< 1 Nyakati 11 >
1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
E TUTTO Israele si adunò appresso di Davide in Hebron, dicendo: Ecco, noi [siamo] tue ossa, e tua carne.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
Ed anche per addietro, eziandio mentre Saulle era re, tu [eri] quel che conducevi Israele fuori e dentro; e il Signore Iddio tuo ti ha detto: Tu pascerai il mio popolo Israele, e sarai il conduttore del mio popolo Israele.
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
Essendo adunque venuti tutti gli Anziani d'Israele al re in Hebron, Davide patteggiò quivi con loro, in presenza del Signore; ed essi unsero Davide per re sopra Israele, secondo la parola del Signore [pronunziata] per Samuele.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
Poi Davide andò con tutto Israele in Gerusalemme, che [è] Gebus; e quivi [erano] i Gebusei, che abitavano in quel paese.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
E gli abitanti di Gebus dissero a Davide: Tu non entrerai qua entro. Ma Davide prese la fortezza di Sion, che [è] la Città di Davide.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
Or Davide avea detto: Chiunque percoterà il primo i Gebusei sarà Capo e Capitano. E Ioab, figliuolo di Seruia, salì il primo; onde fu fatto Capo.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
E Davide abitò in quella fortezza; e perciò ella fu chiamata: La Città di Davide.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
Ed egli edificò la città d'ogn'intorno, dal terrapieno fino a tutto il ricinto; e Ioab rifece il rimanente della città.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
E Davide andava del continuo crescendo, e il Signore degli eserciti [era] con lui.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
OR questi [sono] i principali de' prodi di Davide, i quali si portarono valorosamente appresso di lui nel suo regno, con tutto Israele, per farlo re, secondo che il Signore avea promesso ad Israele.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
E questo [è] il numero de' prodi di Davide: Iasobam, figliuolo di Hacmoni, Capo de' colonnelli; costui mosse la sua lancia contro a trecent'[uomini], e li uccise a una volta.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
E dopo lui, [era] Eleazaro, figliuolo di Dodo, Ahoheo, [il quale] era di que' tre prodi.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
Costui si trovò con Davide in Pasdammim, quando i Filistei si erano quivi adunati in battaglia. Or quivi era un campo pieno d'orzo; ed essendo il popolo fuggito d'innanzi a' Filistei,
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
essi si presentarono [alla battaglia] in mezzo del campo, e lo riscossero, e percossero i Filistei; e il Signore diede una gran vittoria.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Oltre a ciò, questi tre, [ch'erano] capi sopra i trenta, andarono alla rocca, a Davide, nella spelonca di Adullam, essendo il campo de' Filistei posto nella valle de' Rafei.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
E Davide [era] allora nella fortezza, ed i Filistei in quel tempo aveano guernigione in Bet-lehem.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
E Davide fu mosso da desiderio, e disse: Chi mi darà a bere dell'acqua della cisterna di Bet-lehem, ch'[è] alla porta?
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
E que' tre penetrarono nel campo de' Filistei, ed attinsero dell'acqua della cisterna di Bet-lehem, ch'[è] alla porta; e la portarono, e la presentarono a Davide; ma egli non ne volle bere, anzi la sparse al Signore, e disse:
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
Tolga ciò l'Iddio mio da me, che io faccia questo; berrei io il sangue di questi uomini che [sono andati là] al rischio della lor vita? conciossiachè abbiano recata quest'[acqua] al rischio della lor vita; e non ne volle bere. Queste cose fecero que' tre uomini prodi.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
Abisai anch'esso, fratello di Ioab, [era] il principale fra [altri] tre. Esso ancora mosse la sua lancia contro a trecent' [uomini], e li uccise, e fu famoso fra que' tre.
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
Fra que' tre egli era più illustre che i due [altri], e fu lor capo; ma pur non arrivò a quegli [altri] tre.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
[Poi vi era] Benaia, figliuolo di Gioiada, figliuolo d'un uomo valoroso; e [Benaia] avea fatte di gran prodezze, [ed era] da Cabseel. Egli percosse i due Ariel di Moab; scese ancora, e percosse un leone in mezzo d'una fossa, al tempo della neve.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
Egli percosse ancora un uomo Egizio, [il quale era] uomo di grande statura, [cioè], di cinque cubiti. Or quell'Egizio avea in mano una lancia simile ad un subbio di tessitore; ma [Benaia] scese contro a lui con un bastone, e gli strappò la lancia di mano, e l'uccise con la sua propria lancia.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
Queste cose fece Benaia, figliuolo di Gioiada, e fu famoso fra i tre prodi.
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
Ecco, egli era elevato in dignità sopra i trenta; ma pur non arrivò a quegli [altri] tre. E Davide lo costituì sopra la gente ch'egli avea del continuo a suo comando.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Poi [vi erano] gli [altri] prodi degli eserciti, [cioè: ] Asael, fratello di Ioab; Elhanan, figliuolo di Dodo, da Bet-lehem;
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Sammot Harodita; Heles Pelonita;
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Ira, figliuolo d'Iches Tecoita; Abiezer Anatotita;
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sibbecai Husatita;
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Ilai Ahohita; Maharai Netofatita; Heled, figliuolo di Baana, Netofatita;
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Itai, figliuolo di Ribai, da Ghibea de' figliuoli di Beniamino; Benaia Piratonita;
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Hurai, delle valli di Gaas; Abiel Arbatita;
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Azmavet Baharumita; Eliaba Saalbonita;
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
il Ghizonita, de' figliuoli di Hazem; Gionatan, figliuolo di Saghe, Hararita;
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Ahiam, figliuolo di Sacar, Hararita; Elifal, figliuolo di Ur;
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Hefer Mecheratita; Ahia Pelonita;
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hesro Carmelita; Naarai, figliuolo di Ezbai;
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Ioel, fratello di Natan; Mibar, figliuolo di Hagri;
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Selec Ammonita; Naarai Berotita, scudiere di Ioab, figliuolo di Seruia;
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ira Itrita; Gareb Itrita;
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Uria Hitteo; Zabad, figliuolo di Alai;
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adina, figliuolo di Siza, Rubenita, [ch'era] capo de' Rubeniti; e [ne avea] trent'[altri] seco;
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanan, figliuolo di Maaca; Giosafat Mitnita;
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Uzzia Asteratita; Sama, e Ieiel, figliuoli di Hotam, Aroerita;
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Iediael, figliuolo di Simri, e Ioha, suo fratello, Tisita;
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Eliel Hammahavim; e Ieribai, e Iosavia, figliuoli di Elnaam; Itma Moabita;
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Eliel, ed Obed, e Iaasiel da Mesobaia.