< Salmos 113 >

1 Deje que el Señor sea alabado. Oh siervos del Señor, alaben el nombre del Señor.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Sea bendito el nombre del Señor, desde este momento y para siempre.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 Desde la llegada del sol hasta su descenso, el nombre del Señor debe ser alabado.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 El Señor es alto sobre todas las naciones, y su gloria es más alta que los cielos.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 ¿Quién como Jehová nuestro Dios, que está sentado en lo alto?
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 Mirando hacia abajo en los cielos, y en la tierra?
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 Él toma al hombre pobre del polvo, levantándolo de su posición baja;
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 Para darle un lugar entre los gobernantes, con los gobernantes de su pueblo.
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Él le da a la mujer no fértil una familia, convirtiéndola en una madre feliz de hijos. Alaba al Señor.
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Salmos 113 >