< Nehemías 12 >
1 Estos son los sacerdotes y los levitas que subieron con Zorobabel, el hijo de Salatiel, y Josué: Seraías, Jeremías, Esdras,
Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
3 Secanías, Rehum, Meremot,
Shekania, Rehumu, Meremothi,
5 Mijamin, Maadias, Bilga,
Miyamini, Moadia, Bilga,
6 Semaías, y Joiarib, Jedaías.
Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 Salu, Amoc, Hilcias, Jedaias. Estos fueron los jefes de los sacerdotes y de sus hermanos en los días de Josué.
Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
8 Y los levitas: Josué, Binuy, Cadmiel, Serebias, Judá, y Matanias, que estaban encargados de la accion de gracias, él y sus hermanos.
Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
9 Y Bacbuquias y Uni, sus hermanos, estaban frente a ellos para el desempeño de sus guardas.
Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
10 Y Josué fue el padre de Joiacim, y Joiacim fue el padre de Eliasib, y Eliasib fue el padre de Joiada.
Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
11 Y Joiada fue el padre de Johanan, y Johanan fue el padre de Jadua.
Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
12 Y en los días de Joacim había sacerdotes, jefes de familia: de Seraías, Meraías; de Jeremías, Hananías;
Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
13 De Esdras, Mesululam; de Amarias, Johanán;
wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
14 De Malicu, Jonatán; de Sebanías, José;
wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
15 De Harim, Adna; de Meraiot, Helcai;
wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
16 De Ido, Zacarías; de Gineton, Mesulam;
wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
17 De Abías, Zicri; de Miniamin, de Moadias, Piltai;
wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
18 De Bilga, Samua; de Semaías, Jonatan;
wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
19 Y de Joiarib, Matenai; de Jedaias, Uzi;
wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
20 De Salai, Calai; de Amoc, Eber;
wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
21 De Hilcías, Hasabías; de Jedaias, Natanael.
wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
22 Los levitas en los días de Eliasib, Joiada, Johanan y Jadua, fueron catalogados como jefes de familia; y los sacerdotes, cuando Darío el persa era rey.
Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
23 Los hijos de Leví, jefes de familia, fueron registrados en el libro de las crónicas, incluso hasta los días de Johanán, el hijo de Eliasib.
Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
24 Y los jefes de los levitas: Hasabías, Serebias y Josué, el hijo de Cadmiel, con sus hermanos frente a ellos, para bendecir y alabar a Dios según lo ordenó David, el hombre de Dios, durante su respectivo turno de servicio.
Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
25 Matanias, y Bacbuquias, Obadias, Mesulam, Talmon, Acub, eran porteros que vigilaban las puertas de los almacenes.
Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
26 Estos fueron en los días de Joacim, el hijo de Josué, el hijo de Josadac, y en los días de Nehemías el gobernador y Esdras el sacerdote, el escriba.
Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
27 Y cuando llegó el momento de santificar el muro de Jerusalén, enviaron a los levitas de todos sus lugares para que vinieran a Jerusalén, para celebrar la fiesta de dedicación y acción de gracias con alegría, con alabanza y melodía, con címbalos, arpas y liras.
Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
28 Y los hijos de los cantores se reunieron desde las tierras bajas alrededor de de las aldeas de los netofatitas,
Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
29 Y de Bet-gilgal y de los campos de Geba y Azmavet: porque los cantores habían hecho aldeas alrededor de Jerusalén.
kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
30 Y los sacerdotes y los levitas se purificaron; e hicieron purificar a la gente, y las puertas de la ciudad y la muralla.
Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
31 Entonces hice que los gobernantes de Judá subieran a la muralla, y puse en posición dos grandes bandas de ellos que alababan, caminando en líneas ordenadas; uno fue a la derecha en la pared, en dirección a la puerta donde se colocaron los desechos;
Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
32 Y después de ellos fueron Osaias y la mitad de los gobernantes de Judá.
Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
33 Y Azarías, Esdras y Mesulam,
pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
34 Judá y Benjamín y Semaías y Jeremías,
Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
35 Y algunos de los hijos de los sacerdotes con instrumentos de viento; Zacarías, hijo de Jonatán, hijo de Semaías, hijo de Matanías, hijo de Micaías, hijo de Zacur, hijo de Asaf,
pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
36 Y sus hermanos, Semaías, y Azarel, Milalai, Gilalai, Maai, Natanael, Juda y Hanani, con los instrumentos musicales de David, el hombre de Dios; y Esdras el escriba estaba a la cabeza;
pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
37 Y junto a la entrada de la fuente y directamente delante de ellos, subieron por los escalones de la ciudad de David, en la pendiente de la pared, sobre la casa de David, hasta la puerta del Agua hacia el este.
Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
38 Y la otra banda de los que alababan iba a la izquierda, y yo fui tras ellos con la mitad de la gente, en la pared, sobre la torre de los hornos, hasta la pared ancha;
Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
39 Y sobre la puerta de Efraín y junto a la puerta vieja y la puerta de los Peces y la torre de Hananeel y la torre de los Cien, hasta la puerta de las Ovejas: y en la puerta de los Guardias se detuvieron.
juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
40 Así que las dos bandas de los que dieron alabanza tomaron sus posiciones en el templo de Dios, y yo y la mitad de los jefes conmigo:
Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
41 Y los sacerdotes; Eliacim, Maaseias, Miniamin, Micaias, Elioenai, Zacarías, y Hananias, con instrumentos de viento;
na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
42 Y Maasias y Semaías y Eleazar y Uzi y Johanan y Malquias y Elam y Ezer. Y los cantores, supervisados por Jezrahiah, alzaron sus cantos en voz alta.
na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
43 Y aquel día hicieron grandes ofrendas y se alegraron; porque Dios los había alegrado con gran gozo; y las mujeres y los niños se alegraron con ellos, de modo que la alegría de Jerusalén llegó a oídos de los que estaban lejos.
Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
44 Y ese día pusieron a algunos hombres sobre las habitaciones donde estaban almacenadas las cosas que habían sido dadas, por las ofrendas y los primeros frutos y las décimas, que conforme a la ley llegaban las cantidades, de los campos de Cada pueblo, fijado por la ley para los sacerdotes y los levitas, porque Judá se alegró a causa de los sacerdotes y los levitas que estaban en sus lugares.
Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
45 Y ellos guardaban la ordenanza de la purificación y culto a su Dios, y fueron responsables de purificar las cosas, y también lo hicieron los cantores y los encargados de las puertas, como lo ordenaron David y Salomón, su hijo.
Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
46 Porque en los días de David y Asaf en el pasado, había un maestro de la música, de cantos de agradecimiento y alabanza a Dios.
Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
47 Y todo Israel en los días de Zorobabel y en los días de Nehemías dio lo que necesitaban a los cantores y los encargados de las puertas día tras día: e hicieron santos los ofrecimientos para los levitas; y los levitas hicieron lo mismo con los hijos de Aarón.
Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.