< 1 Nyakati 11 >

1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
Then all Israel gathered themselves to David in Hebron, saying: We are thy bone, and thy flesh.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
Yesterday also, and the day before when Saul was king, thou wast he that leddest out and broughtest in Israel: for the Lord thy God said to thee: Thou shalt feed my people Israel, and thou shalt; be ruler over them.
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
So all the ancients of Israel came to the king to Hebron, and David made a covenant with them before the Lord: and they anointed him king over Israel, according to the word of the Lord which he spoke in the hand of Samuel.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
And David and all Israel went to Jerusalem, which is Jebus, where the Jebusites were the inhabitants of the land.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
And the inhabitants of Jebus said to David: Thou shalt not come in here. But David took the castle of Sion, which is the city of David.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
And he said: Whosoever shall first strike the Jebusites, shall be the head and chief captain. And Joab the son of Sarvia went up first, and was made the general.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
And David dwelt in the castle, and therefore it was called the city of David.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
And he built the city round about from Mello all round, and Joab built the rest of the city.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
And David went on growing and increasing, and the Lord of hosts was with him.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
These are the chief of the valiant men of David, who helped him to be made king over all Israel, according to the word of the Lord, which he spoke to Israel.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
And this is the number of the heroes of David: Jesbaam the son of Hachamoni the chief among the thirty: he lifted up his spear against three hundred wounded by him at one time.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
And after him was Eleazar his uncle’s son the Ahohite, who was one of the three mighties.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
He was with David in Phesdomim, when the Philistines were gathered to that place to battle: and the field of that country was full of barley, and the people fled from before the Philistines.
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
But these men stood in the midst of the field, and defended it: and they slew the Philistines, and the Lord gave a great deliverance to his people.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
And three of the thirty captains went down to the rock, wherein David was, to the cave of Odollam, when the Philistines encamped in the valley of Raphaim.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
And David was in a hold, and the garrison of the Philistines in Bethlehem.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
And David longed, and said: O that some man would give me water of the cistern of Bethlehem, which is in the gate.
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
And these three broke through the midst of the camp of the Philistines, and drew water out of the cistern of Bethlehem, which was in the gate, and brought it to David to drink: and he would not drink of it, but rather offered it to the Lord,
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
Saying: God forbid that I should do this in the sight of my God, and should drink the blood of these men: for with the danger of their lives they have brought me the water. And therefore he would not drink. These things did the three most valiant.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
And Abisai the brother of Joab, he was chief of three, and he lifted up his spear against three hundred whom he slew, and he was renowned among the three,
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
And illustrious among the second three, and their captain: but yet he attained not to the first three.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Banaias the son of Joiada, a most valiant man, of Cabseel, who had done many acts: he slew the two ariels of Moab: and he went down, and killed a lion in the midst of a pit in the time of snow.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
And he slew an Egyptian, whose stature was of five cubits, and who had a spear like a weaver’s beam: and he went down to him with a staff, and plucked away the spear, that he held in his hand, and slew him with his own spear.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
These things did Banaias the son of Joiada, who was renowned among the three valiant ones,
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
And the first among the thirty, but yet to the three he attained not: and David made him of his council.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Moreover the most valiant men of the army, were Asahel brother of Joab, and Elchanan the son of his uncle of Bethlehem,
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Sammoth an Arorite, Helles a Phalonite,
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Ira the son of Acces a Thecuite, Abiezer an Anathothite,
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sobbochai a Husathite, Ilai an Ahohite,
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Maharai a Netophathite, Heled the son of Baana a Netophathite,
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Ethai the son of Ribai of Gabaath of the sons of Benjamin, Banal a Pharathonite,
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Hurai of the torrent Gaas, Abiel an Arbathite, Azmoth a Bauramite, Eliaba a Salabonite,
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
The sons of Assem a, Gezonite, Jonathan the son of Sage an Ararite,
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
Ahiam the son of Sachar an Ararite,
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Eliphal the son of Ur,
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Hepher a Mecherathite, Ahia a Phelonite,
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hesro a Carmelite, Naarai the son of Azbai,
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Joel the brother of Nathan, Mibahar the son of Agarai.
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Selec an Ammonite, Naharai a Berothite, the armourbearer of Joab the son of Sarvia.
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ira a Jethrite, Gareb a Jethrite,
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Urias a Hethite, Zabad the son of Oholi,
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adina the son of Siza a Rubenite the prince of the Rubenites, and thirty with him:
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanan the son of Maacha, and Josaphat a Mathanite,
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Ozia an Astarothite, Samma, and Jehiel the sons of Hotham an Arorite,
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Jedihel the son of Zamri, and Jobs his brother a Thosaite,
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Eliel a Mithumite, and Jeribai, and Josaia the sons of Elnaim, and Jethma a Moabite,
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Eliel, and Obed, and Jasiel of Masobia.

< 1 Nyakati 11 >