< 1 Nyakati 12 >
1 Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,
And these [are] those coming to David at Ziklag, while shut up because of Saul son of Kish, and they [are] among the mighty ones, helping the battle,
2 walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):
armed with bow, right and left handed, with stones, and with arrows, with bows, of the brothers of Saul, of Benjamin.
3 Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,
The head [is] Ahiezer, and Joash, sons of Shemaab the Gibeathite, and Jeziel, and Pelet, sons of Azmaveth, and Berachah, and Jehu the Antothite,
4 na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,
and Ishmaiah the Gibeonite, a mighty one among the thirty, and over the thirty, and Jeremiah, and Jahaziel, and Johanan, and Josabad the Gederathite.
5 Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;
Eluzai, and Jerimoth, and Bealiah, and Shemariah, and Shephatiah the Haruphite;
6 Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;
Elkanah, and Jesiah, and Azareel, and Joezer, and Jashobeam the Korahites,
7 Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
and Joelah, and Zebadiah, sons of Jeroham of Gedor.
8 Baadhi ya Wagadi wakajitenga na kujiunga na Daudi katika ngome yake huko jangwani. Walikuwa mashujaa hodari, waliokuwa tayari kwa vita na wenye uwezo wa kutumia ngao na mkuki. Nyuso zao zilikuwa nyuso za simba na walikuwa na wepesi kama paa milimani.
And of the Gadite there have been separated to David, to the fortress, to the wilderness, mighty men of valor, men of the host for battle, setting in array buckler and spear, and their faces [are as] the face of the lion, and as roes on the mountains for speed:
9 Ezeri alikuwa mkuu wao, Obadia alikuwa wa pili katika uongozi, Eliabu wa tatu,
Ezer the head, Obadiah the second, Eliab the third,
10 Mishmana wa nne, Yeremia wa tano,
Mishmannah the fourth, Jeremiah the fifth,
11 Atai wa sita, Elieli wa saba,
Attai the sixth, Eliel the seventh,
12 Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa,
Johanan the eighth, Elzabad the ninth,
13 Yeremia wa kumi, na Makbanai wa kumi na moja.
Jeremiah the tenth, Machbannai the eleventh.
14 Hawa Wagadi walikuwa majemadari. Aliyekuwa wa mwisho kuliko wote aliweza kuongoza askari 100, na aliyekuwa na uweza zaidi ya wote aliongoza 1,000.
These [are] of the sons of Gad, heads of the host; the least [is] one of one hundred, and the greatest, of one thousand;
15 Wao ndio walivuka Mto Yordani katika mwezi wa kwanza ukiwa umefurika hadi kwenye kingo zake zote na kusababisha watu wote waliokuwa wanaishi kwenye mabonde kukimbilia mashariki na wengine magharibi.
these [are] they who have passed over the Jordan in the first month—and it is full over all its banks—and cause all [those in] the valley to flee to the east and to the west.
16 Wabenyamini wengine na baadhi ya watu kutoka Yuda pia walikuja kwa Daudi katika ngome yake.
And [some] from the sons of Benjamin and Judah came to David at the stronghold,
17 Daudi akatoka nje kuwalaki na akawaambia, “Kama mmekuja kwangu kwa amani, kunisaidia, mimi niko tayari kuwaruhusu ninyi kuungana nami. Lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa adui zangu wakati mimi mikono yangu haina hatia, basi Mungu wa baba zetu aone na awahukumu.”
and David goes out before them, and answers and says to them, “If you have come to me for peace, to help me, I have a heart to unite with you; and if to betray me to my adversaries—without violence in my hands—the God of our fathers sees and reproves.”
18 Kisha Roho akaja juu ya Amasai, mkuu wa wale Thelathini, naye akasema: “Sisi tu watu wako, ee Daudi! Nasi tuko pamoja na wewe, ee mwana wa Yese! Ushindi, naam, ushindi uwe kwako, pia ushindi kwa wale walio upande wako, kwa kuwa Mungu wako atakusaidia.” Kwa hiyo Daudi akawapokea na kuwafanya viongozi wa vikosi vyake vya uvamizi.
And the Spirit has clothed Amasai, head of the captains: “To you, O David, and with you, O son of Jesse—peace! Peace to you, and peace to your helper, for your God has helped you”; and David receives them, and puts them among the heads of the troop.
19 Baadhi ya watu kutoka kabila la Manase wakajiunga na Daudi wakati alikwenda pamoja na Wafilisti, kupigana na Sauli. (Daudi na watu wake hawakuwasaidia Wafilisti kwa sababu, baada ya ushauri, watawala wao walimrudisha. Wakasema, “Itatugharimu vichwa vyetu kama Daudi atatuasi na kurudi kwa Sauli bwana wake.”)
And [some] from Manasseh have defected to David in his coming with the Philistines against Israel to battle—and they did not help them, for by counsel the princes of the Philistines sent him away, saying, “He defects with our heads to his master Saul.”
20 Daudi alipokwenda Siklagi, hawa ndio watu wa kabila la Manase waliojiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai, viongozi wa vikosi vya watu 1,000 katika kabila la Manase.
In his going to Ziglag there have fallen to him from Manasseh: Adnah, and Jozabad, and Jediael, and Michael, and Jozabad, and Elihu, and Zillthai, heads of the thousands who [are] of Manasseh;
21 Walimsaidia Daudi dhidi ya makundi ya uvamizi, kwa kuwa wote walikuwa mashujaa hodari na walikuwa majemadari katika jeshi lake.
and they have helped with David over the troop, for all of them [are] mighty men of valor, and they are captains in the host,
22 Siku baada ya siku watu walikuja kumsaidia Daudi, mpaka akawa na jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
for at that time, day by day, they come to David to help him, until it is a great camp, like a camp of God.
23 Hawa ndio watu waliojiandaa kwa ajili ya vita waliokuja kwa Daudi huko Hebroni ili kumtwalia ufalme kutoka kwa Sauli, kama Bwana alivyokuwa amesema:
And these [are] the numbers of the head, of the armed men of the host; they have come to David at Hebron to turn around the kingdom of Saul to him, according to the mouth of YHWH.
24 watu wa Yuda, wanaochukua ngao na mikuki walikuwa 6,800 wote wakiwa tayari kwa vita.
The sons of Judah, carrying buckler and spear, [are] six thousand and eight hundred, armed ones of the host.
25 Watu wa Simeoni, mashujaa waliokuwa tayari kwa vita walikuwa 7,100.
Of the sons of Simeon, mighty men of valor for the host, [are] seven thousand and one hundred.
26 Watu wa Lawi walikuwa 4,600,
Of the sons of Levi [are] four thousand and six hundred;
27 pamoja na Yehoyada, kiongozi wa jamaa ya Aroni, aliyekuwa pamoja na watu 3,700,
and Jehoiada [is] the leader of the Aaronite, and with him [are] three thousand and seven hundred,
28 na Sadoki, kijana shujaa na hodari, aliyekuwa pamoja na maafisa ishirini na wawili kutoka jamaa yake.
and Zadok, a young man, a mighty man of valor, and of the house of his father [are] twenty-two heads.
29 Watu wa Benyamini, ndugu zake Sauli, walikuwa 3,000; wengi wao walikuwa wameendelea kuwa waaminifu kwa Sauli mpaka wakati huo.
And of the sons of Benjamin, brothers of Saul, [are] three thousand, and until now their greater part are keeping the charge of the house of Saul.
30 Watu wa Efraimu, mashujaa hodari 20,800, watu waliokuwa maarufu katika koo zao.
And of the sons of Ephraim [are] twenty thousand and eight hundred, mighty men of valor, men of renown, according to the house of their fathers.
31 Watu wa nusu ya kabila la Manase, waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme, watu 18,000.
And of the half of the tribe of Manasseh [are] eighteen thousand, who have been defined by name, to come to cause David to reign.
32 Watu wa Isakari, waliofahamu majira na kujua kile ambacho Israeli inapasa kufanya, walikuwa viongozi 200, pamoja na jamaa zao wote chini ya uongozi wao.
And of the sons of Issachar, having understanding for the times, to know what Israel should do; their heads [are] two hundred, and all their brothers [are] at their command.
33 Watu wa Zabuloni, askari wenye uzoefu mkubwa walioandaliwa tayari kwa vita wakiwa na silaha za kila aina, ili kumsaidia Daudi kwa uaminifu thabiti, walikuwa 50,000.
Of Zebulun, going forth to the host, arranging battle with all instruments of battle, [are] fifty thousand, and keeping rank without a double heart.
34 Watu wa Naftali, maafisa 1,000, pamoja na watu 37,000 waliochukua ngao na mikuki.
And of Naphtali, one thousand heads, and with them, with buckler and spear, [are] thirty-seven thousand.
35 Watu wa Dani 28,600 waliokuwa tayari kwa vita.
And of the Danite, arranging battle, [are] twenty-eight thousand and six hundred.
36 Watu wa Asheri, askari 40,000 wenye uzoefu mkubwa waliondaliwa kwa ajili ya vita.
And of Asher, going forth to the host, to arrange battle, [are] forty thousand.
37 Na pia watu kutoka mashariki ya Yordani, watu wa Reubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakiwa na kila aina ya silaha, watu 120,000.
And from beyond the Jordan, of the Reubenite, and of the Gadite, and of the half of the tribe of Manasseh, with all instruments of the host for battle, [are] one hundred and twenty thousand.
38 Wote hawa walikuwa watu wapiganaji waliojitolea kutumika katika safu zao. Walikuja Hebroni wakiwa wameamua kikamilifu kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli yote. Waisraeli wengine wote walikuwa pia na nia hiyo moja ya kumfanya Daudi kuwa mfalme.
All these [are] men of war, keeping rank—they have come to Hebron with a perfect heart, to cause David to reign over all Israel, and also all the rest of Israel [are] of one heart, to cause David to reign,
39 Watu hawa wakakaa huko na Daudi siku tatu, wakila na kunywa, kwa sababu jamaa zao zilikuwa zimewapatia mahitaji yao.
and they are there, with David, three days, eating and drinking, for their brothers have prepared for them.
40 Pia, majirani zao hata wale walio mbali hadi Isakari, Zabuloni na Naftali, walikuja wakiwaletea vyakula walivyovibeba kwa punda, ngamia, nyumbu na maksai. Kulikuwepo na wingi wa unga, maandazi ya tini, maandazi ya zabibu kavu, divai, mafuta, ngʼombe na kondoo, kwa maana kulikuwa na furaha katika Israeli.
And also those near to them—to Issachar, and Zebulun, and Naphtali—are bringing in bread on donkeys, and on camels, and on mules, and on oxen—food of fine flour, fig-cakes and grape-cakes, and wine, and oil, and oxen, and sheep, in abundance, for joy [is] in Israel.