< San Mateo 26 >
1 Y cuando Jesús hubo terminado todas estas palabras, dijo a sus discípulos:
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
2 Dentro de dos días es la Pascua, y el Hijo del hombre será entregado para ser crucificado.
“Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
3 Entonces los principales sacerdotes y los escribas y los ancianos del pueblo se juntaron en la casa del sumo sacerdote, que se llamaba Caifás.
Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
4 E hicieron planes juntos para arrestar a Jesús con engaños y matarlo.
Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
5 Pero ellos dijeron: No durante la fiesta, para que no se alborote la gente.
Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
6 Cuando Jesús estaba en Betania, en casa de Simón el leproso,
Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
7 Vino a él una mujer que tenía una botella de perfume muy costoso, y ella le puso el perfume sobre la cabeza cuando estaba sentado a la mesa.
naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
8 Pero cuando los discípulos lo vieron, se enojaron, diciendo: ¿Para qué se desperdicia esto?
Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
9 Porque pudo haberse vendido por mucho dinero y dárselo a los pobres.
Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
10 Pero al ver Jesús, les dijo: ¿Por qué molestas a la mujer? ella me ha hecho un acto amable.
Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
11 Porque a los pobres siempre los tendrán con ustedes, pero a mí no siempre me tendrán.
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
12 Porque al poner este perfume en mi cuerpo, lo hizo para prepararme para mi sepultura.
Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
13 De cierto, de cierto les digo: Dondequiera que se divulguen estás buenas nuevas en todo el mundo, se hablará de lo que hizo esta mujer en memoria de ella.
Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
14 Entonces uno de los doce, que se llamaba Judas Iscariote, fue a los principales sacerdotes,
Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
15 Y les dijo: ¿Qué me darán, si les entrego a Jesus? Y ellos señalaron el precio en treinta monedas de plata.
na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
16 Y a partir de ese momento él estaba esperando la oportunidad de entregarlo en sus manos.
Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu.
17 El primer día de los panes sin levadura, los discípulos se acercaron a Jesús y le dijeron: ¿Dónde debemos preparar para que comas la Pascua?
Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
18 Y él les dijo: vayan a la ciudad de cierto hombre, y dile: El Maestro dice: Mi tiempo está cerca: celebraré la pascua en tu casa con mis discípulos.
Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”
19 Y los discípulos hicieron como Jesús les había dicho; y prepararon la Pascua.
Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile Yesu alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
20 Cuando llegó la noche, estaba sentado a la mesa con los doce discípulos;
Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
21 Y mientras comían, dijo: De cierto les digo que alguno de ustedes me va a traicionar.
Nao walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
22 Y entristecidos en gran manera empezaron a preguntar un tras otro: ¿Soy yo, Señor?
Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
23 Y él respondió y dijo: El que mete su mano en el plato conmigo, me traicionara.
Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
24 A la verdad, el Hijo del Hombre va, como dicen las Escrituras acerca de él; pero la maldición está sobre aquel hombre por quien el Hijo del Hombre es entregado; hubiera sido bueno para ese hombre si nunca hubiera nacido.
Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
25 Y Judas, él que lo entregaba, respondió y dijo: ¿Soy yo, Maestro? Él le dice: tú lo has dicho.
Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
26 Cuando estaban comiendo, Jesús tomó pan y, después de bendecirlo, les dio el pan partido a los discípulos y les dijo: Tómalo; este es mi cuerpo.
Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
27 Y tomando una copa, bendiciendo, se las dio, diciendo:
Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
28 Tomen todos, porque esta es mi sangre de nuevo pacto, que es dada a los hombres para el perdón de sus pecados.
Hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
29 Pero yo os digo que de ahora en adelante no tomaré de este fruto de la vid, hasta el día en que beba con ustedes él vino nuevo en el reino de mi Padre.
Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30 Y después de un canto de alabanza a Dios, salieron al monte de los Olivos.
Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
31 Entonces Jesús les dijo: Todos ustedes se apartaran de mí esta noche; porque está dicho en las Escrituras: Daré muerte al pastor de las ovejas, y las ovejas del rebaño serán dispersadas.
Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
32 Pero después que haya resucitado de entre los muertos, iré delante de ustedes a Galilea.
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
33 Entonces Pedro respondió, y le dijo: Aunque todos te nieguen, yo nunca te negaré.
Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
34 Jesús le dijo: De cierto te digo que esta noche, antes de la hora del grito del gallo, dirás tres veces que no me conoces.
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 Pedro le responde: Aunque me maten contigo, no te negaré. Así lo dijeron todos los discípulos.
Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 Luego viene Jesús con ellos a un lugar llamado Getsemaní, y les dice a sus discípulos: “Siéntense aquí, mientras yo voy allí a orar”.
Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
37 Y tomó consigo a Pedro y a los dos hijos de Zebedeo, y se entristeció y se turbó en gran manera.
Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
38 Entonces él les dice: Mi alma está muy triste, hasta la muerte; velen conmigo aquí.
Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
39 Y él se adelantó un poco, y postrándose en su rostro en oración, dijo: Padre mío, si es posible, pase de mí esta copa; pero no sea como yo quiero, sino como tu quieras.
Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
40 Y vino a los discípulos, y los ve que están durmiendo, y dice a Pedro: ¿Qué? ¿No pudiste velar conmigo una hora?
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
41 Velen y oren, para que no entren a prueba: el espíritu verdaderamente está listo, pero la carne es débil.
Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
42 Una vez más, se fue por segunda vez, y dijo en oración: Padre mío, si esto no puede pasar de mí sin que yo lo tome, que se haga tu voluntad.
Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
43 Y vino otra vez y los vio durmiendo, porque sus ojos estaban cansados.
Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
44 Y se fue de ellos otra vez, y una tercera vez dijo la misma oración.
Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
45 Entonces él viene a los discípulos; y les dice: Duerman ahora, y descansen: porque la hora ha llegado, y el Hijo del hombre es entregado en manos de hombres malos.
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
46 Arriba, vayamos: mira, el que me traiciona está cerca.
Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
47 Mientras él aún hablaba, vino Judas, uno de los doce, y con él una banda armada con espadas y palos, de parte de los principales sacerdotes y de los ancianos del pueblo.
Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
48 Ahora el que lo entregaba les había dado una señal que decía: Aquel a quien doy un beso, ése es él: arrestenlo.
Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
49 Y enseguida vino a Jesús y le dijo: ¡Maestro! y le dio un beso.
Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
50 Y Jesús le dijo: Amigo, haz aquello por lo que has venido. Luego vinieron y pusieron sus manos sobre Jesús, y lo arrestaron.
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.
51 Y uno de los que estaban con Jesús extendió su mano, y sacó su espada, y le dio un golpe al siervo del sumo sacerdote, y le cortó la oreja.
Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
52 Entonces Jesús le dice: Vuelve a poner tu espada en su lugar; porque todos los que tomen la espada, morirán a espada.
Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
53 ¿No te parece posible que si le ruego a mi Padre, incluso ahora me envíe doce legiones de ángeles?
Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 ¿Pero cómo se cumplirian las Escrituras, que dicen que así debe ser?
Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
55 En esa hora, Jesús dijo a la gente: ¿Has salido como un ladrón con espadas y palos para llevarme? Yo enseñaba todos los días en el Templo y tú no me llevabas.
Wakati huo, Yesu akawaambia ule umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
56 Pero todo esto ha sucedido para que las escrituras de los profetas se hagan realidad. Entonces todos sus discípulos dejándole huyeron.
Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
57 Y los que habían hecho prisionero a Jesús lo llevaron a la casa de Caifás, el sumo sacerdote, donde los escribas y los que tenían autoridad sobre el pueblo se habían reunido.
Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
58 Pero Pedro lo siguió a lo lejos, a la casa del sumo sacerdote, y entró y se sentó con los criados para ver el fin.
Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
59 Y los principales sacerdotes y todo el Sanedrín buscaban falso testimonio contra Jesús, para que lo mataran;
Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.
60 Y no lo hallaron, aunque vinieron varios testigos falsos.
Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
61 Pero luego vinieron dos que dijeron: Este dijo: Yo puedo destruir el templo de Dios y reedificar en tres días.
na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”
62 Entonces el sumo sacerdote se levantó y le dijo: ¿No tienes respuesta? ¿Qué es lo que estos dicen contra ti?
Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
63 Pero Jesús no dijo una palabra. Y el sumo sacerdote le dijo: Te juro por el Dios viviente que nos digas si eres el Cristo, el Hijo de Dios.
Lakini Yesu akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
64 Jesús le dice: Tú lo dices; pero yo les digo: Desde ahora verán al Hijo del hombre sentado a la diestra del poder de Dios y viniendo sobre las nubes del cielo.
Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 Entonces el sumo sacerdote, partiéndose violentamente sus vestiduras, dijo: Dijo mal contra Dios: ¿qué más necesidad tenemos de testigos? porque ahora han llegado a sus oídos sus palabras contra Dios:
Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia hayo makufuru.
66 ¿Cuál es su opinión? Respondieron y dijeron: “Está bien que lo maten”.
Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
67 Entonces le escupieron en el rostro, le dieron de puñetazo y otros le abofeteaban, avergonzaron, diciendo:
Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
68 ¡Sé profeta, oh Cristo, y di quien te dio un golpe!
na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
69 Y Pedro estaba sentado en la plaza abierta fuera de la casa; y una criada se le acercó, y le dijo: Tú estabas con Jesús el Galileo.
Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70 Pero Pedro lo negó delante de todos, diciendo: no sé lo que dices.
Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
71 Y cuando salió a la puerta, otra lo vio y dijo a los que estaban allí: Este hombre estaba con Jesús el Nazareno.
Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
72 Y otra vez dijo con un juramento, no conozco al hombre.
Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
73 Y pasado un tiempo, los que estaban cerca vinieron y dijeron a Pedro: Verdaderamente tú eres uno de ellos; porque tu acento te descubre.
Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
74 Luego, con maldiciones y juramentos, dijo: No conozco al hombre. Y de inmediato vino el grito de un gallo.
Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
75 Y la palabra de Jesús regresó a Pedro, cuando dijo: Antes de la hora del grito del gallo, dirás tres veces que no me conoces. Y salió, llorando amargamente.
Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.