< Romanos 3 >

1 ¿Qué ventaja tiene el ser judío? o ¿qué beneficio hay en la circuncisión?
Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
2 Mucho, todos los sentidos: primero porque se les confió la palabra de Dios.
Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
3 Y si algunos no tienen fe, ¿eso hará que la fidelidad de Dios no tenga efecto?
Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
4 De ninguna manera: pero que Dios sea veraz, y todo hombre mentiroso; como se dice en las Escrituras, para que seas justificado en tus palabras, y saldrás vencedor cuando seas juzgado.
La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
5 Pero si nuestra injusticia magnífica la justicia de Dios, ¿qué diremos? ¿Dios es injusto porque nos castiga? (Hablo como hombre)?
Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
6 De ninguna manera: porque si es así, ¿cómo juzgaría Dios al mundo?
La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
7 Pero si, mi mentira sirve para que la verdad de Dios resulte aún más gloriosa, ¿por qué soy juzgado como un pecador?
Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
8 y porque no decir? hagamos mal para que venga el bien (una calumnia que dicen algunos, que yo enseño), pero tales personas su condenación es justa.
Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
9 ¿Entonces qué? los judíos somoss mejores que ellos? De ninguna manera: porque antes hemos dejado en claro que tanto los judíos como los gentiles están bajo el poder del pecado;
Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
10 Como está dicho en las Sagradas Escrituras: no hay justo ni uno solo;
Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
11 No hay quien entienda, no uno que busque a Dios;
Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
12 Todos se han apartado, todos se hicieron inútiles; no hay quien haga el bien, ni siquiera uno:
Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
13 Su garganta es como un sepulcro abierto; con sus lenguas han dicho lo que no es cierto: el veneno de las serpientes está bajo sus labios:
“Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
14 Cuya boca está llena de maldiciones y palabras amargas:
“Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
15 Sus pies corren rápidamente para derramar sangre;
“Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
16 La destrucción y miseria hay en sus caminos;
maangamizi na taabu viko katika njia zao,
17 Y del camino de la paz no tienen conocimiento:
wala njia ya amani hawaijui.”
18 No hay temor de Dios delante de sus ojos.
“Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
19 Ahora bien, sabemos que lo que la ley dice, es para los que están bajo la ley, para que toda boca se cierre y todos los hombres sean juzgados por Dios.
Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
20 Porque por las obras de la ley ningún hombre puede ser justificado, porque a través de la ley viene el conocimiento del pecado.
Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
21 Pero ahora, sin la ley, hay una revelación de la justicia de Dios, a la cual la ley y los profetas dan testimonio;
Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
22 Es decir, la justicia de Dios por medio de la fe en Jesucristo, para todos los que tienen fe en él; porque no hay diferencia entre judío y gentil,
Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
23 porque todos han pecado y están destituidos de la gloria de Dios;
kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
24 siendo justificados gratuitamente, por su gracia, por la salvación que es en Cristo Jesús:
wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
25 Dios hizo que Cristo al derramar su sangre, fuera el instrumento del perdón. Este perdón se alcanza por la fe y demuestra que Dios es justo, y que, si pasó por alto los pecados de otro tiempo.
Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
26 fue solo a causa de su paciencia Y para demostrar su justicia en este tiempo, para que él mismo sea él justo, y él que justifica al que tiene fe en Jesús.
Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
27 ¿Qué razón, entonces, hay para el orgullo del hombre ante Dios? Está eliminado. ¿Por qué tipo de ley? de obras? No, sino por una ley de fe.
Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
28 Por esta razón, entonces, el hombre es justificado por fe sin las obras de la ley.
Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
29 ¿O es Dios el Dios de los Judíos solamente? ¿No es él de la misma manera el Dios de los gentiles? Sí, de gentiles:
Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
30 Si Dios es uno; y él justificará por la fe a los de circuncisión, y por la fe a los que no tienen la circuncisión.
Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
31 Entonces, ¿por medio de la fe, la ley no tiene efecto? de ninguna manera: más bien confirmamos el valor de la ley.
Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.

< Romanos 3 >