< 1 Nyakati 12 >

1 Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,
Et ceux-ci vinrent vers David à Tsiklag, lorsqu’il se tenait loin encore de la face de Saül, fils de Kis; et ceux-ci étaient parmi les hommes forts qui lui donnaient du secours dans la guerre,
2 walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):
armés d’arcs, se servant de la main droite et de la main gauche [pour lancer] des pierres, et [pour tirer] des flèches avec l’arc; ils étaient d’entre les frères de Saül, de Benjamin:
3 Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,
le chef Akhiézer, et Joas, [tous deux] fils de Shemaa, le Guibhathite; et Jeziel, et Péleth, les fils d’Azmaveth; et Beraca, et Jéhu, l’Anathothite;
4 na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,
et Jishmahia, le Gabaonite, homme fort parmi les 30, et au-dessus des 30; et Jérémie, et Jakhaziel, et Jokhanan, et Jozabad, le Guedérathite;
5 Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;
Elhuzaï, et Jerimoth, et Bealia, et Shemaria, et Shephatia, le Haruphite;
6 Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;
Elkana, et Jishija, et Azareël, et Joézer, et Jashobham, Corites;
7 Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
et Joéla et Zebadia, les fils de Jerokham, de Guedor.
8 Baadhi ya Wagadi wakajitenga na kujiunga na Daudi katika ngome yake huko jangwani. Walikuwa mashujaa hodari, waliokuwa tayari kwa vita na wenye uwezo wa kutumia ngao na mkuki. Nyuso zao zilikuwa nyuso za simba na walikuwa na wepesi kama paa milimani.
Et, des Gadites, il se détacha, [pour se joindre] à David dans le lieu fort au désert, des hommes forts et vaillants, hommes exercés pour la guerre, armés de boucliers et de piques; et leurs faces étaient comme des faces de lions, et ils étaient prompts comme des gazelles sur les montagnes:
9 Ezeri alikuwa mkuu wao, Obadia alikuwa wa pili katika uongozi, Eliabu wa tatu,
Ézer, le premier; Abdias, le second; Éliab, le troisième;
10 Mishmana wa nne, Yeremia wa tano,
Mishmanna, le quatrième; Jérémie, le cinquième;
11 Atai wa sita, Elieli wa saba,
Atthaï, le sixième; Éliel, le septième;
12 Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa,
Jokhanan, le huitième; Elzabad, le neuvième;
13 Yeremia wa kumi, na Makbanai wa kumi na moja.
Jérémie, le dixième; Macbannaï, le onzième.
14 Hawa Wagadi walikuwa majemadari. Aliyekuwa wa mwisho kuliko wote aliweza kuongoza askari 100, na aliyekuwa na uweza zaidi ya wote aliongoza 1,000.
Ceux-là, d’entre les fils de Gad, étaient chefs de l’armée; le moindre [était chef] de 100 [hommes], et le plus grand, de 1 000.
15 Wao ndio walivuka Mto Yordani katika mwezi wa kwanza ukiwa umefurika hadi kwenye kingo zake zote na kusababisha watu wote waliokuwa wanaishi kwenye mabonde kukimbilia mashariki na wengine magharibi.
Ce sont ceux qui traversèrent le Jourdain au premier mois, quand il regorge par-dessus tous ses bords; et ils mirent en fuite ceux de toutes les vallées, vers le levant et vers le couchant.
16 Wabenyamini wengine na baadhi ya watu kutoka Yuda pia walikuja kwa Daudi katika ngome yake.
Et des fils de Benjamin et de Juda allèrent vers David dans le lieu fort.
17 Daudi akatoka nje kuwalaki na akawaambia, “Kama mmekuja kwangu kwa amani, kunisaidia, mimi niko tayari kuwaruhusu ninyi kuungana nami. Lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa adui zangu wakati mimi mikono yangu haina hatia, basi Mungu wa baba zetu aone na awahukumu.”
Et David sortit à leur rencontre, et prit la parole et leur dit: Si c’est pour la paix que vous venez vers moi, pour m’aider, mon cœur sera uni à vous; mais si c’est pour me livrer à mes ennemis, quand il n’y a pas de violence en ma main, que le Dieu de nos pères regarde, et punisse.
18 Kisha Roho akaja juu ya Amasai, mkuu wa wale Thelathini, naye akasema: “Sisi tu watu wako, ee Daudi! Nasi tuko pamoja na wewe, ee mwana wa Yese! Ushindi, naam, ushindi uwe kwako, pia ushindi kwa wale walio upande wako, kwa kuwa Mungu wako atakusaidia.” Kwa hiyo Daudi akawapokea na kuwafanya viongozi wa vikosi vyake vya uvamizi.
Et l’Esprit revêtit Amasçaï, chef des principaux capitaines: Nous sommes à toi, David, et avec toi, fils d’Isaï! Paix, paix à toi, et paix à ceux qui t’aident, car ton Dieu t’aide! Et David les reçut, et les établit chefs de bandes.
19 Baadhi ya watu kutoka kabila la Manase wakajiunga na Daudi wakati alikwenda pamoja na Wafilisti, kupigana na Sauli. (Daudi na watu wake hawakuwasaidia Wafilisti kwa sababu, baada ya ushauri, watawala wao walimrudisha. Wakasema, “Itatugharimu vichwa vyetu kama Daudi atatuasi na kurudi kwa Sauli bwana wake.”)
Et, de Manassé, il y en eut qui passèrent à David quand il vint avec les Philistins pour la bataille contre Saül; mais ils ne les aidèrent point, car, après avoir tenu conseil, les princes des Philistins le renvoyèrent, disant: Au péril de nos têtes il passera à son seigneur Saül.
20 Daudi alipokwenda Siklagi, hawa ndio watu wa kabila la Manase waliojiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai, viongozi wa vikosi vya watu 1,000 katika kabila la Manase.
Quand il s’en alla à Tsiklag, [ceux-ci], de Manassé, passèrent à lui: Adnakh, et Jozabad, et Jediaël, et Micaël, et Jozabad, et Élihu, et Tsilthaï, chefs des milliers qui étaient dans Manassé;
21 Walimsaidia Daudi dhidi ya makundi ya uvamizi, kwa kuwa wote walikuwa mashujaa hodari na walikuwa majemadari katika jeshi lake.
et ils aidèrent David dans ses expéditions, car ils étaient tous forts et vaillants, et ils furent chefs dans l’armée.
22 Siku baada ya siku watu walikuja kumsaidia Daudi, mpaka akawa na jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
Car de jour en jour il arrivait [des gens] vers David pour l’aider, jusqu’à ce que le camp fut grand, comme un camp de Dieu.
23 Hawa ndio watu waliojiandaa kwa ajili ya vita waliokuja kwa Daudi huko Hebroni ili kumtwalia ufalme kutoka kwa Sauli, kama Bwana alivyokuwa amesema:
Et c’est ici le nombre des hommes équipés pour l’armée, qui vinrent vers David à Hébron, afin de lui transférer le royaume de Saül, selon le commandement de l’Éternel:
24 watu wa Yuda, wanaochukua ngao na mikuki walikuwa 6,800 wote wakiwa tayari kwa vita.
Fils de Juda, portant le bouclier et la pique, 6 800, équipés pour l’armée.
25 Watu wa Simeoni, mashujaa waliokuwa tayari kwa vita walikuwa 7,100.
Des fils de Siméon, hommes forts et vaillants pour l’armée, 7 100.
26 Watu wa Lawi walikuwa 4,600,
Des fils de Lévi, 4 600.
27 pamoja na Yehoyada, kiongozi wa jamaa ya Aroni, aliyekuwa pamoja na watu 3,700,
Et Jehoïada, prince [des fils] d’Aaron, et avec lui 3 700.
28 na Sadoki, kijana shujaa na hodari, aliyekuwa pamoja na maafisa ishirini na wawili kutoka jamaa yake.
Et Tsadok, jeune homme fort et vaillant; et la maison de son père, 22 chefs.
29 Watu wa Benyamini, ndugu zake Sauli, walikuwa 3,000; wengi wao walikuwa wameendelea kuwa waaminifu kwa Sauli mpaka wakati huo.
Et, des fils de Benjamin, frères de Saül, 3 000; car jusqu’alors la plus grande partie d’entre eux faisaient la garde de la maison de Saül.
30 Watu wa Efraimu, mashujaa hodari 20,800, watu waliokuwa maarufu katika koo zao.
Et, des fils d’Éphraïm, 20 800 hommes forts et vaillants, hommes de renom dans leurs maisons de pères.
31 Watu wa nusu ya kabila la Manase, waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme, watu 18,000.
Et, de la demi-tribu de Manassé, 18 000, qu’on avait nommés par nom pour aller établir David roi.
32 Watu wa Isakari, waliofahamu majira na kujua kile ambacho Israeli inapasa kufanya, walikuwa viongozi 200, pamoja na jamaa zao wote chini ya uongozi wao.
Et, des fils d’Issacar, qui savaient discerner les temps pour savoir ce que devait faire Israël: leurs chefs, 200, et tous leurs frères à leur commandement.
33 Watu wa Zabuloni, askari wenye uzoefu mkubwa walioandaliwa tayari kwa vita wakiwa na silaha za kila aina, ili kumsaidia Daudi kwa uaminifu thabiti, walikuwa 50,000.
De Zabulon, ceux qui allaient à l’armée, préparés pour le combat, avec toutes les armes de guerre: 50 000, gardant leur rang, n’ayant point un cœur double.
34 Watu wa Naftali, maafisa 1,000, pamoja na watu 37,000 waliochukua ngao na mikuki.
Et, de Nephthali, 1 000 chefs, et avec eux, portant le bouclier et la lance, 37 000.
35 Watu wa Dani 28,600 waliokuwa tayari kwa vita.
Et, des Danites, préparés pour la guerre, 28 600.
36 Watu wa Asheri, askari 40,000 wenye uzoefu mkubwa waliondaliwa kwa ajili ya vita.
Et, d’Aser, qui allaient à l’armée pour se mettre en ordre de bataille pour le combat, 40 000.
37 Na pia watu kutoka mashariki ya Yordani, watu wa Reubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakiwa na kila aina ya silaha, watu 120,000.
Et, d’au-delà le Jourdain, des Rubénites, et des Gadites, et de ceux de la demi-tribu de Manassé, avec toutes les armes de guerre pour combattre: 120 000.
38 Wote hawa walikuwa watu wapiganaji waliojitolea kutumika katika safu zao. Walikuja Hebroni wakiwa wameamua kikamilifu kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli yote. Waisraeli wengine wote walikuwa pia na nia hiyo moja ya kumfanya Daudi kuwa mfalme.
Tous ceux-là, hommes de guerre, gardant leurs rangs en ordre de bataille, vinrent à Hébron d’un cœur droit, pour établir David roi sur tout Israël; et aussi tout le reste d’Israël était d’un seul cœur pour établir David roi.
39 Watu hawa wakakaa huko na Daudi siku tatu, wakila na kunywa, kwa sababu jamaa zao zilikuwa zimewapatia mahitaji yao.
Et ils furent là avec David trois jours, mangeant et buvant; car leurs frères leur avaient [tout] préparé.
40 Pia, majirani zao hata wale walio mbali hadi Isakari, Zabuloni na Naftali, walikuja wakiwaletea vyakula walivyovibeba kwa punda, ngamia, nyumbu na maksai. Kulikuwepo na wingi wa unga, maandazi ya tini, maandazi ya zabibu kavu, divai, mafuta, ngʼombe na kondoo, kwa maana kulikuwa na furaha katika Israeli.
Et même, ceux qui étaient le plus rapprochés d’eux, jusqu’à Issacar et à Zabulon et à Nephthali, apportaient des vivres sur des ânes et sur des chameaux et sur des mulets et sur des bœufs, des aliments de farine, des gâteaux de figues sèches, et des gâteaux de raisins secs, et du vin, et de l’huile, et du gros et du menu bétail en abondance; car il y avait de la joie en Israël.

< 1 Nyakati 12 >