< 1 Nyakati 11 >

1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
Tout Israël s'assembla auprès de David à Hébron, en disant: " Voici que nous sommes tes os et ta chair.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
Autrefois déjà, quand Saül était roi, c'était toi qui menais et ramenais Israël. Et Yahweh, ton Dieu, t'a dit: C'est toi qui paîtras mon peuple d'Israël, et c'est toi qui seras chef sur mon peuple d'Israël. "
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
Ainsi tous les anciens d'Israël vinrent auprès du roi à Hébron, et David fit alliance avec eux devant Yahweh, à Hébron; et ils oignirent David pour roi sur Israël, selon la parole de Yahweh prononcée par Samuel.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
David marcha avec tout Israël contre Jérusalem, qui est Jébus; là étaient les Jébuséens, habitants du pays.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
Les habitants de Jébus dirent à David: " Tu n'entreras pas ici. " Mais David s'empara de la forteresse de Sion: c'est la cité de David.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
David dit: " Quiconque battra le premier les Jébuséens sera chef et prince. " Joab, fils de Sarvia, monta le premier, et il devint chef.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
David s'établit dans la forteresse; c'est pourquoi on l'appela cité de David.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
Il bâtit la ville tout autour, à partir du Mello et aux environs, et Joab répara le reste de la ville.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
David devenait de plus en plus grand, et Yahweh des armées était avec lui.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
Voici les chefs des héros qui étaient au service de David, et qui, avec tout Israël, l'aidèrent pendant son règne, après avoir contribué à le faire roi, selon la parole de Yahweh au sujet d'Israël.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
Voici le nombre des héros qui étaient au service de David: Jesbaam, fils de Hachamoni, chef des Trente. Il brandit sa lance sur trois cents hommes, qu'il fit périr en une seule fois.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
Après lui, Eléazar, fils de Dodo, l'Ahohite; il était parmi les trois vaillants.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
Il était avec David à Phes-Domim, et les Philistins s'y étaient rassemblés pour combattre. Il y avait là une pièce de terre pleine d'orge, et le peuple fuyait devant les Philistins.
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
Ils se placèrent au milieu du champ, le défendirent et battirent les Philistins; et Yahweh opéra une grande délivrance.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Trois d'entre les trente capitaines descendirent auprès de David sur le rocher, à la caverne d'Odollam, tandis que le camp des Philistins était dressé dans la vallée des Réphaïm.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
David était alors dans la forteresse, et il y avait un poste de Philistins à Bethléem.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
David eut un désir, et il dit: " Qui me fera boire de l'eau de la citerne qui est à la porte de Bethléem? "
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
Aussitôt les trois hommes, passant au travers du camp des Philistins, puisèrent de l'eau de la citerne qui est à la porte de Bethléem. Ils la prirent et l'apportèrent à David; mais David ne voulut pas la boire, et il en fit une libation à Yahweh,
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
en disant: " Que mon Dieu me garde de faire cela! Boirais-je le sang de ces hommes avec leur vie? Car c'est au péril de leur vie qu'ils l'ont apportée. " Et il ne voulut pas la boire. Voilà ce que firent ces trois braves.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
Abisaï, frère de Joab, était chef des Trois; il brandit sa lance contre trois cents hommes et les tua, et il eut du renom parmi les trois.
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
Il était le plus considéré de la seconde triade, et il fut leur chef; mais il n'égala pas les trois premiers.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Banaïas, fils de Joïada, fils d'un homme vaillant et riche en exploits, de Cabséel. Il frappa les deux ariels de Moab. Il descendit et frappa le lion au milieu de la citerne un jour de neige.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
Il frappa un Egyptien d'une stature de cinq coudées; et dans la main de l'Egyptien, il y avait une lance semblable à une ensouple de tisserand. Il descendit vers lui avec un bâton, et il arracha la lance de la main de l'Egyptien et le frappa de sa propre lance.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
Voilà ce que fit Banaïas, fils de Joïada, et il eut du renom parmi les trois vaillants.
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
Voici qu'il était plus considéré que les trente, mais il n'égala pas les trois. David le fit membre de son conseil secret.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Hommes vaillants de l'armée: Asaël, frère de Joab; Elchanan, fils de Dodo, de Bethléem;
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Sammoth, d'Arori; Hellès, de Phalon;
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Hira, fils d'Accès, de Thécué; Abiéser, d'Anathot;
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sobbochaï, le Husathite; Ilaï, l'Ahohite;
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Maharaï, de Nétopha; Héled, fils de Baana, de Nétopha;
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Ethaï, fils de Ribaï, de Gabaa des fils de Benjamin; Banaïa, de Pharaton;
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Huraï, des vallées de Gaas; Abiel, d'Araba; Azmaveth, de Bauram; Eliaba, de Salabon;
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Bené-Assem, de Gézon; Jonathan, fils de Sagé, d'Arar;
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
Ahiam, fils de Sachar, d'Arar;
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Eliphal, fils d'Ur;
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Hépher, de Méchéra; Ahia, de Phélon;
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hesro, de Carmel; Naaraï fils d'Asbaï;
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Joël frère de Nathan; Mibahar, fils d'Agaraï;
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Sélec, l'Ammonite; Naharaï, de Béroth, écuyer de Joab, fils de Sarvia;
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ira, de Jéther; Gareb, de Jéther;
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Urie, le Hethéen; Zabad, fils d'Oholi;
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adina, fils de Siza le Rubénite, chef des Rubénites, et trente avec lui;
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanan, fils de Maacha; Josaphat, de Mathan;
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Ozia, d'Astaroth; Samma et Jéhiel, fils de Hotham d'Aroër;
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Jédihel, fils de Samri; Joha, son frère, le Thosaïte;
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Eliel, de Mahum; Jéribaï et Josaïa, fils d'Elnaëm; Jethma, le Moabite;
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Eliel, Obed et Jasiel, de Masobia.

< 1 Nyakati 11 >