< Salmos 78 >
1 Escucha, oh mi pueblo, a mi ley; deja que tus oídos se inclinen a las palabras de mi boca.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Abriendo mi boca voy a dar una historia, incluso los dichos oscuros de los viejos tiempos;
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 Que han venido a nuestro oído y a nuestro conocimiento, tal como nos fueron dados por nuestros padres.
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 No los mantendremos en secreto de nuestros hijos; aclararemos a la generación venidera las alabanzas del Señor y su fortaleza, y las grandes obras de asombro que ha hecho.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 Puso un testigo en Jacob, e hizo una ley en Israel; que él dio a nuestros padres para que pudieran darles conocimiento de ellos a sus hijos;
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 Para que la generación venidera pueda tener conocimiento de ellos, incluso de los hijos del futuro, que les den a conocer a sus hijos;
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 Para que pongan su esperanza en Dios, y no dejen que las obras de Dios se salgan de sus mentes, sino que guarden sus leyes;
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 y no sean como sus padres, una generación dura e incontrolada; una generación cuyo corazón era duro, cuyo espíritu no era fiel a Dios.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 Los hijos de Efraín, armados con arcos, volvieron las espaldas en el día de la pelea.
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 No fueron gobernados por la palabra de Dios, y no quisieron ir en el camino de su ley;
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 Dejaron sus obras fuera de su memoria, y las maravillas que les había hecho ver.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Hizo grandes obras delante de sus padres, en la tierra de Egipto, en los campos de Zoán.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 El mar fue cortado en dos para que pudieran pasar; las aguas se juntaron de lado a lado.
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 Durante el día los guiaba en la nube, y durante toda la noche con una luz de fuego.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 Las rocas del desierto fueron quebradas por su poder, y él les dio a beber como de las aguas profundas.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Hizo salir arroyos de la peña; y las aguas descender como ríos.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 Y siguieron pecando contra él aún más, apartándose del Altísimo en el desierto;
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 Probando a Dios en sus corazones, pidiendo carne por su deseo.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 Dijeron palabras crueles contra Dios, diciendo: ¿Puede Dios preparar una mesa en el desierto?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Mira, la roca fue cortada por su poder, por lo que el agua salió corriendo, y arroyos desbordantes; ¿él puede darnos pan? ¿es capaz de obtener carne para su gente?
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Así que estas cosas vinieron a oídos del Señor, y él se enojó; y se encendió un fuego contra Jacob, y vino la ira contra Israel;
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 Porque no tenían fe en Dios, ni esperanza en su salvación.
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Y dio órdenes a las nubes en lo alto, y las puertas del cielo estaban abiertas;
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 Y envió como lluvia de maná, y les dio el grano del cielo.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 El hombre tomó parte en el alimento de los ángeles; les envió carne en toda su medida.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 Envió un viento del este del cielo, impulsando el viento del sur con su poder.
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 Envió carne sobre ellos como el polvo, y aves emplumadas como la arena del mar,
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Y él dejó que baje a su lugar de descanso, alrededor de sus tiendas.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 Así que tenían comida y estaban llenos; porque él les dio su deseo;
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Pero no se apartaron de sus deseos; y mientras la comida todavía estaba en sus bocas,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 Vino sobre ellos la ira de Dios, y mató a los más robustos, y acabó con los jóvenes de Israel.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 Por todo esto siguieron pecando aún más, y no tuvieron fe en sus grandes maravillas.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Así que sus días fueron desperdiciados como un aliento, y sus años en problemas.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Cuando les mandó la muerte, lo buscaron; entonces se volvían a él buscándolo con cuidado;
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 Entonces se acordaban que Dios era su Roca, y el Dios Altísimo su salvador.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Pero sus labios y lengua le eran falsos;
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 Y sus corazones no estaban bien con él, y no guardaron su pacto con él.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 Pero él, lleno de piedad, tiene perdón por el pecado, y no pone fin al hombre: frecuentemente retracta su ira, y no se enoja violentamente.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Así que tuvo en cuenta que ellos eran solo carne; un aliento que se va rápidamente, y no volverá.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 ¡Con qué frecuencia iban contra él en el desierto. y le daban motivo de aflicción en el desierto!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Otra vez pusieron a Dios a prueba, y le dieron dolor al Santo de Israel.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 No tuvieron en cuenta el trabajo de su mano, ni el día en que los quitó del poder de sus enemigos;
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 cómo hizo sus señales en Egipto, y sus maravillas en el campo de Zoán;
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 De modo que sus ríos se convirtieron en sangre, y no pudieron beber de sus arroyos.
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 Envió diferentes tipos de moscas entre ellos, envenenando su carne; y ranas para su destrucción.
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 El dio el aumento de sus campos a los gusanos, los frutos de su industria a los saltamontes.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 Envió hielo para la destrucción de sus vides; sus árboles fueron dañados por el frío glacial.
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 Hielo fue llovido sobre su ganado; tormentas eléctricas enviaron destrucción entre las bandadas.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 Envió sobre ellos el ardor de su ira, su amargo disgusto, y liberó ángeles malvados entre ellos.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 Dejó que su ira se saliera con la suya; él no retuvo su alma de la muerte, sino que dio su vida a la enfermedad.
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 Él dio a la destrucción a todos los primeros hijos de Egipto; los primeros frutos de su fuerza en las tiendas de Cam;
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 Pero él tomó a su pueblo como ovejas, y los guió en la tierra desolada como un rebaño.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Los llevó a salvo para que no tuvieran miedo; pero sus enemigos estaban cubiertos por el mar.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 Y él fue su guía a su tierra santa, hasta el monte que su diestra había hecho suyo;
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Expulsando naciones delante de ellos, marcando la línea de su herencia, y dando a las personas de Israel sus tiendas para un lugar de descanso.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Pero ellos se amargaron contra el Dios Altísimo, lo probaron y no guardaron sus leyes;
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Sus corazones se volvieron atrás y falsos como sus padres; fueron convertidos a un lado como un arco retorcido.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 Le enojaron con sus altares paganos; adorando ídolos, lo provocaron a celos.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Cuando esto llegó a oídos de Dios, se enojó mucho y abandonó a Israel por completo;
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 Y se fué del lugar santo en Silo, la tienda que había puesto entre los hombres;
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 Y permitió que sus enemigos capturaran él símbolo de su poder y gloria.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 Él entregó a su pueblo a la espada, y se enojó con su pueblo.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Sus jóvenes fueron quemados en el fuego; y sus vírgenes no fueron alabadas en la canción de la novia.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Sus sacerdotes fueron muertos a espada, y sus viudas no lloraron por ellos.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Entonces el Señor era como el que se despierta del sueño, y como un hombre fuerte que clama por el vino.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 Sus enemigos fueron rechazados por sus golpes y avergonzados para siempre.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Y puso la tienda de José a un lado, y no tomó la tribu de Efraín;
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 Pero él tomó la tribu de Judá para sí, y el monte de Sión, en el cual tuvo placer.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 E hizo su lugar santo como el alto cielo, como la tierra que él fija para siempre.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 Tomó a David para que fuera su siervo, y lo llevó del lugar de las ovejas;
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 De cuidar las ovejas que daban leche, lo llevó a dar de comer a Jacob su pueblo, y a Israel su heredad.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 Y David cuido del pueblo de Dios. Los cuido y dirigió con mano hábil y corazón sincero.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.