< 1 Nyakati 11 >
1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
Then all of Israel was gathered to David at Hebron, saying: “We are your bone and your flesh.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
Also, yesterday and the day before, when Saul still reigned, you were the one who led out and brought in Israel. For the Lord your God said to you: ‘You shall pasture my people Israel, and you shall be the leader over them.’”
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
Therefore, all those greater by birth of Israel went to the king at Hebron. And David formed a pact with them before the Lord. And they anointed him king over Israel, in accord with the word of the Lord, which he spoke by the hand of Samuel.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
Then David and all of Israel went to Jerusalem. The same is Jebus, where the Jebusites, the inhabitants of the land, were.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
And those who were living in Jebus said to David: “You shall not enter here.” But David seized the stronghold of Zion, which is the city of David.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
And he said, “Whoever shall strike the Jebusites first, shall be ruler and commander.” And so Joab, the son of Zeruiah, ascended first, and he was made the leader.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
Then David lived in the stronghold, and for this reason it was called the City of David.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
And he built up the city all around, from Millo even to every side. But Joab built the rest of the city.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
And David continued advancing and increasing, and the Lord of hosts was with him.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
These are the leaders of the strong men of David, who assisted him, so that he would become king over all of Israel, in accord with the word of the Lord, which he spoke to Israel.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
And this is the number of the robust of David: Jashobeam, the son of a Hachmonite, leader among the thirty. He lifted up his spear over three hundred, who were wounded at one time.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
And after him, there was Eleazar, the son of his uncle, an Ahohite, who was among the three powerful ones.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
He was with David in Pasdammim, when the Philistines were gathered to that place for battle. Now the field of that region was full of barley, but the people had fled from the face of the Philistines.
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
These men stood in the midst of the field, and they defended it. And when they had struck down the Philistines, the Lord gave a great salvation to his people.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Then three from the thirty leaders descended to the rock where David was, to the cave of Adullam, when the Philistines had made camp in the Valley of the Rephaim.
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
Now David was in a stronghold, and a garrison of the Philistines was in Bethlehem.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
And then David desired and said, “O if only someone would give me water from the well of Bethlehem, which is at the gate!”
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
Therefore, these three broke through to the midst of the camp of the Philistines, and they drew water from the well of Bethlehem, which was at the gate. And they took it to David, so that he might drink. But he was not willing; and instead, he offered it as a libation to the Lord,
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
saying: “Far be it from me, that I would do this in the sight of my God, and that I would drink the blood of these men. For at the peril of their own lives, they brought the water to me.” And for this reason, he was not willing to drink. The three most powerful accomplished these things.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
Also, Abishai, the brother of Joab, was the leader of the three, and he lifted up his spear against three hundred, who were wounded. And he was most renowned among the three,
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
and he was famous among the second three and their leader. Yet truly, he did not reach as far as the first three.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Benaiah, the son of Jehoiada, from Kabzeel, was a very mature man, who had accomplished many deeds. He struck down the two lions of God from Moab. And he descended and killed a lion in the middle of a pit, in the time of snow.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
And he struck down an Egyptian man, whose stature was five cubits, and who had a spear like a weaver’s beam. And yet he descended to him with a staff. And he seized the spear that he was holding in his hand. And he killed him with his own spear.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
These things were done by Benaiah, the son of Jehoiada, who was most renowned among the three robust ones,
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
the first among the thirty. Yet truly, he did not reach as far as the three. Then David placed him beside his ear.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Moreover, the strongest men of the army were Asahel, the brother of Joab; and Elhanan, the son of his uncle, from Bethlehem;
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Shammoth, a Harorite; Helez, a Pelonite;
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Ira, the son of Ikkesh, a Tekoite; Abiezer, an Anathothite;
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sibbecai, a Hushathite; Ilai, an Ahohite;
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Maharai, a Netophathite; Heled, the son of Baanah, a Netophathite;
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Ithai, the son of Ribai, from Gibeah, of the sons of Benjamin; Benaiah, a Pirathonite;
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Hurai, from the torrent Gaash; Abiel, an Arbathite; Azmaveth, a Baharumite; Eliahba, a Shaalbonite.
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
The sons of Hashem, a Gizonite: Jonathan, the son of Shagee, a Hararite;
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
Ahiam, the son of Sachar, a Hararite;
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Eliphal, the son of Ur;
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Hepher, a Mecherathite; Ahijah, a Pelonite;
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hezro, a Carmelite; Naharai, the son of Ezbai;
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Joel, the brother of Nathan; Mibhar, the son of Hagri;
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Zelek, an Ammonite; Naarai, a Beerothite, the armor bearer of Joab, the son of Zeruiah;
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Ira, an Ithrite; Gareb, an Ithrite;
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Uriah, a Hittite; Zabad, the son of Ahlai;
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adina, the son of Shiza, a Reubenite, the leader of the Reubenites, and thirty who were with him;
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanan, the son of Maacah; and Joshaphat, a Mithnite;
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Uzzia, an Ashterathite; Shama and Jeiel, the sons of Hotham, an Aroerite;
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Jediael, the son of Shimri; and Joha, his brother, a Tizite;
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Eliel, a Mahavite; and Jeribai and Joshaviah, the sons of Elnaam; and Ithmah, a Moabite;
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Eliel, and Obed, and Jaasiel from Mezobaite.