< Salmos 78 >
1 Escucha, oh mi pueblo, a mi ley; deja que tus oídos se inclinen a las palabras de mi boca.
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Abriendo mi boca voy a dar una historia, incluso los dichos oscuros de los viejos tiempos;
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 Que han venido a nuestro oído y a nuestro conocimiento, tal como nos fueron dados por nuestros padres.
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 No los mantendremos en secreto de nuestros hijos; aclararemos a la generación venidera las alabanzas del Señor y su fortaleza, y las grandes obras de asombro que ha hecho.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 Puso un testigo en Jacob, e hizo una ley en Israel; que él dio a nuestros padres para que pudieran darles conocimiento de ellos a sus hijos;
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 Para que la generación venidera pueda tener conocimiento de ellos, incluso de los hijos del futuro, que les den a conocer a sus hijos;
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 Para que pongan su esperanza en Dios, y no dejen que las obras de Dios se salgan de sus mentes, sino que guarden sus leyes;
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 y no sean como sus padres, una generación dura e incontrolada; una generación cuyo corazón era duro, cuyo espíritu no era fiel a Dios.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 Los hijos de Efraín, armados con arcos, volvieron las espaldas en el día de la pelea.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 No fueron gobernados por la palabra de Dios, y no quisieron ir en el camino de su ley;
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 Dejaron sus obras fuera de su memoria, y las maravillas que les había hecho ver.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Hizo grandes obras delante de sus padres, en la tierra de Egipto, en los campos de Zoán.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 El mar fue cortado en dos para que pudieran pasar; las aguas se juntaron de lado a lado.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 Durante el día los guiaba en la nube, y durante toda la noche con una luz de fuego.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 Las rocas del desierto fueron quebradas por su poder, y él les dio a beber como de las aguas profundas.
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 Hizo salir arroyos de la peña; y las aguas descender como ríos.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Y siguieron pecando contra él aún más, apartándose del Altísimo en el desierto;
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 Probando a Dios en sus corazones, pidiendo carne por su deseo.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 Dijeron palabras crueles contra Dios, diciendo: ¿Puede Dios preparar una mesa en el desierto?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Mira, la roca fue cortada por su poder, por lo que el agua salió corriendo, y arroyos desbordantes; ¿él puede darnos pan? ¿es capaz de obtener carne para su gente?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Así que estas cosas vinieron a oídos del Señor, y él se enojó; y se encendió un fuego contra Jacob, y vino la ira contra Israel;
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 Porque no tenían fe en Dios, ni esperanza en su salvación.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 Y dio órdenes a las nubes en lo alto, y las puertas del cielo estaban abiertas;
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 Y envió como lluvia de maná, y les dio el grano del cielo.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 El hombre tomó parte en el alimento de los ángeles; les envió carne en toda su medida.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 Envió un viento del este del cielo, impulsando el viento del sur con su poder.
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 Envió carne sobre ellos como el polvo, y aves emplumadas como la arena del mar,
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 Y él dejó que baje a su lugar de descanso, alrededor de sus tiendas.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 Así que tenían comida y estaban llenos; porque él les dio su deseo;
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 Pero no se apartaron de sus deseos; y mientras la comida todavía estaba en sus bocas,
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 Vino sobre ellos la ira de Dios, y mató a los más robustos, y acabó con los jóvenes de Israel.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 Por todo esto siguieron pecando aún más, y no tuvieron fe en sus grandes maravillas.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 Así que sus días fueron desperdiciados como un aliento, y sus años en problemas.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 Cuando les mandó la muerte, lo buscaron; entonces se volvían a él buscándolo con cuidado;
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 Entonces se acordaban que Dios era su Roca, y el Dios Altísimo su salvador.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 Pero sus labios y lengua le eran falsos;
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 Y sus corazones no estaban bien con él, y no guardaron su pacto con él.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Pero él, lleno de piedad, tiene perdón por el pecado, y no pone fin al hombre: frecuentemente retracta su ira, y no se enoja violentamente.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 Así que tuvo en cuenta que ellos eran solo carne; un aliento que se va rápidamente, y no volverá.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 ¡Con qué frecuencia iban contra él en el desierto. y le daban motivo de aflicción en el desierto!
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 Otra vez pusieron a Dios a prueba, y le dieron dolor al Santo de Israel.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 No tuvieron en cuenta el trabajo de su mano, ni el día en que los quitó del poder de sus enemigos;
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 cómo hizo sus señales en Egipto, y sus maravillas en el campo de Zoán;
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 De modo que sus ríos se convirtieron en sangre, y no pudieron beber de sus arroyos.
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 Envió diferentes tipos de moscas entre ellos, envenenando su carne; y ranas para su destrucción.
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 El dio el aumento de sus campos a los gusanos, los frutos de su industria a los saltamontes.
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 Envió hielo para la destrucción de sus vides; sus árboles fueron dañados por el frío glacial.
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 Hielo fue llovido sobre su ganado; tormentas eléctricas enviaron destrucción entre las bandadas.
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 Envió sobre ellos el ardor de su ira, su amargo disgusto, y liberó ángeles malvados entre ellos.
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 Dejó que su ira se saliera con la suya; él no retuvo su alma de la muerte, sino que dio su vida a la enfermedad.
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 Él dio a la destrucción a todos los primeros hijos de Egipto; los primeros frutos de su fuerza en las tiendas de Cam;
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 Pero él tomó a su pueblo como ovejas, y los guió en la tierra desolada como un rebaño.
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 Los llevó a salvo para que no tuvieran miedo; pero sus enemigos estaban cubiertos por el mar.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 Y él fue su guía a su tierra santa, hasta el monte que su diestra había hecho suyo;
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 Expulsando naciones delante de ellos, marcando la línea de su herencia, y dando a las personas de Israel sus tiendas para un lugar de descanso.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 Pero ellos se amargaron contra el Dios Altísimo, lo probaron y no guardaron sus leyes;
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 Sus corazones se volvieron atrás y falsos como sus padres; fueron convertidos a un lado como un arco retorcido.
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 Le enojaron con sus altares paganos; adorando ídolos, lo provocaron a celos.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 Cuando esto llegó a oídos de Dios, se enojó mucho y abandonó a Israel por completo;
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 Y se fué del lugar santo en Silo, la tienda que había puesto entre los hombres;
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 Y permitió que sus enemigos capturaran él símbolo de su poder y gloria.
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 Él entregó a su pueblo a la espada, y se enojó con su pueblo.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 Sus jóvenes fueron quemados en el fuego; y sus vírgenes no fueron alabadas en la canción de la novia.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Sus sacerdotes fueron muertos a espada, y sus viudas no lloraron por ellos.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 Entonces el Señor era como el que se despierta del sueño, y como un hombre fuerte que clama por el vino.
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 Sus enemigos fueron rechazados por sus golpes y avergonzados para siempre.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 Y puso la tienda de José a un lado, y no tomó la tribu de Efraín;
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 Pero él tomó la tribu de Judá para sí, y el monte de Sión, en el cual tuvo placer.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 E hizo su lugar santo como el alto cielo, como la tierra que él fija para siempre.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 Tomó a David para que fuera su siervo, y lo llevó del lugar de las ovejas;
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 De cuidar las ovejas que daban leche, lo llevó a dar de comer a Jacob su pueblo, y a Israel su heredad.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 Y David cuido del pueblo de Dios. Los cuido y dirigió con mano hábil y corazón sincero.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.