israeli, “Kama mkiona ni vyema, na kama ni mapenzi ya Bwana Mungu wetu, tupeleke ujumbe kwa ndugu zetu wengine walio mbali na walio karibu katika nchi yote ya Israeli, pia kwa makuhani na Walawi walio pamoja nao katika miji yao na katika sehemu zao za malisho yao, waje waungane na sisi.
and David says to all the assembly of Israel, “If it is good to you, and it has broken forth from our God YHWH—we send to our brothers, those left in all the lands of Israel, and the priests and the Levites with them in the cities of their outskirts, and they are gathered to us,
3 Sisi na tulirudishe Sanduku la Mungu wetu kwetu kwa maana hatukujali wakati wa utawala wa Sauli.”
and we bring around the Ark of our God to us, for we did not seek Him in the days of Saul.”
4 Kusanyiko lote likakubaliana kufanya hivyo, kwa sababu ilionekana vyema kwa watu wote.
And all the assembly says to do so, for the thing is right in the eyes of all the people.
5 Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia Mto Shihori ulioko Misri hadi Lebo-Hamathi, ili kulileta Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu.
And David assembles all Israel from Shihor of Egypt even to the entering in of Hamath, to bring in the Ark of God from Kirjath-Jearim,
6 Daudi akiwa pamoja na Waisraeli wote wakaenda Baala ya Yuda (yaani Kiriath-Yearimu) kulipandisha Sanduku la Mungu Bwana, yeye anayeketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi: Sanduku linaloitwa kwa Jina lake, kutoka huko.
and David goes up, and all Israel, to Ba‘alah, to Kirjath-Jearim that [belongs] to Judah, to bring up from there the Ark of God, YHWH, inhabiting the cherubim, where the Name is called on.
7 Wakalisafirisha Sanduku la Mungu kwa gari jipya la kukokotwa na maksai kutoka nyumba ya Abinadabu, Uza na Ahio wakiliongoza gari hilo.
And they place the Ark of God on a new cart from the house of Abinadab, and Uzza and Ahio are leading the cart,
8 Daudi pamoja na Waisraeli wote walikuwa wanasifu kwa nguvu zao zote mbele za Mungu, kwa nyimbo na kwa vinubi, zeze, matari, matoazi na tarumbeta.
and David and all Israel are playing before God, with all strength, and with songs, and with harps, and with psalteries, and with timbrels, and with cymbals, and with trumpets.
9 Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Kidoni, Uza akaunyoosha mkono wake ili kulizuia Sanduku, kwa sababu maksai walijikwaa.
And they come to the threshing-floor of Chidon, and Uzza puts forth his hand to seize the Ark, for the oxen were released,
10 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza, akampiga kwa sababu aliuweka mkono wake kwenye Sanduku. Kwa hiyo akafa pale mbele za Mungu.
and the anger of YHWH is kindled against Uzza, and He strikes him, because that he has put forth his hand on the Ark, and he dies there before God.
11 Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, mahali pale pakaitwa Peres-Uza hadi leo.
And it is displeasing to David, because YHWH has made a breach on Uzza, and one calls that place “Breach of Uzza” to this day.
12 Siku ile Daudi akamwogopa Mungu naye akauliza. “Nitawezaje kulichukua Sanduku la Mungu kwangu?”
And David fears God on that day, saying, “How do I bring the Ark of God to me?”
13 Hakulichukua hilo Sanduku akae nalo katika Mji wa Daudi. Badala yake, akalipeleka nyumbani kwa Obed-Edomu, Mgiti.
And David has not turned aside the Ark to himself, to the City of David, and turns it aside to the house of Obed-Edom the Gittite.
14 Sanduku la Mungu likabaki pamoja na jamaa ya Obed-Edomu, nyumbani kwake kwa miezi mitatu, naye Bwana akaibariki nyumba yake pamoja na kila kitu alichokuwa nacho.
And the Ark of God dwells with the household of Obed-Edom, in his house, three months, and YHWH blesses the house of Obed-Edom, and all that he has.