< Números 8 >
1 Y él Señor dijo a Moisés:
Bwana akamwambia Mose,
2 Dile a Aarón, Cuando ponga las luces en sus lugares, las siete luces darán luz delante del candelabro.
“Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
3 Y Aarón lo hizo; puso las luces en sus lugares para que dieran luz delante del candelabro, como el Señor le dio órdenes a Moisés.
Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
4 El candelabro para las luces era labrado de oro martillado, desde su base hasta sus flores fue labrado a martillo; a partir del diseño que el Señor le había dado a Moisés, él hizo el apoyo para las luces.
Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
5 Y él Señor dijo a Moisés:
Bwana akamwambia Mose:
6 Saca a los levitas de entre los hijos de Israel y purifícalos.
“Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
7 Y así es como debes purificarlos: deja que el agua sagrada que quita el pecado sea puesta sobre ellos, y deja que el pelo de todo su cuerpo se corte con una cuchilla afilada, y deja que sus ropas se laven y así quedarán puros.
Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
8 Luego, que tomen un becerro su ofrenda de harina, el grano triturado mezclado con aceite, y tomen otro becerro para una ofrenda por el pecado.
Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
9 Y haz que los levitas se adelanten frente a la tienda de reunión, y que todos los hijos de Israel se junten:
Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
10 Y debes llevar a los levitas ante el Señor, y los hijos de Israel deben poner sus manos sobre ellos:
Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
11 Y Aarón debe dar los levitas al Señor como una ofrenda de los hijos de Israel, para que puedan hacer la obra del Señor.
Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
12 Y los levitas deben poner sus manos sobre las cabezas de los becerros, y uno de los becerros debe ser ofrecido por una ofrenda por el pecado y el otro por una ofrenda quemada al Señor para quitar el pecado de los Levitas.
“Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
13 Entonces los levitas deben ser puestos delante de Aarón y sus hijos, para ser ofrecidos como una ofrenda al Señor.
Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
14 Así que debes separar a los levitas de los hijos de Israel, y los levitas serán míos.
Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
15 Después de eso, los levitas entrarán a hacer lo que sea necesario en la Tienda de reunión; Debes purificarlos y darlos como ofrenda mecida.
“Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
16 Porque me han sido dados de entre los hijos de Israel; En lugar del primer hijo de toda madre, el primero en nacer en Israel, los he tomado para mí.
Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
17 Porque el primer hijo de toda madre entre los hijos de Israel es mío, el primer nacimiento masculino de un hombre o una bestia: el día en que envié la muerte a todos los primeros hijos en la tierra de Egipto, los hice míos.
Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
18 Y en lugar de los primeros hijos entre los hijos de Israel, tomé a los levitas.
Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
19 Y se los he dado a Aarón y a sus hijos, de entre los hijos de Israel, para que emprendan por ellos toda la obra de la Tienda de reunión, y para quitar el pecado de los hijos de Israel para que no haya maldad sobre ellos cuando se acerquen al lugar santo.
Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
20 Todas estas cosas que Moisés y Aarón y los hijos de Israel hicieron a los levitas; como él Señor dio órdenes a Moisés acerca de los levitas, así lo hicieron los hijos de Israel.
Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
21 Y los levitas fueron y se purificaron del pecado, y sus ropas fueron lavadas, y Aarón los dio en ofrenda mecida delante del Señor; y Aarón quitó sus pecados y los purificó.
Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
22 Y luego los levitas entraron a hacer su trabajo en la tienda de reunión delante de Aarón y sus hijos: todas las órdenes que el Señor le había dado a Moisés acerca de los levitas se pusieron en práctica.
Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
23 Y él Señor dijo a Moisés:
Bwana akamwambia Mose,
24 Esta es la regla para los levitas: los de veinticinco años y más deben entrar y hacer el trabajo de la tienda de reunión;
“Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
25 Pero después de cumplir los cincuenta años, deben abandonar su trabajo y no hacerlo más;
lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
26 Pero servirán con sus hermanos en la Tienda de la reunión, cuidándolo pero sin hacer ningún trabajo. Esto es lo que debes hacer en relación con los levitas y su servicio.
Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”