< 1 Nyakati 12 >
1 Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,
Tito pak jsou, kteříž přišli k Davidovi do Sicelechu, když se ještě kryl před Saulem synem Cis, a ti byli mezi udatnými, pomocníci boje,
2 walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):
Nosíce lučiště, a bojujíce pravicí i levicí kamením i střelami z lučiště, a byli z bratří Saulových, z pokolení Beniaminova:
3 Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,
Kníže Achiezer a Joas, synové Semmaa Gabatského, a Jeziel a Felet, synové Azmavetovi, Beracha, a Jéhu Anatotský,
4 na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,
A Ismaiáš Gabaonitský, silný mezi třidcíti, kterýž byl nad třidcíti, Jeremiáš, Jachaziel, Jochanan a Jozabad Gederatský,
5 Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;
A Eluzai, Jerimot, Bealiáš, Semariáš, a Sefatiáš Charufský,
6 Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;
Elkána, Isiáš, Azareel, Joezer a Jasobam, Chorejští,
7 Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
A Joela a Zebadiáš synové Jerochamovi z Gedor.
8 Baadhi ya Wagadi wakajitenga na kujiunga na Daudi katika ngome yake huko jangwani. Walikuwa mashujaa hodari, waliokuwa tayari kwa vita na wenye uwezo wa kutumia ngao na mkuki. Nyuso zao zilikuwa nyuso za simba na walikuwa na wepesi kama paa milimani.
Též i z pokolení Gádova utekli k Davidovi k pevnosti na poušť, muži udatní, muži způsobní k boji, užívajíce štítu a pavézy, jichžto tváři jako tváři lvové, a podobní srnám na horách v rychlosti:
9 Ezeri alikuwa mkuu wao, Obadia alikuwa wa pili katika uongozi, Eliabu wa tatu,
Ezer první, Abdiáš druhý, Eliab třetí,
10 Mishmana wa nne, Yeremia wa tano,
Mismanna čtvrtý, Jeremiáš pátý,
11 Atai wa sita, Elieli wa saba,
Attai šestý, Eliel sedmý,
12 Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa,
Jochanan osmý, Elzabad devátý,
13 Yeremia wa kumi, na Makbanai wa kumi na moja.
Jeremiáš desátý, Machbannai jedenáctý.
14 Hawa Wagadi walikuwa majemadari. Aliyekuwa wa mwisho kuliko wote aliweza kuongoza askari 100, na aliyekuwa na uweza zaidi ya wote aliongoza 1,000.
Ti byli z synů Gádových, knížata vojska, jeden nad stem menší, a větší nad tisícem.
15 Wao ndio walivuka Mto Yordani katika mwezi wa kwanza ukiwa umefurika hadi kwenye kingo zake zote na kusababisha watu wote waliokuwa wanaishi kwenye mabonde kukimbilia mashariki na wengine magharibi.
Ti jsou, kteříž přepravili se přes Jordán měsíce prvního, ačkoli se byl vylil ze všech břehů svých, a zahnali všecky z údolí na východ i na západ.
16 Wabenyamini wengine na baadhi ya watu kutoka Yuda pia walikuja kwa Daudi katika ngome yake.
Přišli také někteří z synů Beniaminových a Judových k pevnosti Davidově.
17 Daudi akatoka nje kuwalaki na akawaambia, “Kama mmekuja kwangu kwa amani, kunisaidia, mimi niko tayari kuwaruhusu ninyi kuungana nami. Lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa adui zangu wakati mimi mikono yangu haina hatia, basi Mungu wa baba zetu aone na awahukumu.”
I vyšel jim David vstříc, a mluvě, řekl jim: Jestliže z příčiny pokoje jdete ke mně, abyste mi pomáhali, i mé srdce také s vámi se sjednotí; pakli k vyzrazení mne nepřátelům mým, (ješto není nepravosti při mně), popatřiž Bůh otců našich a tresci.
18 Kisha Roho akaja juu ya Amasai, mkuu wa wale Thelathini, naye akasema: “Sisi tu watu wako, ee Daudi! Nasi tuko pamoja na wewe, ee mwana wa Yese! Ushindi, naam, ushindi uwe kwako, pia ushindi kwa wale walio upande wako, kwa kuwa Mungu wako atakusaidia.” Kwa hiyo Daudi akawapokea na kuwafanya viongozi wa vikosi vyake vya uvamizi.
Duch pak posilnil Amazu předního mezi hejtmany, i řekl: Tobě, ó Davide, a těm, jenž s tebou jsou, synu Izai, pokoj; pokoj tobě, pokoj i pomocníkům tvým. Toběť zajisté pomáhá Bůh tvůj. A tak přijal je David, a postavil je mezi knížaty houfů.
19 Baadhi ya watu kutoka kabila la Manase wakajiunga na Daudi wakati alikwenda pamoja na Wafilisti, kupigana na Sauli. (Daudi na watu wake hawakuwasaidia Wafilisti kwa sababu, baada ya ushauri, watawala wao walimrudisha. Wakasema, “Itatugharimu vichwa vyetu kama Daudi atatuasi na kurudi kwa Sauli bwana wake.”)
Nadto i z pokolení Manassesova odstoupili k Davidovi, když táhl s Filistinskými k boji proti Saulovi, ale nepomáhali jim. Nebo uradivše se, propustili ho zase knížata Filistinská, řkouce: S nebezpečenstvím hrdel našich odstoupil by ku pánu svému Saulovi.
20 Daudi alipokwenda Siklagi, hawa ndio watu wa kabila la Manase waliojiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai, viongozi wa vikosi vya watu 1,000 katika kabila la Manase.
Takž když táhl do Sicelechu, odstoupili k němu někteří z pokolení Manassesova: Adnach, Jozabad, Jediael, Michael, Jozabad, Elihu, a Zilletai, hejtmané nad tisíci v pokolení Manassesovu.
21 Walimsaidia Daudi dhidi ya makundi ya uvamizi, kwa kuwa wote walikuwa mashujaa hodari na walikuwa majemadari katika jeshi lake.
Ti také pomáhali Davidovi s houfy jeho; nebo udatní byli všickni, pročež byli knížaty v jeho vojště.
22 Siku baada ya siku watu walikuja kumsaidia Daudi, mpaka akawa na jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
Anobrž každého dne přibývalo jich Davidovi ku pomoci, až bylo vojsko veliké, jako vojsko Boží.
23 Hawa ndio watu waliojiandaa kwa ajili ya vita waliokuja kwa Daudi huko Hebroni ili kumtwalia ufalme kutoka kwa Sauli, kama Bwana alivyokuwa amesema:
Tento pak jest počet vývod způsobných k boji, kteříž přišli k Davidovi do Hebronu, aby obrátili království Saulovo k němu podlé slova Hospodinova.
24 watu wa Yuda, wanaochukua ngao na mikuki walikuwa 6,800 wote wakiwa tayari kwa vita.
Z synů Judových, nosících pavézy a kopí, šest tisíc a osm set způsobných k boji.
25 Watu wa Simeoni, mashujaa waliokuwa tayari kwa vita walikuwa 7,100.
Z synů Simeonových, udatných mužů k boji, sedm tisíc a sto.
26 Watu wa Lawi walikuwa 4,600,
Z synů Léví čtyři tisíce a šest set.
27 pamoja na Yehoyada, kiongozi wa jamaa ya Aroni, aliyekuwa pamoja na watu 3,700,
Joiada také vývoda synů Aronových, a s ním tři tisíce a sedm set.
28 na Sadoki, kijana shujaa na hodari, aliyekuwa pamoja na maafisa ishirini na wawili kutoka jamaa yake.
A Sádoch mládenec rek udatný, a z domu otce jeho knížat dvamecítma.
29 Watu wa Benyamini, ndugu zake Sauli, walikuwa 3,000; wengi wao walikuwa wameendelea kuwa waaminifu kwa Sauli mpaka wakati huo.
A z synů Beniaminových, bratří Saulových tři tisíce; nebo ještě množství jiných drželi stráž domu Saulova.
30 Watu wa Efraimu, mashujaa hodari 20,800, watu waliokuwa maarufu katika koo zao.
Z synů též Efraimových dvadceti tisíc a osm set. Ti byli rekové udatní, muži slovoutní v čeledech otců svých.
31 Watu wa nusu ya kabila la Manase, waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme, watu 18,000.
Z polovice pak pokolení Manassesova osmnáct tisíc, kteříž vyčteni byli ze jména, aby přišli a ustanovili Davida za krále.
32 Watu wa Isakari, waliofahamu majira na kujua kile ambacho Israeli inapasa kufanya, walikuwa viongozi 200, pamoja na jamaa zao wote chini ya uongozi wao.
Z synů také Izacharových, znajících a rozumějících časům, tak že věděli, co by měl činiti lid Izraelský, knížat jejich dvě stě, a všickni bratří jejich činili podlé rčení jejich.
33 Watu wa Zabuloni, askari wenye uzoefu mkubwa walioandaliwa tayari kwa vita wakiwa na silaha za kila aina, ili kumsaidia Daudi kwa uaminifu thabiti, walikuwa 50,000.
Z synů Zabulon vycházejících na vojnu, vycvičených v bitvě všelijakými nástroji válečnými, padesáte tisíc, a ku potýkání se v šiku bez choulostivosti srdce.
34 Watu wa Naftali, maafisa 1,000, pamoja na watu 37,000 waliochukua ngao na mikuki.
Z Neftalímova pak pokolení knížat tisíc, a s nimi pavézníků a kopidlníků třidceti a sedm tisíc.
35 Watu wa Dani 28,600 waliokuwa tayari kwa vita.
Z pokolení Dan, způsobných k boji, osm a dvadceti tisíc a šest set.
36 Watu wa Asheri, askari 40,000 wenye uzoefu mkubwa waliondaliwa kwa ajili ya vita.
A z pokolení Asserova, kteříž způsobní byli k boji, a umělí v šikování se k bitvě, čtyřidceti tisíc.
37 Na pia watu kutoka mashariki ya Yordani, watu wa Reubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakiwa na kila aina ya silaha, watu 120,000.
A z Zajordání, totiž z Rubenských a Gádských, a z polovice pokolení Manassesova, přišli se všemi nástroji válečnými sto a dvadceti tisíc.
38 Wote hawa walikuwa watu wapiganaji waliojitolea kutumika katika safu zao. Walikuja Hebroni wakiwa wameamua kikamilifu kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli yote. Waisraeli wengine wote walikuwa pia na nia hiyo moja ya kumfanya Daudi kuwa mfalme.
Všickni ti muži bojovní, umělí v šiku, úmyslem upřímým přišli do Hebronu, aby ustanovili Davida za krále nade vším lidem Izraelským. Nýbrž i všickni ostatní Izraelští srdce jednoho byli, aby za krále ustanovili Davida.
39 Watu hawa wakakaa huko na Daudi siku tatu, wakila na kunywa, kwa sababu jamaa zao zilikuwa zimewapatia mahitaji yao.
I byli tu s Davidem tři dni, jedouce a pijíce, nebo jim byli připravili bratří jejich.
40 Pia, majirani zao hata wale walio mbali hadi Isakari, Zabuloni na Naftali, walikuja wakiwaletea vyakula walivyovibeba kwa punda, ngamia, nyumbu na maksai. Kulikuwepo na wingi wa unga, maandazi ya tini, maandazi ya zabibu kavu, divai, mafuta, ngʼombe na kondoo, kwa maana kulikuwa na furaha katika Israeli.
Ano i ti, kteříž jim blízcí byli až k Izachar a Zabulon a Neftalím, přinášeli chleba na oslích a na velbloudích, i na mezcích a na volích, potravy, mouky, fíků a hroznů sušených, vína, oleje, volů, a ovcí v hojnosti. Nebo radost byla v lidu Izraelském.