< Números 31 >

1 Entonces el SEÑOR dijo a Moisés:
Bwana akamwambia Mose,
2 Da a los madianitas el castigo por el mal que hicieron a los hijos de Israel: y después de eso serás recogido a tu pueblo, morirás.
“Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
3 Entonces Moisés dijo al pueblo: Que los hombres de entre ustedes estén armados para la guerra para poner en práctica el castigo de Madián el Señor.
Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
4 De cada tribu de Israel envía mil a la guerra.
Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
5 Así, de los miles de Israel se tomaron mil de cada tribu, doce mil hombres armados para la guerra.
Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
6 Y Moisés los envió a la guerra, mil de cada tribu, y con ellos Finees, el hijo del sacerdote Eleazar, tomando en sus manos los vasos del lugar santo y los cuernos para hacer sonar la nota de la guerra.
Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
7 E hicieron guerra contra Madián, como el Señor le dio órdenes a Moisés; y matan a todos los varones.
Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
8 Ellos mataron a los reyes de Madián con el resto, Evi y Requem y Zur y Hur y Reba, los cinco reyes de Midian; y Balaam, el hijo de Beor, los mataron con la espada.
Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
9 Las mujeres de Midian con sus pequeños los hijos de Israel tomaron prisioneras; y tomaron para sí todos sus ganados y sus rebaños y todos sus bienes;
Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
10 Y después de quemar todos sus pueblos y todos sus campamentos de tiendas,
Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
11 Se fueron con los bienes que habían tomado, hombre y bestia.
Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
12 Y los prisioneros y los bienes y todo lo que habían tomado, llevaron a Moisés y al sacerdote Eleazar y al pueblo de Israel, al campamento de tiendas de campaña en las tierras bajas de Moab, junto al Jordán en Jericó.
nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
13 Entonces Moisés y el sacerdote Eleazar y los jefes de la gente salieron a ellos antes de entrar en el campamento de la tienda.
Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
14 Y Moisés se enojó con los jefes del ejército, los capitanes de miles y los capitanes de cientos que habían regresado de la guerra.
Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
15 Y Moisés les dijo: ¿Por qué habéis salvado a todas las mujeres?
Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
16 Fueron éstas quienes, por él consejo Balaam, fueron la causa del pecado de Israel contra el Señor en la cuestión de Baal-Peor, debido a la enfermedad que afectó a la gente del Señor.
“Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
17 Así que ahora da muerte a cada hijo varón, y a toda mujer que haya tenido relaciones sexuales con un hombre.
Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
18 Pero todas las niñas que no han tenido relaciones sexuales con hombres, pueden quedarse con ustedes.
lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
19 Ustedes mismos deberán mantenerse fuera del campamento de la tienda durante siete días, cualquiera de ustedes que haya matado a una persona o se haya acercado a un cadáver; y en el tercer día y en el séptimo día hagan que ustedes y sus prisioneros se purifiquen.
“Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
20 Y toda ropa, y cualquier cosa hecha de cuero o pelo de cabra o madera, debes limpiarla.
Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
21 Entonces el sacerdote Eleazar dijo a los hombres de guerra que habían estado en la lucha: Esta es la ley, de la ley que el Señor ha dado a Moisés:
Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
22 Más oro y plata y latón, hierro y estaño y plomo.
Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
23 Y cualquier cosa que pueda ser calentada, es pasar por el fuego y ser limpiada; pero además se debe poner en el agua de la purificación, y cualquier cosa que no pase por el fuego se debe poner en el agua.
na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
24 Y en el séptimo día, después de lavar tu ropa, estarás limpio, y luego podrás entrar en el campamento de la tienda.
Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
25 Y él Señor dijo a Moisés:
Bwana akamwambia Mose,
26 Obtenga una cuenta de todo lo que se tomó en la guerra, del hombre y de la bestia, tú y el sacerdote Eleazar y los jefes de las familias de la gente.
“Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
27 Y ​​que la división se haga en dos partes, una para los hombres de guerra que salieron a la lucha, y otra para todo el pueblo.
Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
28 Y de los hombres de guerra que salieron, se ofrezca al Señor uno de cada quinientos, de las personas, y de los becerros, asnos y ovejas.
Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
29 Toma esto de su parte y dáselo al sacerdote Eleazar como ofrenda para ser elevado al Señor.
Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
30 Y de la parte dada a los hijos de Israel, toma uno de cada cincuenta, de las personas, y de los bueyes y asnos y ovejas, y dáselo a los levitas que tienen el cuidado de la Casa de los Señor.
Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
31 Entonces Eleazar y Moisés hicieron lo que el Señor le había ordenado a Moisés.
Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Las bestias capturadas, además de lo que los guerreros tomaron para sí, eran seiscientas setenta y cinco mil ovejas,
Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
33 Y setenta y dos mil bueyes,
ngʼombe 72,000,
34 Y sesenta y un mil asnos;
punda 61,000,
35 Y treinta y dos mil personas, es decir, mujeres que nunca habían tenido relaciones sexuales con un hombre.
na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
36 Y la mitad entregada a los hombres que fueron a la guerra, fue de trescientos treinta y siete mil quinientas ovejas.
Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
37 De los cuales la parte del Señor era seiscientos setenta y cinco.
ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
38 El número de bueyes era treinta y seis mil, de los cuales la parte del Señor era setenta y dos;
ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
39 El número de asnos fue treinta mil quinientos, de los cuales la parte del Señor era sesenta y uno.
punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
40 Y el número de personas era dieciséis mil, de las cuales la parte del Señor era treinta y dos personas.
Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
41 Entonces Moisés dio la parte del Señor, que se levantó como ofrenda, al sacerdote Eleazar, como el Señor le había dado órdenes a Moisés.
Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
42 Y de la mitad dada a los hijos de Israel, que Moisés había mantenido separada de la que se daba a los combatientes,
Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
43 La mitad del pueblo era trescientos treinta y siete mil quinientas ovejas,
nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
44 Y treinta y seis mil bueyes.
ngʼombe 36,000,
45 Y treinta mil quinientos asnos,
punda 30,500,
46 Y dieciséis mil personas;
na wanadamu 16,000.
47 Incluso de la mitad de los hijos de Israel, Moisés tomó uno de cada cincuenta hombres y bestias, y se los dio a los levitas que cuidaban de la Tienda del Señor; como el SEÑOR dio órdenes a Moisés.
Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
48 Entonces los hombres en autoridad sobre los miles del ejército, los capitanes de miles y los capitanes de cientos vinieron a Moisés.
Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
49 Y le dijeron: Tus siervos han tomado nota del número de todos los combatientes bajo nuestras órdenes, y todos están presentes;
na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
50 Y aquí tenemos una ofrenda para el Señor de lo que cada hombre tomó en la guerra, adornos de oro, cadenas para las piernas y anillos para los brazos, anillos para los dedos, aretes y adornos para el cuello, para hacer nuestra Almas libres del pecado delante del Señor.
Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
51 Y Moisés y el sacerdote Eleazar les quitaron el oro, y todos los ornamentos trabajados.
Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
52 Y el oro que los capitanes de miles y los capitanes de cientos dieron, como ofrenda para ser levantados delante del Señor, llegó a dieciséis mil setecientos cincuenta siclos.
Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
53 Porque cada hombre del ejército había tomado bienes para sí mismo en la guerra.
Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
54 Entonces Moisés y el sacerdote Eleazar tomaron el oro dado por los capitanes de miles y capitanes de cientos, y lo llevaron a la Tienda de la reunión, para ser una señal en memoria de los hijos de Israel ante el Señor.
Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.

< Números 31 >