< Salmos 88 >
1 Oh Señor, Dios de mi salvación, te pido auxilio día y noche.
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 Permite que mi oración venga delante de ti; escucha mi clamor.
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 Porque mi alma está llena de males, y mi vida se ha acercado al inframundo. (Sheol )
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol )
4 Soy contado entre los que descienden al sepulcro; Me he vuelto como un hombre sin fuerzas:
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 Mi alma está entre los muertos, como en el infierno, a la que no le das más vueltas; porque están separados de tu cuidado. ()
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 Me has puesto en las profundidades más bajas, incluso en lugares oscuros.
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 El peso de tu ira me aplasta, todas tus olas me han vencido. (Selah)
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 Has enviado a mis amigos lejos de mí; me has hecho una cosa repugnante en sus ojos: estoy encerrado y no puedo salir.
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 Mis ojos se están consumiendo a causa de mi problema: Señor, mi llanto ha subido a ti todos los días, mis manos están extendidas hacia ti.
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 ¿Harás obras de maravilla por los muertos? volverán los muertos para darte el elogio? (Selah)
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 ¿Se dará la historia de tu misericordia en la casa de los muertos? ¿Las noticias de tu fe llegarán al lugar de la destrucción?
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 ¿Puede haber conocimiento de tus maravillas en la oscuridad? o de tu justicia en la tierra del olvido?
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 Pero a ti envié mi clamor, oh Señor; por la mañana mi oración vino ante ti.
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 Señor, ¿por qué desechas mi alma? ¿Por qué escondes de mí tu cara?
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 He estado angustiado y temeroso de la muerte desde que era joven; tu ira es dura conmigo, y no tengo fuerzas.
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 El ardor de tu ira me ha sobrepasado; Estoy roto, me ha vencido.
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 Me rodean todo el día como agua; han hecho un círculo sobre mí.
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 Has enviado a mis amigos y al compañero lejos de mí; Me he ido de la memoria de aquellos que son queridos por mí.
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.