< 1 Nyakati 11 >
1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
Or, tout Israël s'assembla vers David, à Hébron, en disant: Voici nous sommes tes os et ta chair;
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
Même ci-devant, quand Saül était roi, c'est toi qui faisais sortir et qui ramenais Israël. Et l'Éternel, ton Dieu, t'a dit: Tu paîtras mon peuple d'Israël, et tu seras le chef de mon peuple d'Israël.
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
Tous les anciens d'Israël vinrent donc vers le roi à Hébron, et David fit alliance avec eux à Hébron, devant l'Éternel; et ils oignirent David pour roi sur Israël, selon la parole de l'Éternel, prononcée par Samuel.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
Puis David marcha avec tout Israël sur Jérusalem, qui est Jébus; là étaient les Jébusiens, habitants du pays.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
Et les habitants de Jébus dirent à David: Tu n'entreras point ici. Mais David s'empara de la forteresse de Sion; c'est la cité de David.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
Or, David avait dit: Quiconque aura battu le premier les Jébusiens, sera chef et prince. Joab, fils de Tséruja, monta le premier, et il devint chef.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
Et David habita dans la forteresse; c'est pourquoi on l'appela la cité de David.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
Il bâtit la ville tout autour, depuis Millo et aux environs; et Joab répara le reste de la ville.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
Et David allait s'avançant et grandissant, et l'Éternel des armées était avec lui.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
Voici les chefs des hommes vaillants qu'avait David, et qui l'aidèrent, avec tout Israël, dans sa royauté, pour le faire régner, selon la parole de l'Éternel au sujet d'Israël.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
Voici donc le nombre des hommes vaillants qu'avait David: Jashobeam, fils de Hacmoni, chef de ceux qui combattaient sur des chars. Il brandit sa lance sur trois cents hommes, qu'il fit périr en une seule fois.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
Après lui, Éléazar, fils de Dodo, l'Achochite, l'un des trois hommes vaillants.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
C'est lui qui était avec David à Pas-Dammin, où les Philistins s'étaient assemblés pour combattre. Il y avait une portion de champ remplie d'orge; et le peuple fuyait devant les Philistins.
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
lls se placèrent au milieu du champ, le défendirent, et battirent les Philistins. Et l'Éternel accorda une grande délivrance.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Trois des trente chefs descendirent sur le rocher, vers David, dans la caverne d'Adullam, lorsque le camp des Philistins était dressé dans la vallée des Réphaïm.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
David était alors dans la forteresse, tandis qu'une garnison des Philistins était à Bethléhem.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
Et David fit un souhait, et dit: Qui me fera boire de l'eau du puits qui est à la porte de Bethléhem?
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
Alors ces trois hommes passèrent au travers du camp des Philistins, et puisèrent de l'eau du puits qui est à la porte de Bethléhem; et l'ayant apportée, ils la présentèrent à David; mais David ne voulut pas la boire, et il la répandit devant l'Éternel.
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
Et il dit: Que mon Dieu me garde de faire cela! Boirais-je le sang de ces hommes qui sont allés au péril de leur vie? Car ils m'ont apporté cette eau au péril de leur vie. Et il ne voulut pas la boire. Voilà ce que firent ces trois hommes vaillants.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
Abishaï, frère de Joab, était le chef des trois. Il brandit sa lance sur trois cents hommes, qu'il frappa à mort; et il eut du renom parmi les trois.
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
Entre les trois il fut plus honoré que les deux autres, et fut leur chef; toutefois, il n'égala point les trois premiers.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Bénaja, fils de Jéhojada, fils d'un homme vaillant, grand par ses exploits, de Kabtséel. Il tua deux des plus puissants hommes de Moab. Il descendit aussi et tua un lion, au milieu d'une fosse, en un jour de neige.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
Il frappa un Égyptien dont la stature était de cinq coudées. L'Égyptien avait en sa main une lance comme une ensuble de tisserand; il descendit vers lui avec un bâton, arracha la lance de la main de l'Égyptien, et le tua de sa propre lance.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
Voilà ce que fit Bénaja, fils de Jéhojada, et il eut un nom parmi ces trois vaillants hommes.
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
Il était le plus honoré des trente, mais il n'égala pas les trois premiers. David le mit en son conseil privé.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Hommes vaillants de l'armée: Asaël, frère de Joab; Elchanan, fils de Dodo, de Bethléhem;
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Shammoth, Harorite; Hélets, Pélonien;
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Ira, fils d'Ikkèsh, Thékoïte; Abiézer, d'Anathoth;
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sibbecaï, le Hushathite; Ilaï, Achochite;
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Maharaï, Nétophathite; Héled, fils de Baana, Nétophathite;
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Ithaï, fils de Ribaï, de Guibea, des enfants de Benjamin; Bénaja, Pirathonite;
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Huraï, de Nachalé-Gaash; Abiel, Arbathite;
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Azmaveth, Bacharumite; Éliachba, Shaalbonite;
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
Bené-Hashem, Guizonite; Jonathan, fils de Shagué, Hararite;
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Achijam, fils de Sacar, Hararite; Éliphal, fils d'Ur;
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Hépher, Mékérathite; Achija, Pélonien;
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hetsro, de Carmel; Naaraï, fils d'Ezbaï;
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Joël, frère de Nathan; Mibchar, fils d'Hagri;
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Tsélek, Ammonite; Nacharaï, Béerothite, qui portait les armes de Joab, fils de Tséruja;
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ira, Jithrite; Gareb, Jithrite;
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Urie, le Héthien; Zabad, fils d'Achlaï;
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adina, fils de Shiza, le Rubénite, chef des Rubénites, et trente avec lui;
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanan, fils de Maaca; Joshaphat, Mithnite;
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Uzzija, Ashthérathite; Shama et Jéhiel, fils de Hotham, Aroérite;
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Jédiaël, fils de Shimri; Jocha son frère, le Thitsite;
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Éliel de Machavim, Jéribaï et Joshavia, fils d'Elnaam; Jithma, Moabite;
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Éliel, Obed, et Jaasiel-Metsobaja.