< 1 Nyakati 10 >
1 Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika mlima Gilboa.
And the Philistines fought against Israel; and the men of Israel fled from before the Philistines, and fell down slain on mount Gilboa.
2 Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua.
And the Philistines followed hard after Saul and after his sons; and the Philistines smote Jonathan, and Abinadab, and Malchi-shua, Saul's sons.
3 Mapigano yakawa makali kumzunguka Sauli na wakati wapiga mishale walipompata, wakamjeruhi.
And the battle went sore against Saul, and the archers came up with him, and he was terrified by the archers.
4 Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
Then said Saul to his armour-bearer, Draw thy sword, and thrust me through with it; lest these uncircumcised come and abuse me. But his armour-bearer would not; for he was much afraid. So Saul took the sword and fell on it.
5 Mbeba silaha wake alipoona kwamba Sauli amekufa, naye pia akauangukia upanga wake akafa.
And when his armour-bearer saw that Saul was dead, he fell likewise on the sword, and died.
6 Kwa hiyo Sauli na wanawe watatu wakafa, pamoja na nyumba yake yote.
So Saul died, and his three sons, and all his house died together.
7 Waisraeli wote waliokuwa bondeni walipoona kwamba jeshi limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliacha miji yao wakakimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
And when all the men of Israel that were in the valley saw that they fled, and that Saul and his sons were dead, they forsook their cities and fled; and the Philistines came and dwelt in them.
8 Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe wameanguka katika Mlima Gilboa.
And it came to pass the next day, that the Philistines came to strip the slain, and they found Saul and his sons fallen on mount Gilboa.
9 Wakamvua mavazi, wakachukua kichwa chake pamoja na silaha zake, wakawatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari hizi miongoni mwa sanamu zao na watu wao.
And they stripped him, and took his head, and his armour, and sent [them] into the land of the Philistines round about, to announce the glad tidings to their idols, and to the people.
10 Waliweka silaha zake katika hekalu la miungu yao, wakatundika kichwa chake katika hekalu la Dagoni.
And they put his armour in the house of their god, and fastened his head in the house of Dagon.
11 Wakazi wote wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yote Wafilisti waliyomtendea Sauli,
And when all they of Jabesh-Gilead heard of all that the Philistines had done to Saul,
12 mashujaa wao wote wakaondoka, wakautwaa mwili wa Sauli na miili ya wanawe, wakaileta Yabeshi. Wakaizika mifupa yao chini ya mti mkubwa huko Yabeshi, nao wakafunga kwa siku saba.
all the valiant men arose, and took up the body of Saul and the bodies of his sons, and brought them to Jabesh, and buried their bones under the terebinth of Jabesh, and fasted seven days.
13 Sauli alikufa kwa sababu hakuwa mwaminifu kwa Bwana. Hakulishika neno la Bwana, hata akataka shauri kwa mwaguzi kwa ajili ya uongozi,
And Saul died for his unfaithfulness which he committed against Jehovah, because of the word of Jehovah which he kept not, and also for having inquired of the spirit of Python, asking counsel of it;
14 hakumuuliza Bwana. Kwa hiyo Bwana alimuua, na ufalme akampa Daudi mwana wa Yese.
and he asked not counsel of Jehovah; therefore he slew him, and transferred the kingdom to David the son of Jesse.