< Filipenses 1 >
1 Pablo y Timoteo, siervos de Jesucristo, a todos los santos en Cristo Jesús en Filipos, con los Obispos y Diáconos de la iglesia:
Waraka wa Paulo na Timotheo, watumishi wa Kristo Yesu: Kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu walioko Filipi, pamoja na waangalizi na mashemasi:
2 Gracia y paz a ustedes de parte de Dios nuestro Padre y del Señor Jesucristo.
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
3 Doy gracias a mi Dios en cada recuerdo tuyo,
Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.
4 Y en todas mis oraciones por todos ustedes, haciendo mis súplicas con alegría,
Katika maombi yangu yote daima nimekuwa nikiwaombea ninyi nyote kwa furaha,
5 Por su ayuda en dar las buenas nuevas desde el primer día hasta ahora;
kwa sababu ya kushiriki kwenu katika kueneza Injili, tangu siku ya kwanza hadi leo.
6 Porque estoy seguro de esto mismo, de que aquel por quien la buena obra comenzó en ustedes lo completará hasta el día de Jesucristo:
Nina hakika kwamba yeye aliyeianza kazi njema mioyoni mwenu, ataiendeleza na kuikamilisha hata siku ya Kristo Yesu.
7 Así que es correcto para mí pensar en todos ustedes de esta manera, porque Te llevo en mi corazón; como en mis cadenas, y en mis argumentos ante los jueces en apoyo de las buenas nuevas, dejando en claro que es verdad, todos ustedes tienen su parte conmigo en la gracia.
Ni haki na ni wajibu wangu kufikiri hivi juu yenu nyote, kwa sababu ninyi mko moyoni mwangu. Ikiwa nimefungwa au nikiwa ninaitetea na kuithibitisha Injili, ninyi nyote mnashiriki neema ya Mungu pamoja nami.
8 Porque Dios es mi testigo, como mi amor se extiende a todos ustedes en las amorosas misericordias de Cristo Jesús.
Mungu ni shahidi wangu jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote kwa huruma ya Kristo Yesu.
9 Y mi oración es que puedan aumentar cada vez más en conocimiento y discernimiento;
Haya ndiyo maombi yangu: kwamba upendo wenu uongezeke zaidi na zaidi katika maarifa na ufahamu wote,
10 Para que puedas dar tu aprobación a las mejores cosas; para que seas verdadero y sin malas acciones hasta el día de Cristo;
ili mpate kutambua yale yaliyo mema, mkawe safi, wasio na hatia hadi siku ya Kristo,
11 Estar llenos de los frutos de la justicia, que son por medio de Jesucristo, para la gloria y la alabanza de Dios.
mkiwa mmejawa na matunda ya haki yapatikanayo kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa za Mungu.
12 Ahora mi propósito es aclararles, hermanos, que la causa de la predicación del mensaje de salvación ha sido ayudada por mis experiencias;
Basi, ndugu zangu, nataka mjue kwamba mambo yale yaliyonipata kwa kweli yamesaidia sana kueneza Injili.
13 De modo que quedó claro a través de todo el Pretorio y de todos los demás, que estoy preso por causa de Cristo;
Matokeo yake ni kwamba imejulikana wazi kwa walinzi wote wa jumba la kifalme na kwa wengine wote kuwa nimefungwa kwa ajili ya Kristo.
14 Y la mayoría de los hermanos en el Señor, tomando ánimo a causa de mis cadenas, son todos más fuertes para dar la palabra de Dios sin temor.
Kwa sababu ya vifungo vyangu, ndugu wengi katika Bwana wametiwa moyo kuhubiri neno la Mungu kwa ujasiri zaidi na bila woga.
15 Aunque algunos están predicando a Cristo por envidia y competencia, otros lo hacen con buen corazón:
Ni kweli kwamba wengine wanamhubiri Kristo kutokana na wivu na kwa kutaka kushindana, lakini wengine wanamhubiri Kristo kwa nia njema.
16 Pero aquellos están predicando a Cristo en espíritu de competencia, no de sus corazones, pero con el propósito de darme dolor en mi prisión.
Hawa wa mwisho wanamhubiri Kristo kwa moyo wa upendo, wakifahamu kwamba nimo humu gerezani kwa ajili ya kuitetea Injili.
17 Pero los otros por amor, sabiendo que estoy dispuesto para la defensa del evangelio.
Hao wa kwanza wanamtangaza Kristo kutokana na tamaa zao wenyewe wala si kwa moyo mweupe, bali wanakusudia kuongeza mateso yangu katika huku kufungwa kwangu.
18 ¿Entonces qué? solo que en todos los sentidos, falsa o verdaderamente, la predicación de Cristo continúa; y en esto estoy contento, y me alegraré.
Lakini inadhuru nini? Jambo la muhimu ni kwamba kwa kila njia, ikiwa ni kwa nia mbaya au njema, Kristo anahubiriwa. Nami kwa ajili ya jambo hilo ninafurahi. Naam, nami nitaendelea kufurahi,
19 Porque soy consciente de que esto será para mi salvación, mediante su oración y la entrega de las riquezas almacenadas del Espíritu de Jesucristo,
kwa maana ninajua kwamba kwa maombi yenu na kwa msaada unaotolewa na Roho wa Yesu Kristo, yale yaliyonipata mimi yatageuka kuwa wokovu wangu.
20 En la medida de mi gran esperanza y creencia de que en nada seré avergonzado, pero que sin temor, como en todo momento, ahora Cristo tendrá gloria en mi cuerpo, ya sea por la vida o por la muerte.
Ninatarajia kwa shauku kubwa na kutumaini kwamba sitaaibika kwa njia yoyote, bali nitakuwa na ujasiri wa kutosha ili sasa kama wakati mwingine wowote, Kristo atukuzwe katika mwili wangu, ikiwa ni kwa kuishi au kwa kufa.
21 Porque para mí la vida es Cristo y la muerte es ganancia.
Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
22 Pero si sigo viviendo en la carne, si este es el fruto de mi trabajo, entonces no veo qué decisión tomar.
Kama nitaendelea kuishi katika mwili, kwangu hili ni kwa ajili ya matunda ya kazi. Lakini sijui nichague lipi? Mimi sijui!
23 Estoy en una posición difícil entre los dos, tengo un deseo de irme y estar con Cristo, lo cual es mucho mejor:
Ninavutwa kati ya mambo mawili: Ninatamani kuondoka nikakae pamoja na Kristo, jambo hilo ni bora zaidi.
24 Sin embargo, continuar en la carne es más necesario debido a ustedes.
Lakini kwa sababu yenu ni muhimu zaidi mimi nikiendelea kuishi katika mwili.
25 Y estando seguro de esto, soy consciente de que continuaré, sí, y continuaré con todos ustedes, para su crecimiento y gozo en la fe;
Kwa kuwa nina matumaini haya, ninajua kwamba nitaendelea kuwepo na kuwa pamoja nanyi nyote, ili mpate kukua na kuwa na furaha katika imani.
26 Para que su orgullo en mí aumente en Cristo Jesús al estar presente ustedes otra vez.
Ili kwamba furaha yenu iwe nyingi katika Kristo Yesu kwa ajili yangu kwa kule kuja kwangu kwenu tena.
27 Solo deja que su comportamiento haga honor a las buenas nuevas de Cristo, de modo que si voy a verlos y si estoy lejos de ustedes, puedo tener noticias de ustedes de que son fuertes en un espíritu, trabajando junto con una sola alma para la fe de las buenas nuevas;
Lakini lolote litakalotukia, mwenende kama ipasavyo Injili ya Kristo, ili kwamba nikija na kuwaona au ikiwa sipo, nipate kusikia haya juu yenu: Kuwa mnasimama imara katika roho moja, mkiishindania imani ya Injili kwa umoja,
28 No teniendo miedo de los que están contra ustedes lo cual es una clara señal de su destrucción, pero de su salvación, y esto de Dios;
wala msitishwe na wale wanaowapinga. Hii ni ishara kwao kuwa wataangamia, lakini ninyi mtaokolewa, na hii ni kazi ya Mungu.
29 Porque a ustedes se les ha dado por la causa de Cristo no solo tener fe en él, sino sufrir dolor por su cuenta:
Kwa maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, bali pia kuteswa kwa ajili yake,
30 Peleando la misma batalla que viste en mí, y ahora tienen noticia que sigo luchando.
kwa kuwa mnashiriki mashindano yale yale mliyoyaona nikiwa nayo na ambayo hata sasa mnasikia kuwa bado ninayo.