< Salmos 26 >

1 Oh Señor, sé mi juez, porque mi comportamiento ha sido recto: he puesto mi fe en el Señor sin titubear.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 Ponme en la balanza, oh Señor, para que yo sea probado; examina y pon a prueba mis pensamientos y mi corazón.
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 Porque tu misericordia está delante de mis ojos; y te he sido fiel.
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 No me he sentado con personas mentirosas, y no voy con hombres hipócritas.
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 He sido aborrecedor de la banda de malhechores, y no me senté entre pecadores.
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 Haré que mis manos estén limpias del pecado; así iré alrededor de tu altar, oh Señor;
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 Para dar la voz de alabanza y acción de gracias. y hacer públicas todas las maravillas que has hecho.
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 Señor, tu casa me ha sido querida y el lugar de descanso de tu gloria.
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 No se cuente mi alma entre los pecadores, ni mi vida entre los sanguinarios;
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 En cuyas manos hay malos designios, y cuyas diestras toman dinero para sobornar.
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 ¡Pero en cuanto a mí, seguiré mis caminos rectos: sé mi salvador, y ten misericordia de mí!
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 ¡Mi pie ha estado en rectitud; Alabaré al Señor en las reuniones de su pueblo!
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.

< Salmos 26 >