< Números 29 >

1 En el séptimo mes, el primer día del mes, que haya una reunión santa; en él no podrás hacer trabajo de campo; Que el día sea marcado por el soplar de cuernos;
“‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
2 Y da al Señor una ofrenda quemada por aroma dulce; Un becerro, un carnero, siete corderos del primer año, sin ningún defecto en ellos:
Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
3 Y su ofrenda de cereales, la mejor harina mezclada con aceite, tres décimas partes para un buey, dos décimas partes para un carnero,
Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
4 Y una décima parte separada para cada uno de los siete corderos;
na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
5 Y un chivo para el sacrificio por el pecado, para quitar tu pecado.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
6 Además de la ofrenda quemada de la luna nueva, y su ofrenda de cereales, y la ofrenda quemada regular y su ofrenda de cereales, y sus ofrendas de bebidas, según se les ordena, para un aroma dulce, una ofrenda hecha por fuego al Señor.
Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
7 Y en el décimo día de este séptimo mes habrá una reunión santa; manténganse del placer y no hagan ningún tipo de trabajo;
“‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
8 Y da al Señor una ofrenda quemada por un aroma dulce; un becerro, un carnero, siete corderos del primer año, solo se pueden usar aquellos sin ningún defecto:
Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
9 Y su ofrenda de cereales, la mejor harina mezclada con aceite, tres décimas partes para un buey, dos décimas partes para un carnero,
Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
10 Una décima parte separada para cada uno de los siete corderos;
na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
11 Un chivo para el sacrificio por el pecado; además de la ofrenda por quitar tu pecado, y la ofrenda quemada regular y su ofrenda de cereales, y sus ofrendas de bebida.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
12 Y a los quince días del mes séptimo, habrá una reunión santa; no haga trabajos de campo, y celebrarán una fiesta al Señor durante siete días;
“‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
13 Y ofrenda quemada, ofrenda encendida de aroma dulce al Señor, trece becerros, dos carneros, catorce corderos del primer año, todos sin ningún defecto;
Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
14 Y su ofrenda de cereales, la mejor harina mezclada con aceite, tres décimas partes por cada uno de los trece becerros, dos décimas partes por cada carnero,
Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
15 Y una décima parte por cada uno de los catorce corderos;
na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
16 Y un chivo para el sacrificio por el pecado; además de la ofrenda quemada regular, y su ofrenda de cereales, y su ofrenda de bebida.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
17 En el segundo día de la fiesta, ofrenda doce becerros, dos carneros, catorce corderos del primer año, sin ningún defecto en ellos;
“‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
18 Y su ofrenda de comida y sus ofrendas de bebida para los bueyes y las ovejas y los corderos, en relación con su número, como se ordena:
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
19 Y un chivo para el sacrificio por el pecado, además de la ofrenda quemada regular, y su ofrenda de cereales, y sus ofrendas de bebida.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
20 Y al tercer día once becerros, dos carneros, catorce corderos del primer año, sin ningún defecto;
“‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
21 Y su ofrenda de cereales y ofrendas de de los becerros, los carneros, y para los corderos, en relación con su número, como se ordena.
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
22 Y un chivo para el sacrificio por el pecado; además de la ofrenda quemada regular, y su ofrenda de cereales, y su ofrenda de bebida.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
23 Y al cuarto día, diez bueyes, dos ovejas, catorce corderos del primer año, sin ningún defecto:
“‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
24 Y su ofrenda de cereales y sus ofrendas de bebida para los becerros, para los carneros, y para los corderos, en relación con su número, como se ordena.
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
25 Y un chivo para el sacrificio por el pecado; además de la ofrenda quemada regular, y su ofrenda de cereales, y su ofrenda de bebida.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
26 Y en el quinto día nueve becerros, dos carneros, catorce corderos del primer año, sin ningún defecto:
“‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
27 Y ​​su ofrenda de comida y sus ofrendas de bebida para los bueyes, para las ovejas y para los corderos, en relación con su número, como se ordena:
Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
28 Y un chivo para el sacrificio por el pecado; además de la ofrenda quemada regular, y su ofrenda de cereales, y su ofrenda de bebida.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
29 Y en el sexto día ocho becerros, dos carneros, catorce corderos del primer año, sin ningún defecto.
“‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
30 Y su ofrenda de cereales y sus ofrendas de bebida para los becerros, para los carneros, y para los corderos, en relación con su número, como se ordena:
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
31 Y un chivo para el sacrificio por el pecado; además de la ofrenda quemada regular, su ofrenda de cereales y sus ofrendas de bebida.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
32 Y al séptimo día, siete becerros, dos carneros, catorce corderos del primer año, sin ningún defecto:
“‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
33 Y su ofrenda de cereales y sus ofrendas de bebida para los becerros, para los carneros, y para los corderos, en relación con su número, como se ordena:
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
34 Y un chivo para el sacrificio por el pecado; además de la ofrenda quemada regular, su ofrenda de cereales y su ofrenda de bebida.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
35 Al octavo día, hágase una reunión santa: no puede hacer trabajo de campo;
“‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
36 Y ofrenda quemada, ofrenda encendida de aroma dulce al Señor: un becerro, un carnero, siete corderos del primer año, sin ningún defecto.
Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
37 Con la ofrenda de cereales y las ofrendas de bebida para el becerro, un carnero y los corderos, en relación con su número, como se ordena:
Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
38 Y un chivo para el sacrificio por el pecado; además de la ofrenda quemada regular, y su ofrenda de cereales, y su ofrenda de bebida.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
39 Estas son las ofrendas que debes entregar al Señor en tus fiestas regulares, además de las ofrendas para un juramento y las ofrendas gratuitas que das, por tus ofrendas quemadas y tus ofrendas de bebidas y tus ofrendas de paz.
“‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
40 Entonces Moisés les dio a los hijos de Israel todas estas instrucciones como el Señor le había ordenado.
Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.

< Números 29 >