< 1 Nyakati 11 >

1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
И собрася весь Израиль к Давиду в Хеврон, глаголюще: се, кости твоя и плоть твоя мы:
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
вчера же и третияго дне, егда еще царствоваше Саул, ты был еси изводяй и вводяй Израиля, и тебе рече Господь Бог твой: ты упасеши люди Моя Израиля, и ты будеши князь над людьми Моими Израилем.
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
И приидоша вси старейшины Израилевы ко царю в Хеврон: и утверди Давид с ними завет в Хевроне пред Господем: и помазаша Давида в царя над Израилем по словеси Господню, (еже глагола) рукою Самуиловою.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
И иде царь Давид и весь Израиль во Иерусалим, сей есть Иевус, идеже бяху Иевусее жителие земли.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
Рекоша же Давиду, иже обиташа в Иевусе: не внидеши семо. И взя Давид крепость Сионю, яже есть град Давидов.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
Рече же Давид: всяк иже убиет Иевусеа в первых, будет князь и воевода. И взыде нань прежде Иоав сын Саруиев и бысть князем.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
И седе Давид во обдержании: сего ради именова е град Давидов.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
И созда град окрест от Маала даже да окружения: Иоав же прочее града сострои: и воева и взя град.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
Преспеваше же Давид идый и растый, и Господь Вседержитель бе с ним.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
Сии же князи сильных Давидовых, иже помогаху ему в царстве его со всем Израилем, да царь будет по словеси Господню, над Израилем,
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
и сие число крепких Давидовых: Иесваал сын Ахамань, первый между тридесятми: той извлече мечь свой единожды на триста язвеных во едино время.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
И по нем Елеазар, сын Додеа Ахохии: сей бе между треми сильными:
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
сей бе с Давидом в Фасодомине, идеже иноплеменницы собрани быша на брань, и бе часть нивы полна ячменя, и людие побегоша от лица иноплеменнича:
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
и ста посреде части и защити ю, и изби иноплеменники, и сотвори Господь спасение велие (людем Своим).
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Снидоша же тии трие от тридесяти князей на камень ко Давиду в пещеру Одолламлю, а полк иноплеменничь стояше во юдоли Гигантов.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
Давид же бе тогда в крепости, полк же иноплеменничь бе тогда в Вифлееме.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
И возжада Давид и рече: кто напоит мя водою от кладязя Вифлеемска, иже есть во вратех?
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
И трие тии проторгошася сквозе полк иноплеменничь и почерпоша воду из кладязя, иже в Вифлееме, иже бе во вратех, и взяша и принесоша к Давиду, да пиет. И не восхоте Давид пити ея и возлия ю Господеви
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
и рече: милостив ми Бог, еже сотворити глагол сей: аще кровь мужей сих испию в душах их, понеже душами своими принесоша. И не восхоте пити ея. Сие сотвориша трие сильнии.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
И Авесса брат Иоавль, той бе первый в триех: сей извлече мечь свой противу триех сот мужей во един час и уби их, и той бе посреде триех именит:
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
от триех между двема преславный, и бе им началник, обаче ко трием первым не достиже.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
И Ванеа сын Иодаев, сын мужа крепкаго, многа дела его, от Каваслила: той уби двоих Ариилов Моавских, и той сниде и уби льва у кладязя во время снега:
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
и той уби мужа Египтянина, емуже возраст бе пять лакот, и в руце Египтянина копие яко вратило ткущих: и сниде к нему Ванеа с жезлом, и восхити копие из руки Египтянина и уби его копием его:
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
сия сотвори Ванеа сын Иодаев, и бе именит посреде триех сильных:
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
над тридесятию бе славен сей, а ко трием не достиже: и постави его Давид над отечеством своим.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
И сильнии сил: Асаил, брат Иоавль, Елеанан, сын Додоев от Вифлеема,
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Саммоф Аддитянин, Хелкий Афелонин,
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Орей сын от Киса Фекуйский, Авиезер Анафофский,
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Совохай Асофийский, Илий Ахойский,
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Воорай сын Нетофафиев, Еллаф сын Ваинака Нетофафийскаго,
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Ифай сын Ривеин от холма Вениаминя, Ванеа сын Фарафониев,
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Урий от Неали, Галсавиил Аравефийский,
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Азмоф Варсамийский, Елиава Саламийский,
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
Ирас Гоинийский, Ионафан сын Саги Арарийский,
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Ахиам сын Сахара Арарийскаго, Зифаал сын Орин,
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Афер Мехурафинский, Ахиа Фелонийский,
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Асарай Мармелинский, Ноорай сын Авдиев,
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Иоиль брат Нафанов, Мавар сын Тараиев,
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Селлик Аммониин, Наарей Вирофин, иже носил оружие Иоава сына Саруиева,
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ира Иефериин, Гарив Фериин,
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Уриа Хетфейский, Вазаф сын Оолиев,
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Адина сын Саха, Рувима князь, и у него тридесять,
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Анан сын Маахин, и Иосафат Фафаин,
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Озиа Астарофин, Самма и Иеил сынове Хофана Арариина,
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Иедиил сын Саамерин, и Иозае брат его Фосаин,
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Иелиил Маоин, и Арива, и Осоиа сын его, Енаам, и Иефема Моавитский,
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Елиил, и Овид, и Иесиил Месовиев.

< 1 Nyakati 11 >