< 1 Nyakati 12 >
1 Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,
Un šie ir, kas pie Dāvida nāca uz Ciklagu, kad tas vēl mita svešumā Saula, Ķisa dēla, pēc. Un tie bija arīdzan no tiem varoņiem, kara palīgi,
2 walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):
Stopu nesēji, akmeņu metēji ar labo un ar kreiso roku un bultu šāvēji no stopa. Tie bija no Saula brāļiem, no Benjamina.
3 Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,
Tie pirmie bija Aķiēzers un Joas, Zaāmas bērni no Ģibeas, tad Jeziēls un Pelecs, Asmaveta bērni, un Barakus un Jeūs no Antotas.
4 na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,
Un Jezmaja no Gibeonas bija jo varens starp tiem trīsdesmit un pār tiem trīsdesmit. Un Jeremija un Jaēziēls un Jehohanans un Jozabats no Ģederas,
5 Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;
Eleūzajus un Jerimots un Bealija un Samarija un Zevataja no Aravas,
6 Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;
Elkanus un Jezija un Azareēls un Joēzers un Jazabeams, Koraha dēli,
7 Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
Un Joēlus un Zabadija, Jeroama dēli, no Ģedoras.
8 Baadhi ya Wagadi wakajitenga na kujiunga na Daudi katika ngome yake huko jangwani. Walikuwa mashujaa hodari, waliokuwa tayari kwa vita na wenye uwezo wa kutumia ngao na mkuki. Nyuso zao zilikuwa nyuso za simba na walikuwa na wepesi kama paa milimani.
No Gada bērniem arīdzan Dāvidam tai pilskalnā tuksnesī piekrita vareni karavīri, priekšturamu bruņu un šķēpu nesēji, no izskata kā lauvas un čakli kā stirnas pa kalniem.
9 Ezeri alikuwa mkuu wao, Obadia alikuwa wa pili katika uongozi, Eliabu wa tatu,
Tas pārākais bija Ezers, otrais Obadija, trešais Elijabs,
10 Mishmana wa nne, Yeremia wa tano,
Ceturtais Mazmanus, piektais Jeremija,
11 Atai wa sita, Elieli wa saba,
Sestais Atajus, septītais Eliēls,
12 Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa,
Astotais Jehohanans, devītais Ebsabads,
13 Yeremia wa kumi, na Makbanai wa kumi na moja.
Desmitais Jeremija, vienpadsmitais Makbanajus.
14 Hawa Wagadi walikuwa majemadari. Aliyekuwa wa mwisho kuliko wote aliweza kuongoza askari 100, na aliyekuwa na uweza zaidi ya wote aliongoza 1,000.
Šie bija no Gada bērniem, kara virsnieki, tie mazākie viens par simtu, tie lielākie par tūkstoti.
15 Wao ndio walivuka Mto Yordani katika mwezi wa kwanza ukiwa umefurika hadi kwenye kingo zake zote na kusababisha watu wote waliokuwa wanaishi kwenye mabonde kukimbilia mashariki na wengine magharibi.
Šie ir tie, kas pār Jardāni pārgāja pirmā mēnesī, kad tā bija pilna līdz pašiem krastiem, un tie izdzina visus ielejas ļaudis pret rītiem un pret vakariem.
16 Wabenyamini wengine na baadhi ya watu kutoka Yuda pia walikuja kwa Daudi katika ngome yake.
No Benjamina un Jūda bērniem nāca arīdzan pie Dāvida uz pilskalnu.
17 Daudi akatoka nje kuwalaki na akawaambia, “Kama mmekuja kwangu kwa amani, kunisaidia, mimi niko tayari kuwaruhusu ninyi kuungana nami. Lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa adui zangu wakati mimi mikono yangu haina hatia, basi Mungu wa baba zetu aone na awahukumu.”
Un Dāvids tiem izgāja pretī un bildināja un uz tiem sacīja: ja jūs ar miera prātu pie manis esat nākuši, man palīdzēt, tad man būs viena sirds ar jums; bet ja jūs mani ar viltu gribat nodot maniem ienaidniekiem, un tomēr netaisnības pie manis nav, tad lai mūsu Dievs to redz un soda.
18 Kisha Roho akaja juu ya Amasai, mkuu wa wale Thelathini, naye akasema: “Sisi tu watu wako, ee Daudi! Nasi tuko pamoja na wewe, ee mwana wa Yese! Ushindi, naam, ushindi uwe kwako, pia ushindi kwa wale walio upande wako, kwa kuwa Mungu wako atakusaidia.” Kwa hiyo Daudi akawapokea na kuwafanya viongozi wa vikosi vyake vya uvamizi.
Bet Tas Gars nāca uz Amaaju, to virsnieku pār trīsdesmit (un tas sacīja): tev mēs piederam, Dāvid un ar tevi mēs būsim, tu Isajus dēls: miers, miers lai ir ar tevi un miers ar taviem palīgiem, jo tavs Dievs ir tavs palīgs. Tad Dāvids tos pieņēma un tos iecēla par karapulku virsniekiem.
19 Baadhi ya watu kutoka kabila la Manase wakajiunga na Daudi wakati alikwenda pamoja na Wafilisti, kupigana na Sauli. (Daudi na watu wake hawakuwasaidia Wafilisti kwa sababu, baada ya ushauri, watawala wao walimrudisha. Wakasema, “Itatugharimu vichwa vyetu kama Daudi atatuasi na kurudi kwa Sauli bwana wake.”)
Arī no Manasus Dāvidam piekrita, kad tas ar Fīlistiem nāca pret Saulu karot, bet šiem nepalīdzēja; jo Fīlistu lielkungi pēc sava padoma to atlaida sacīdami: viņš pāries pie sava kunga Saula un mūsu galvas kritīs.
20 Daudi alipokwenda Siklagi, hawa ndio watu wa kabila la Manase waliojiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai, viongozi wa vikosi vya watu 1,000 katika kabila la Manase.
Kad viņš gāja uz Ciklagu, tad tam no Manasus piekrita Adnaks un Jozabats un Jediaēls un Mikaēls un Jozabads un Elijus un Ciltajus, virsnieki pār Manasus tūkstošiem.
21 Walimsaidia Daudi dhidi ya makundi ya uvamizi, kwa kuwa wote walikuwa mashujaa hodari na walikuwa majemadari katika jeshi lake.
Un tie Dāvidam palīdzēja pret (Amalekiešu) sirotājiem, jo tie visi bija stipri varoņi un palika par kara virsniekiem.
22 Siku baada ya siku watu walikuja kumsaidia Daudi, mpaka akawa na jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
Un ikdienas Dāvidam piekrita palīgi, tiekams tas karaspēks palika tik liels kā Dieva karaspēks.
23 Hawa ndio watu waliojiandaa kwa ajili ya vita waliokuja kwa Daudi huko Hebroni ili kumtwalia ufalme kutoka kwa Sauli, kama Bwana alivyokuwa amesema:
Un šis ir to galvu skaits, kas bija apbruņojušies uz karu un nākuši pie Dāvida uz Hebroni, ka viņam piešķirtu Saula valstību pēc Tā Kunga vārda.
24 watu wa Yuda, wanaochukua ngao na mikuki walikuwa 6,800 wote wakiwa tayari kwa vita.
Jūda bērnu, kas priekšturamās bruņas un šķēpus nesa, bija seši tūkstoši un astoņsimt uz karu gatavi.
25 Watu wa Simeoni, mashujaa waliokuwa tayari kwa vita walikuwa 7,100.
No Sīmeana bērniem bija septiņi tūkstoši un simts stipri kara varoņi.
26 Watu wa Lawi walikuwa 4,600,
No Levja bērniem četrtūkstoš un sešsimt.
27 pamoja na Yehoyada, kiongozi wa jamaa ya Aroni, aliyekuwa pamoja na watu 3,700,
Un Jojadus, Ārona bērnu valdnieks, un ar to trīs tūkstoši un septiņsimt.
28 na Sadoki, kijana shujaa na hodari, aliyekuwa pamoja na maafisa ishirini na wawili kutoka jamaa yake.
Un Cadoks, jauns stiprs varonis, un no viņa tēva nama bija divdesmit divi virsnieki.
29 Watu wa Benyamini, ndugu zake Sauli, walikuwa 3,000; wengi wao walikuwa wameendelea kuwa waaminifu kwa Sauli mpaka wakati huo.
Un no Benjamina bērniem bija Saula brāļu trīs tūkstoši; jo līdz tam laikam vēl viss vairums turējās pie Saula nama.
30 Watu wa Efraimu, mashujaa hodari 20,800, watu waliokuwa maarufu katika koo zao.
Un no Efraīma bērniem divdesmit tūkstoši un astoņsimt stipri varoņi, vīri, kam bija liela slava savu tēvu namā.
31 Watu wa nusu ya kabila la Manase, waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme, watu 18,000.
Un no Manasus puscilts astoņpadsmit tūkstoši, kas ar vārdu tika noteikti, ka nāktu, Dāvidu celt par ķēniņu.
32 Watu wa Isakari, waliofahamu majira na kujua kile ambacho Israeli inapasa kufanya, walikuwa viongozi 200, pamoja na jamaa zao wote chini ya uongozi wao.
Un no Izašara bērniem, kas bija gudri noprast, kas Israēlim katrā laikā bija darāms; šo virsnieku bija divsimt, un visi viņu brāļi darīja pēc viņu vārda.
33 Watu wa Zabuloni, askari wenye uzoefu mkubwa walioandaliwa tayari kwa vita wakiwa na silaha za kila aina, ili kumsaidia Daudi kwa uaminifu thabiti, walikuwa 50,000.
No Zebulona, kas izgāja karā apbruņoti ar visādām karabruņām, bija piecdesmit tūkstoši, savā kārtā stāvēdami ar drošu sirdi.
34 Watu wa Naftali, maafisa 1,000, pamoja na watu 37,000 waliochukua ngao na mikuki.
Un no Naftalus bija tūkstotis virsnieki un ar tiem trīsdesmit septiņi tūkstoši ar priekšturamām bruņām un šķēpiem.
35 Watu wa Dani 28,600 waliokuwa tayari kwa vita.
Un no Dana bērniem uz karu gatavi divdesmit un astoņi tūkstoši un sešsimt.
36 Watu wa Asheri, askari 40,000 wenye uzoefu mkubwa waliondaliwa kwa ajili ya vita.
Un no Ašera, kas izgāja karā, uz kaušanos gatavi, četrdesmit tūkstoši.
37 Na pia watu kutoka mashariki ya Yordani, watu wa Reubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakiwa na kila aina ya silaha, watu 120,000.
Un no PārJardānes, no Rūbena un Gada bērniem un no Manasus puscilts ar visādām kara bruņām, simts un divdesmit tūkstoši.
38 Wote hawa walikuwa watu wapiganaji waliojitolea kutumika katika safu zao. Walikuja Hebroni wakiwa wameamua kikamilifu kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli yote. Waisraeli wengine wote walikuwa pia na nia hiyo moja ya kumfanya Daudi kuwa mfalme.
Visi šie karavīri, ar drošu sirdi pēc kārtas pulkos stāvēdami, nāca uz Hebroni, Dāvidu celt par ķēniņu pār visu Israēli. Un arī visiem citiem no Israēla bija vienāda sirds, Dāvidu celt par ķēniņu.
39 Watu hawa wakakaa huko na Daudi siku tatu, wakila na kunywa, kwa sababu jamaa zao zilikuwa zimewapatia mahitaji yao.
Un tie tur bija pie Dāvida trīs dienas, ēda un dzēra, jo viņu brāļi priekš tiem bija sataisījuši.
40 Pia, majirani zao hata wale walio mbali hadi Isakari, Zabuloni na Naftali, walikuja wakiwaletea vyakula walivyovibeba kwa punda, ngamia, nyumbu na maksai. Kulikuwepo na wingi wa unga, maandazi ya tini, maandazi ya zabibu kavu, divai, mafuta, ngʼombe na kondoo, kwa maana kulikuwa na furaha katika Israeli.
Un kas tuvu pie tiem dzīvoja līdz Īsašaram un Zebulonam un Naftalum, tie nesa maizi uz ēzeļiem un kamieļiem un zirgēzeļiem un uz vēršiem, miltu ēdienus, vīģu un rozīņu raušus un vīnu un eļļu un vēršus un avis lielā pulkā; jo līksmība bija iekš Israēla.