< Proverbios 27 >
1 No presumas sobre el mañana, ya que no estás seguro de cuál será el resultado de hoy.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Deja que otro hombre te alabe, y no tu boca; alguien que es extraño para ti, y no tus labios.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 Una piedra tiene un gran peso, y la arena es aplastante; pero la ira de los tontos es de mayor peso que estos.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 La ira es cruel y la sensación de enojo es una corriente desbordante; pero, ¿quién no cede ante la envidia?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Mejor es la protesta abierta que el amor mantenido en secreto.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Las heridas de un amigo se dan de buena fe, pero los besos de un enemigo son falsos.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 El hombre completo no tiene utilidad para la miel, pero para el hombre que necesita alimento, todo lo amargo es dulce.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 Como un pájaro que vaga desde el lugar de sus huevos, es hombre que vagabundea del lugar donde nació.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 El aceite y el perfume alegran el corazón, y la sabia sugerencia de un amigo es dulce para el alma.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 No renuncies a tu amigo y al amigo de tu padre; y no vayas a la casa de tu hermano en el día de tu problema: es mejor que un vecino esté cerca que un hermano que esté lejos.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 Hijo mío, sé sabio y haz que mi corazón se alegre, así podré dar una respuesta al que me avergüenza.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 El hombre prudente ve el mal y se refugia: los simples van directos y se meten en problemas.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Toma como prenda la ropa de un hombre si él se hace fiador de un hombre extraño, y haz una promesa de él que da su palabra para los hombres extraños.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 El que da la bendición a su amigo a gran voz, levantándose temprano en la mañana, lo pondrá en su cuenta como una maldición.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 Como una caída interminable en un día de lluvia es una mujer de lengua amargada.
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 El que mantiene en secreto el secreto de su amigo, obtendrá un nombre para la buena fe.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 El hierro afila el hierro; entonces un hombre afila a otro hombre.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 El que guarda una higuera tendrá su fruto; y el sirviente que espera a su amo será honrado.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Como el rostro que mira la cara en el agua, así son los corazones de los hombres unos con los otros.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 El inframundo y Abaddón nunca están llenos, y los ojos del hombre nunca tienen suficiente. (Sheol )
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol )
21 La olla de calefacción es para la plata y el horno de fuego para él oro, y un hombre se mide por lo que es alabado.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Aunque un hombre insensato sea aplastado con un martillo en una vasija de grano molido, aún así no se apartará de él su insensatez.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Ten conocimiento sobre la condición de tus ovejas, cuidando mucho de tus rebaños;
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 Porque la riqueza no es para siempre, y el dinero no dura para todas las generaciones.
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 Aparece el pasto y se ve la hierba joven, y entran las plantas de la montaña.
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 Los corderos son para tu ropa, y los machos cabríos dan el valor de un campo:
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 Habrá leche de cabra suficiente para tu alimento, y para el sostén de tus siervas.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.