< 1 Nyakati 11 >
1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
Entonces todo Israel se reunió con David en Hebrón y dijo: En verdad, somos tu hueso y tu carne.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
En el pasado, cuando Saúl era rey, eras tú a la cabeza de Israel cuando salían o regresaban; Y el SEÑOR tu Dios te dijo: Tú debes de alimentar a mi pueblo Israel y gobernarlo.
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
Entonces todos los responsables de Israel vinieron al rey en Hebrón; y David llegó a un acuerdo con ellos en Hebrón delante del Señor; y pusieron el aceite santo sobre David y lo hicieron rey sobre Israel, como el Señor lo había dicho por Samuel.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
Entonces David y todo Israel fueron a Jerusalén (que es Jebus); y los jebuseos, la gente de la tierra, estaban allí.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
Y la gente de Jebus dijo a David: No entrarás aquí. Pero aún así, David tomó el lugar fuerte de Sión, que es la ciudad de David.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
Y David dijo: El primero en vencer a los jebuseos será el jefe y el capitán. Y Joab, el hijo de Sarvia, subió primero, y llegó a ser jefe.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
Y David tomó la fortaleza para su lugar de vida, por lo que se llamó la ciudad de David.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
Y construyó David la ciudad alrededor, comenzando desde el terraplén todo alrededor; Y Joab reparó el resto del pueblo.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
Y David se hizo cada vez más grande en poder, porque el Señor de los ejércitos estaba con él.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
Ahora, estos son los principales hombres de guerra de David, quienes fueron sus fuertes partidarios en el reino y, con todo Israel, lo hicieron rey, como el Señor había dicho acerca de Israel.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
Esta es la lista de los hombres de guerra de David: Jasobeam, el hijo de Hacmoni, el jefe de los tres: mató a trescientos a la vez con su lanza.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
Después de él, Eleazar, hijo de Dodo el ahohíta, fue uno de los tres grandes combatientes.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
Estaba con David en Pas-damim, donde los filisteos se habían reunido para la lucha, cerca de un pedazo de tierra llena de cebada; Y el pueblo huyó ante los filisteos.
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
Tomó su posición en medio del campo, contuvo su ataque y venció a los filisteos; y el Señor dio gran victoria.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Y tres de los treinta bajaron a David, a la roca, al lugar fuerte de Adulam; y el ejército de los filisteos había tomado su posición en el valle de Refaim.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
En ese momento, David se había puesto a cubierto en una fortaleza, y una fuerza armada de los filisteos estaba en Belén.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
Y David, conmovido por un fuerte deseo, dijo: ¡Si alguien me diera un trago del agua del pozo de agua de Belén junto a la puerta de entrada a la ciudad!
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
Así que los tres, abriéndose paso a través del ejército filisteo, tomaron agua del pozo de agua de Belén, junto a la entrada de la ciudad, y se la llevaron a David; pero David no la tomó, sino que hizo una ofrenda, la derramó al Señor,
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
Diciendo: ¡Dios mío, lejos de mí hacer esto! ¿Cómo puedo tomar como bebida la sangre vital de estos hombres que han puesto sus vidas en peligro? así que no lo tomó. Estas cosas hicieron los tres grandes hombres de guerra.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
Y Abisai, el hermano de Joab, era el jefe de los treinta, porque mató a trescientos con su lanza, y tuvo fama entre los tres.
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
De los treinta, él era el más noble, y fue nombrado su capitán, pero no era igual a los tres primeros.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Benaía, el hijo de Joiada, un guerrero de Cabseel, había hecho grandes actos; mató a dos hombres de Moab fieros como leones entrando en su lugar secreto; también descendió a un agujero y mató a un león en tiempo de nieve.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
E hizo un ataque a un egipcio, un hombre muy alto, de unos cinco codos de altura, armado con una lanza que parecía él rodillo de un telar; Bajó a él con un palo y sacando su lanza de la mano del egipcio, lo mató con esa misma lanza.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
Estos fueron los hechos de Benaía, el hijo de Joiada, que tuvo un gran nombre entre los treinta hombres de guerra.
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
Fue honrado con los treinta, pero fue más distinguido que los tres primeros; y David lo puso sobre él mando de su guardia personal.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Y estos eran los grandes hombres de guerra: Asael, el hermano de Joab, Elhanán, el hijo de Dodo de Belén,
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Samot de Harod, Heles el Paltita,
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Ira, el hijo de Iques, de Tecoa, Abiezer, de Anatot,
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sibecai, de Husa, Ilai, el Ahohita,
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Maharai, de Netofa, Heled, el hijo de Baana de Netofa,
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Itai, el hijo de Ribai, de Gabaa, de los hijos de Benjamín, Benaía, de Piraton,
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Hidai, del arroyo de gaas, Abiel, el Arbatita;
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Azmavet, de Bahurim, Eliaba, Saalbonita,
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
Los hijos de Jasén, el Gizonita, Jonatán, hijo de Sage él ararita,
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Ahiam, el hijo de Sacar el ararita, Elifal, el hijo de Ur,
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Hefer mequeratita, Ahías, pelonita.
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hezrai de carmel, Naarai, el hijo de Ezbai,
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Joel, el hermano de Natán, Mibhar, el hijo de Hagrai,
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Selec el Amonita, y Naharai, el Berot, el siervo que cuidaba las armas de Joab, el hijo de Sarvia;
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ira, de Jatir; Gareb de Jatir;
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Urías el hitita, Zabad, el hijo de Ahlai,
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adina, hijo de Siza, el Rubénita, jefe de los rubenitas, y treinta hombres con él;
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanán, el hijo de Maaca, y Josafat, el mitnita.
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Uzia de Astarot, Sama y Jehiel, los hijos de Hotham de Aroer,
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Jediael, el hijo de Simri, y Joha su hermano, el tizita,
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Eliel el Mahanaiam, Jeribai y Josavia, los hijos de Elnaam, e Itma el Moabita.
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Eliel y Obed, y Jaasiel de Soba.