< Números 33 >

1 Estos son los viajes de los hijos de Israel, cuando salieron de la tierra de Egipto en sus ejércitos, bajo la dirección de Moisés y Aarón.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Y las etapas de su viaje al salir fueron escritas por Moisés por orden del Señor: estas son las etapas de su viaje y la forma en que se fueron.
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 El decimoquinto día del primer mes salieron de Ramsés; El día después de la Pascua, los hijos de Israel salieron por el poder del Señor ante los ojos de todos los egipcios.
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 Mientras los egipcios colocaban en la tierra los cuerpos de sus hijos a quienes el Señor había enviado destrucción: y sus dioses habían sido juzgados por él.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Entonces los hijos de Israel salieron de Ramsés y pusieron sus tiendas en Sucot.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Y salieron de Sucot y levantaron sus tiendas en Etam, al borde del desierto.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Y desde Etam, volviendo a Pi-hahirot que está antes de Baal-zefón, levantaron sus tiendas antes de Migdol.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Y después de haber viajado desde delante de Hahiroth, atravesaron el mar hacia el desierto recorrieron tres días por el desierto de Etam y pusieron sus tiendas en Mara.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Y de Mara pasaron a Elim, y en Elim había doce manantiales de agua y setenta palmeras; y allí levantaron sus tiendas.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Y salieron de Elim y pusieron sus tiendas junto al Mar Rojo.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 Luego, desde el Mar Rojo, avanzaron y acamparon en el desierto de sin.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Y salieron del desierto de Sin, y pusieron sus tiendas en Dofca.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Y salieron de Dofca y pusieron sus tiendas en Alus.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Salieron de Alus y pusieron sus tiendas en Refidim, donde no había agua para el pueblo.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Y salieron de Refidim, y pusieron sus tiendas en el desierto del Sinaí.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Salieron de la tierra baldía de Sinaí y pusieron sus tiendas en Kibrot Hataava.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Salieron de Kibrot-hataava y pusieron sus tiendas en Hazerot.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Y se fueron de Hazerot, y pusieron sus tiendas en Ritma.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Y salieron de Ritma, y pusieron sus tiendas en Rimón -peres.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Y salieron de Rimón Peres, y pusieron sus tiendas en Libna.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Y se fueron de Libna y pusieron sus tiendas en Rissa.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Y se fueron de Rissa y pusieron sus tiendas en Ceelata.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Y salieron de Ceelata, y pusieron sus tiendas en el monte Sefer.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Salieron del monte Sefer y pusieron sus tiendas en Harada.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Salieron de Harada y pusieron sus tiendas en Macelot.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Y ellos se fueron de Macelot, y pusieron sus tiendas en Tahat.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Y ​​salieron de Tahat y pusieron sus tiendas en Taré.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Y se fueron de Taré y pusieron sus tiendas en Mitca.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Y salieron de Mitca y pusieron sus tiendas en Hasmona.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Y salieron de Hasmona y pusieron sus tiendas en Moserot.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Salieron de Moserot y pusieron sus tiendas en Bene-jaacan.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Y se fueron de Bene-jaacan, y pusieron sus tiendas en Gidgad.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Y se fueron de Gidgad, y pusieron sus tiendas en Jotbata.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Y salieron de Jotbata y levantaron sus tiendas en Abrona.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Y salieron de Abrona, y pusieron sus tiendas en Ezion-geber.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Y salieron de Ezión-geber y levantaron sus tiendas en el desierto de Zin (que es Cades).
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Y salieron de Cades y levantaron sus tiendas en el monte Hor, en el límite de la tierra de Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Entonces el sacerdote Aarón subió al monte por orden del Señor, y murió allí, en el cuadragésimo año después de que los hijos de Israel hubieran salido de la tierra de Egipto, en el quinto mes. El primer día del mes.
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 Aarón tenía ciento veintitrés años cuando murió en el monte Hor.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Y llegó la noticia de la venida de los hijos de Israel al rey de Arad, el cananeo, que vivía en el sur de la tierra de Canaán.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Y desde el monte Hor siguieron y pusieron sus tiendas en Zalmona.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Y salieron de Zalmona, y pusieron sus tiendas en Punón.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Y salieron de Punón, y pusieron sus tiendas en Obot.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Salieron de Obot y pusieron sus tiendas en Ije-abarim, al borde de Moab.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Y salieron de Ije-abarim pusieron sus tiendas en Dibon-gad.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Y de Dibón-gad continuaron y pusieron sus tiendas en Almón-diblataim.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Y de Almon-diblataim siguieron y levantaron sus tiendas en las montañas de Abarim, delante de Nebo.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Salieron de los montes de Abarim y acamparon en las llanuras de Moab, junto al Jordán en Jericó.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 Plantando sus tiendas al lado del Jordán desde Bet-jesimot hasta Abel-sitim en las tierras bajas de Moab.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Y en las llanuras de Moab, junto al Jordán en Jericó, el Señor dijo a Moisés:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 Di a los hijos de Israel: Cuando pases el Jordán a la tierra de Canaán,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 Mira que todas las personas de la tierra son expulsadas de ti, y destruyen todas sus piedras labradas, todas sus imágenes metálicas y todos sus lugares altos.
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Y tomen la tierra para ustedes, para su lugar de descanso: porque a ustedes les he dado la tierra como su herencia.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Y tomarás tu herencia en la tierra por la decisión del Señor, a cada familia su parte; cuanto mayor sea la familia, mayor será su patrimonio, y cuanto más pequeña sea la familia, menor será su patrimonio; dondequiera que la decisión del Señor dé a cualquier hombre su parte, esa será suya; Las tribus de tus padres te harán la distribución.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 Pero si demoras en expulsar a la gente de la tierra, entonces aquellos de los que todavía están allí serán como puntos de alfiler en tus ojos y como espinas en tus costados, molestándote en la tierra donde estás habitando.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 Y sucederá que tal como fue mi propósito hacerles, así te haré a ti.
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Números 33 >