< Salmos 63 >
1 Oh Dios, tú eres mi Dios; de madrugada te buscaré: mi alma está seca por necesidad de ti, mi carne se desperdicia con deseo por ti, como una tierra seca y ardiente donde no hay agua;
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 Para ver tu poder y tu gloria, como te he visto en el lugar santo.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Porque tu misericordia es mejor que la vida, mis labios te darán alabanza.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Así que continuaré bendiciéndote toda mi vida, levantando mis manos en tu nombre.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 Mi alma será consolada, como con buena comida; y mi boca te dará alabanza con canciones de alegría;
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 Cuando el recuerdo de ti viene a mí en mi cama, y cuando pienso en ti por la noche.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Porque has sido mi ayuda, tendré gozo a la sombra de tus alas.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 Mi alma se mantiene siempre cerca de ti: tu diestra es mi apoyo.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 Pero aquellos cuyo deseo es la destrucción de mi alma bajará a las partes más bajas de la tierra.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 Serán cortados por la espada; serán alimento para zorros.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Pero el rey tendrá gozo en Dios; todos los que juran por él tendrán motivos de orgullo; pero la boca falsa se detendrá.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.