< 1 Nyakati 11 >

1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
Then all Israel gathered themselues to Dauid vnto Hebron, saying, Beholde, we are thy bones and thy flesh.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
And in time past, euen when Saul was King, thou leddest Israel out and in: and the Lord thy God sayde vnto thee, Thou shalt feede my people Israel, and thou shalt be captaine ouer my people Israel.
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
So came all the Elders of Israel to the King to Hebron, and Dauid made a couenant with them in Hebron before the Lord. And they anoynted Dauid King ouer Israel, according to the word of the Lord by the hand of Samuel.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
And Dauid and all Israel went to Ierusalem, which is Iebus, where were the Iebusites, the inhabitants of the land.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
And the inhabitants of Iebus said to Dauid, Thou shalt not come in hither. Neuertheles Dauid tooke the towre of Zion, which is the city of Dauid.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
And Dauid sayd, Whosoeuer smiteth the Iebusites first, shalbe the chiefe and captaine. So Ioab the sonne of Zeruiah went first vp, and was captaine.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
And Dauid dwelt in the tower: therefore they called it the citie of Dauid.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
And he built the citie on euery side, from Millo euen round about, and Ioab repaired the rest of the citie.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
And Dauid prospered, and grewe: for the Lord of hostes was with him.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
These also are the chiefe of the valiant men that were with Dauid, and ioyned their force with him in his kingdome with al Israel, to make him King ouer Israel, according to the worde of the Lord.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
And this is the nomber of the valiant men whome Dauid had, Iashobeam the sonne of Hachmoni, the chiefe among thirtie: he lift vp his speare against three hundreth, whom he slewe at one time.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
And after him was Eleazar the sonne of Dodo the Ahohite, which was one of the three valiant men.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
He was with Dauid at Pas-dammim, and there the Philistims were gathered together to battel: and there was a parcell of ground full of barley, and the people fled before the Philistims.
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
And they stood in the middes of the field, and saued it, and slewe the Philistims: so the Lord gaue a great victorie.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
And three of the thirtie captaines went to a rocke to Dauid, into the caue of Adullam. And the armie of the Philistims camped in the valley of Rephaim.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
And when Dauid was in the hold, the Philistims garison was at Beth-lehem.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
And Dauid longed, and said, Oh, that one would giue me to drinke of the water of the well of Beth-lehem that is at the gate.
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
Then these three brake thorowe the hoste of the Philistims, and drewe water out of the well of Beth-lehem that was by the gate, and tooke it and brought it to Dauid: but Dauid would not drinke of it, but powred it for an oblation to the Lord,
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
And said, Let not my God suffer me to do this: should I drinke the blood of these mens liues? for they haue brought it with the ieopardie of their liues: therefore he would not drinke it: these things did these three mightie men.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
And Abishai the brother of Ioab, he was chiefe of the three, and he lift vp his speare against three hundreth, and slew them, and had the name among the three.
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
Among the three he was more honourable then the two, and he was their captaine: but he attained not vnto the first three.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Benaiah the sonne of Iehoiada (the sonne of a valiant man) which had done many actes, and was of Kabzeel, he slewe two strong men of Moab: he went downe also and slewe a lion in the middes of a pit in time of snowe.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
And he slewe an Egyptian, a man of great stature, euen fiue cubites long, and in the Egyptians hand was a speare like a weauers beame: and he went downe to him with a staffe, and plucked the speare out of the Egyptians hand, and slewe him with his owne speare.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
These things did Benaiah ye sonne of Iehoiada, and had the name among the three worthies.
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
Behold, he was honourable among thirtie, but he attained not vnto the first three. And Dauid made him of his counsell.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
These also were valiant men of warre, Asahel the brother of Ioab, Elhanan the sonne of Dodo of Beth-lehem,
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Shammoth the Harodite, Helez the Pelonite,
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Ira the sonne of Ikkesh the Tekoite, Abiezer the Antothite,
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sibbecai the Husathite, Ilai the Ahohite,
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Maharai the Netophathite, Heled ye sonne of Baanah the Netophathite,
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Ithai the sonne of Ribai of Gibeah of the children of Beniamin, Benaiah the Pirathonite,
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Hurai of the riuers of Gaash, Abiel the Arbathite,
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Azmaueth the Baharumite, Elihaba the Shaalbonite,
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
The sonnes of Hashem the Gizonite, Ionathan the sonne of Shageh the Harite,
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Ahiam the sonne of Sacar the Hararite, Eliphal the sonne of Vr,
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Hepher the Mecherathite, Ahiiah the Pelonite,
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hezro the Carmelite, Naarai the sonne of Ezbai,
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Ioel the brother of Nathan, Mibhar the sonne of Haggeri,
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Zelek the Ammonite, Nahrai the Berothite, the armour bearer of Ioab, the sonne of Zeruiah,
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ira the Ithrite, Garib the Ithrite,
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Vriah the Hittite, Zabad the sonne of Ahlai,
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adina the sonne of Shiza the Reubenite, a captaine of the Reubenites, and thirtie with him,
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanan the sonne of Maachah, and Ioshaphat the Mithnite,
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Vzia the Ashterathite, Shama and Ieiel the sonnes of Otham the Aroerite,
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Iediael the sonne of Shimri, and Ioha his brother the Tizite,
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Eliel the Mahauite, and Ieribai and Ioshauiah the sonnes of Elnaam, and Ithmah the Moabite,
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Eliel and Obed, and Iaasiel the Mesobaite.

< 1 Nyakati 11 >